Clouds tv waonesha vita ya Libya

Clouds tv waonesha vita ya Libya

Nini Libya?waonyeshe Syria kabisa.
25th Oct kura yangu Ukawa.
 
Hiv tz unawezaje kulingajisha na Libya jaman....??!lini tz elimu bure ,lini tz afya bure,lini tz asiye na ajira hulipwa,lini tz makazi bure,lini tz bidhaa za ujenzi hazina kodi ......,???!!! Acha na sisi tufikie huko then tuone kama tutapigana??!!
 
Tunaendelea kukusanya ushahidi,kikinuka tu tukutane ICC The Hague .
 
CLOUDS ni ya KUKIFUTA KABISA...

Clouds ni ya KUITOKOMEZA KABISA... iwe funzo, na UKAWA wataifuta hii TV haraka sana hapo JANUARY mwakani..

TCRA naona wamelala tu...
 
clouds wawe makini sana kwani wao ndio wataanza kufikishwa the haugue
 
Yan clouds media hata haivutii tena kusikiliza wala kutazama. Wamekuwa wapumbavu kiasi cha kutumika vibaya. Tangu waonyeshe upendeleo kwa mafisiemu na kukandamiza UKAWA siwapendi hata kuwasikia pamoja na star tv. Tbc ndo sina hata muda wa kujisumbua kuiangalia. Nimeitoa hata kwny decoder yangu...
 
wanatuonyesha vita kwani taifa letu lipo vitani?? sasa cloud Fm mnaelekea kubaya sana...
 
Kama wameonyesha vita ya Libya tcra inapaswa kuwahoji sababu za kufanya hivyo. Katika tamko la tcra walishasema chombo cha Habari kiepuke kurusha habari ya kutia hofu Watu wengine hasa wapiga kura. Sijui kwanini watanzania hatubadiliki, tunaamini sana kubadili chama cha kuongoza nchi ni kuleta vita. Tufanye siasa zenye ushindani wa hoja tuache upuuzi na kuleta vitu vya kutia hofu. Unaweza onyesha hiyo video kwania ya kutia hofu Watu kumbe ndo ikawa kuwafundisha wasiohope. Tcra kuweni makini na vyombo vya Habari
 
Media house karibu zote zimesahau jukumu la msingi na wengi hawajui umuhimu wao kabisa kama wao ni sehemu muhimu kipindi hiki wakijashtuka watoto wana bunduki mkononi kuja kuziacha ni ngumu.
God bless us...Peace ✌🏿
 
Waunganishe na video ya machafuko Rwanda ikifatiwa na vurugu Kenya, back to back advert free no commercials. Mabadiliko lazima.
 
Katika habari yao ya jioni hii Clouds tv wameanza na habari ya kulinda amani.

Chakushangaza wameanza kwa kuonyesha vita vya Libya na kuanza kuweka ulinganishi na hali ya Tanzania na matamko ya Amani yaliyotolewa leo.

Mmeweka hzo video tena na sauti ili iweje?
Wito wangu ni huu, Clouds tv acheni huo mtindo mnaotaka kuanza huko ni kuwapa hofu wananchi katika kufanya maamuzi yao.

Wapiga kura ndiyo wenye maamuzi. Wao waweke zote wanazofahamu ila kwa sasa wapigakura washaelewa namna ya kufanya tar25Oct.
 
Na ile MOVIE ya vita ya pili ya dunia WW2 wataionyesha lini sababu ninayo shauku kubwa ya kumuona Adolf-Hiltler na rafiki yake Bennito Mussolini Kisha tarhe 25 Oct..kura yangu kwa LOWASAAAAA
 
Back
Top Bottom