Coaster za Mbeya - Dar@Hakuna Kulala

Coaster za Mbeya - Dar@Hakuna Kulala

Kassim Awadh

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2012
Posts
884
Reaction score
187
Wakuu kuna huu usafiri wa Mbeya - Dar kwa kutumia Coaster wenyewe wanaziita hakuna kulala, Zinaanzia Uyole pale jijini mbeya na kwa Dar zinapakilia Kidongo Chekundu, Zinaondoka around saa 9&10 jioni sehemu kubwa ya safari ni usiku, ni usafiri usio rasmi kwa maana ya kutambuliwa na Sumatra maana hawana TLA ya PSV bali Tours hivyo kuwa na kibao cha "private", Concern yangu hapa ni uendeshaji wa hatari unaofanywa na madereva hawa, muda wote wako katika haraka ya ajabu, timings zao ni kuwahi wapite check point iringa kabla ya saa 6 na morogoro mjini muda ambao kwa sheria zetu ndo mwisho kwa magari ya abiria, nilisafiri na mmoja akawa na mwendo wa hatari, overtake za hatari more worse kila abiria walipomkanya ndio kwanza alizidisha mwendo na madoido mengine. Rai yangu kwa Sumatra watupie jicho na kuona namna ya kuwadhibiti hawa halikadhalika Polisi ambao hata hivyo ndio wachukua posho wakuu kutoka magari haya
 
hizo gari zinatusaidia sisi tusiopenda kulala dar tunaingia asubuhi jioni tunarudi mbeya
 
mbona hazipatagj ajali???

Hornet;
Hii ndo ajabu. Hao wenye TLA kila siku njia ya Mbeya - Dar vilio haviishi. Naona kuna kitu mlete hoja anataka tumsaidie hapa ila anaogopa tu kuwa muwazi. Swali la kizushi tu; Weye ni dereva wa bus au mmiliki?
 
nazipenda zile coaster natoka dar jioni asubui nakua tunduma nakuvuka border hakuna kulala hotel
 
tunashukuru kwa taarifa
hapa kazi tu na hii ndio slogan yetu
 
Hizo gari zimechangia sana maendeleo ya Mkoa wa Mbeya, asilimia kubwa ya matajiri wa Mkoa wa Mbeya wametajirikia kwenye hayo magari.
 
Coaster zinapiga makelele tu zikikanyagwa sana ila hazikimbii kihivyo ndio maana hazipati ajali hovyo
 
Ungesema gari za magazet kidogo ungeeleweka,hizo coaster mbona mwendo wao wa kawaida tu mkuu.....!
 
Huyu Mleta Mada Ni Mmiliki Wa Bus Nadhan Ila Hataki Kujipambanua, Funguka Tukusaidie Mkuu
 
Mara nyingi zinatoka saa saba mchana na kufika alfajiri siku inayofuata..zingekua zinakimbia sana zingefika saa sita usiku dar.ila wengi wa madereva wa izo coaster hawana leseni za kubeba abiria na hawajui sheria za barabarani..mara nyingi sana zinaacha njia izo sio kwamba hazipati ajali ni vile zinapata ajali muda ambao haziruhusiwi kuwa bara barani kwa iyo wanamaliza kwa rushwa tu.
 
Wakuu kuna huu usafiri wa Mbeya - Dar kwa kutumia Coaster wenyewe wanaziita hakuna kulala, Zinaanzia Uyole pale jijini mbeya na kwa Dar zinapakilia Kidongo Chekundu, Zinaondoka around saa 9&10 jioni sehemu kubwa ya safari ni usiku, ni usafiri usio rasmi kwa maana ya kutambuliwa na Sumatra maana hawana TLA ya PSV bali Tours hivyo kuwa na kibao cha "private", Concern yangu hapa ni uendeshaji wa hatari unaofanywa na madereva hawa, muda wote wako katika haraka ya ajabu, timings zao ni kuwahi wapite check point iringa kabla ya saa 6 na morogoro mjini muda ambao kwa sheria zetu ndo mwisho kwa magari ya abiria, nilisafiri na mmoja akawa na mwendo wa hatari, overtake za hatari more worse kila abiria walipomkanya ndio kwanza alizidisha mwendo na madoido mengine. Rai yangu kwa Sumatra watupie jicho na kuona namna ya kuwadhibiti hawa halikadhalika Polisi ambao hata hivyo ndio wachukua posho wakuu kutoka magari haya

Kwa ushauri wangu usirudie kupanda gari hizo,wanaopanda wengi ni wafanyabiashara ambao hawataki kulala dar
 
Back
Top Bottom