Condoleezza Rice: Kim Jong Un is pretty clever


Mkuu Malcom Lumumba ndiyo maana mimi siku zote nimekuwa nikiamini kwamba South and North Korea ni projects zilizosukwa kimkakati. They agreed/decided to divide in order to advance and contain.
Haya mataifa yenye umri mkubwa (1000+ years) huwa wana akili zilizo beba maono ya mbali sana. Na mikakati yao ni kuvivusha na kuvijenga vizazi vyao siyo class fulani. Hivyo mataifa kama China, Korea kusini na Kaskazini wanaweza kufanya lolote kwa ajili ya vizazi vyao.
Kuna series niliwahi pata kuiangalia kuna kakipande kadogo mno kwenye moja ya Episode kanaonyesha namna usiri mkuu uliopo baina ya mataifa haya ukikaangalia kwa akili nzuri utaona kuna mikakati ilishatengenezwa kabla hata hawajafarakana ni namna gani watakuja kuungana huko mbele. Na kuna watu wanahakikisha mgogoro unakua mkubwa kwa gharama yoyote ile lakini hii yote ni mbinu tu.
Korea Kaskazini ni mbeba msalaba lakini lastly hawa kuna kitu wanamchota mzungu.
 

Nakubaliana na wewe kaka na nategemea iwe kama ulivyosema,
Kuna kitu nimekiongezea hapo juu kiangalie.
Kinachoniegopesha ni kwamba nyakati zimebadilika sana tofauti na miaka ya nyuma.
Dunia imefungamanika sana kipindi hiki kuliko nyakati zozote zile katika historia ya binadamu.
Kitakachotokea Korea kule mbali kabisa kinauwezo mkubwa sana wa kutuathiri mimi na wewe kwa namna moja au nyingine

Upande wa pili,
Haya mataifa makubwa yanapenda kabisa hizi Korea ziungane tokea imepata Uhuru toka kwa Japani,
Lakini mwisho wa siku swali la Msingi linakuja "Hizi Korea zikishaungana ni kwa faida na hasara ya nani ??"
Linapokuja swali gumu kama hili ndiyo mambo mazito ya Balance of Power yanaingia hapa na wanaanza kuvutana tena.

Mfano Mzuri ni kwamba Bara la Ulaya mpaka leo wanapenda sana kuungana na kuwa nchi moja kaa ilivyokuwa kipindi cha Mfalme Justine au Mfalme Charlemagne wa dola Rumi. Wazungu wa Ulaya na akili zao zote walijaribu kufanya kila aina ya mbinu lakini mwisho wa siku ni Urusi na Marekani ndiyo kikwazo kwasababu wanajua Ulaya iliyoungana ni hatari sana kwa ushawishi wa Urusi na Marekani. Hivyo kila mtu anazuia huu muungano na pia anataka Bara la Ulaya liungane likiwa upande wake yeye binafsi.

Kina kipindi UN walipendekeza baadhi ya nchi kama Ujerumani, Brazil, India na AU wapewe kura za VETO kwenye Baraza la Ulinzi la Umoja wa Mataifa lakini taharuki ilikuwa kubwa sana. Swali ni hili: Je, kama Marekani na Urusi wana nia njema na ustawi wa mataifa na amani ya dunia kwanini wapinge kwa kiasi kikubwa wengine kuwa na VETO ??
Jibu ni rahisi tu, Ule mpango utavuruga BALANCE OF POWER Kwasababu mwaka 1972 walifanya jaribio la kumpa Uchina kura ya VETO badala ya nchi ya TAIWAN lakini leo wanajuta. Sasa wampe nchi nyingine kama Ujerumani lazima itakula kwao.

NB: Hoja nayotaka niiseme hapa ni kwamba haya mataifa makubwa hayafurahii ustawi wa hizi nchi nyingine huku yakiona maslahi yao yanaharibika. Marekani, Urusi na Uchina kama yanakubaliana na huu mjadala ni lazima basi yanapata maslahi ya moja kwa moja (Hakuna cha bure): maana tokea mwaka 1945 hadi leo Warusi, Wachina na Wamarekani wametupa mabilioni ya fedha nchi Korea (Kaskazini na Kusini) na wanajeshi wao wamekufa sana kwenye vita za Korea, ni lazima wanategemea kitu cha manufaa ya kiusalama au kibiashara.
 
Nadhani wewe bado sana. Hujui hata kiswahili
Badala ya kuandika neno "ivoo" andika "hivyo"
Badala ya kuandika "sio" andika "siyo"
Elimu ya bure hiyo dogo.


lakini ujumbe umefika si ndio. Kwanza unauwakika gani mm mtanzania au laa? As long as message sent and delivered thats what matters, grammatical errors potezea
 
Shitholer unawaza sura badala ya point anazoongea.. watu weusi mnawazaga ngono tu.
SASA KATI YA MM NA WW NANI ANAWAZA NGONO, MAANA INAONESHA ICHO NDICHO KIPO AKILINI MWAKO NDO MAANA UMELIGUSIA. PIA HII PLATFORM NI HURU, ACHA WENGE!
 
Urais wa USA siku hizi umekua kwa watu shitholes/assholes kama "Trump"

Vichwa wamekaa pembeni wanamcheki tu.
Kama hapa kwetu jinsi vichwa walivyokaa pemben..wanamchek tuu uncle padlock
 
Madeline Albright ndio alikuwa the best sema alikuwa na Clinton ambaye alikuwa mpole.
Yaa naye alikuwa vizuri sana, Condoleezza Rice amefanya kazi kwenye mazingira magumu sana kipindi cha vita ya Iraq baada ya Collin Powel kujiuzuru.Kipindi hiki dunia ilikuwa imegawanyika kutokana na uvamizi wa marekani nchini Iraq.Lakini huyu mama alijitahidi sana kufanya kazi yake, moja ya kazi zake za kukumbukwa ni ile ya kusuluhisha mgogoro wa Kenya, pia ni kuzuia jaribio la North korea ya baba yake Kim Jong Un kuunda silaha za Nyukilia
 
samahani ndugu nisahihishe...drone hazikufika kambini
 

Hahahaha,
Madeline Albright na Clinton walifanya mambo ambayo yamaiponza Marekani leo hii.
Walishauriwa sana kuhusiana na kutanua NATO, kusaidia waasi Chechenya na kuvamia Yogoslavia lakini wakagoma.
Hawa wamaza wawili hawana utofauti wowote ule (In their sense of Belligerency), leo hii Urusi kawa mbogo kisa sera zao.

Yaani baada ya vita Baridi kuisha,
Marekani imekuwa na majanga mazito kwenye Diplomasia.
Yugoslavia blunder, Afghanistan Blunder, Iraq Blunder, Syria Blunder, Libya Blunder, Ukraine Blunder.
Yaani ni Quagmire After Quagmire..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…