Clouds Media acheni uhuni, mahojiano yenu na Feisal Salum siyo professional!

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,131
7,902
Baada ya kuangalia mahojiano ambayo Feisal Salum amefanya na Clouds Media, nimeshangazwa sana na kitendo chao cha kuachia mambo ya "off-air" yaruke hewani tena kwa muda mrefu.

Kuna video ambayo imekuwa inasambaa ambayo inasikika Feisal akizungumza na Wakili wake pamoja na watangazaji wa Clouds wakijadiliana nini aseme, nini asiseme na asemeje. Kwanza nikumbushe majadiliano kama hayo si kitu cha ajabu kwa mtu yoyote anayeenda kufanya mahojiano katika radio au television. Hadi viongozi wakubwa wa kitaifa, akiwemo Rais wa nchi lazima apangwe nini cha kusema na asemeje kwenye vyombo vya habari, hasa kama ni mahojiano yaliyo "sensitive" kisheria. Mara nyingine unayeenda kuhojiwa unaweza hata kutaka swali au maswali fulani usiulizwe na makubaliano haya huwa ni lazima yaheshimiwe.

Kinachonishangaza ni kwamba kituo kikubwa kama Clouds kurusha matangazo LIVE halafu kuachia kwa muda mrefu vile mambo ya "off-air" yaendelee kuruka. Kuna wakati camera zimemuonyesha Feisal muda mrefu huku kipindi kikiwa kimesimama. Hii inanifanya nianze kuhisi Clouds walikuwa wanataka kunasa kitu kutoka kwake ama cha picha au sauti kitakachomuharibia au tu kupata kitu cha kutrend.

Hivi unataka kuniambia Clouds katika urushaji wa matangazo yao hawana mtu maalumu anayemonita mambo ya sauti muda wote wa matangazo? Je huyu mtu aliyekuwa anamonita hakusikia mazungumzo hayo na hakuona umuhimu wa kukata sauti? Na pia kwa nini camera zenu zinaendelea kuruka LIVE zikimuonyesha Feisal kwa muda mrefu wakati kipindi kimesimama? Mnajua ethics za utangazaji kweli?

Mwisho nimalizie kwa kumwambia Feisal awe makini sana na kila anachokifanya sasa na hata siku zijazo maana si kila atakayemfuata atakuwa na nia nzuri na yeye. Kwa hiki anachokifanya kupigania haki zake amejijengea maadui wengi. Mambo haya ya Yanga na Simba ukiacha maslahi binafsi ya watu hayana tofauti sana na dini. Wengine watataka tu kumdhuru kisa anapingana na kiongozi wa timu yao.

Pia kutokana na uzito wa kile alichokuwa anaenda kujadili, nadhani angefanya mahojiano na mtu anayeweza kuwa serious kama Salama badala ya kwenda kwa hao wahuni ambao kwanza wanajivalia hovyo hovyo wakati mwingine bila kujali wanayemuhoji.
 
Mahojiano yalikuwa ni radio katika kipindi cha power breakfast kinachorushwa kuanzia saa 11 alfajiri mpaka saa 4 asubuhi sasa nyinyi mmejichanganya kuangalia mahojiano ya radio kwenye video sisi tuliokuwa tunasikiliza radio hatujasikia hayo ya Fei kupangiwa cha kuongea.

Justice..
 
Mahojiano yalikuwa ni radio katika kipindi cha power breakfast kinachorushwa kuanzia saa 11 alfajiri mpaka saa 4 asubuhi sasa nyinyi mmejichanganya kuangalia mahojiano ya radio kwenye video sisi tuliokuwa tunasikiliza radio hatujasikia hayo ya Fei kupangiwa cha kuongea.

Justice..
Dunia ilishahama huko unakosemea. Walikua live sehem mbili, radio na YouTube channel.
 
media za bongo haswa clouds ni za kihuni...wanatumia matatizo ya watu ili wapate kutrend,na kweli jana wamejua kutrend hasa pale walipovujisha hiyo clip,ni wao wenyewe waliovujisha na ni makusudi ila wapate ku trend DAMN ZAO
Redio ya kihuni siwezi kuisikiliza hata siku moja
Nimeshangazwa sana na jinsi gani walivyo unprofessional. Mambo serious wanachekacheka tu. Haikuwa sehemu sahihi kwa Feisal kwenda kuyajadili. Angetafuta mwandishi mmoja anayeheshimika akapiga naye exclusive.
 
Nimeshangazwa sana na jinsi gani walivyo unprofessional. Mambo serious wanachekacheka tu. Haikuwa sehemu sahihi kwa Feisal kwenda kuyajadili. Angetafuta mwandishi mmoja anayeheshimika akapiga naye exclusive.
Mallard Ayo ingependeza zaidi.
 
Achana nayo hiyo redio, ilishakufa siku aliyesema ogopa Mungu na Teknolojia alipofariki. Hawana mpya. Ukiangalia Kipanya alivyokuwa anamwangalia mla ugali na sukari. Utajua anamuona ni ZERO brain.
 
feisal usije ukakubali kurudi yanga.kama ni mizigo uliyobeba hawana wa kumpa wampe hata jisiem mwenyewe abebe.kijana nyota yako kali sana.ndo maana wanaogopa ukiondoka watafeli.
 
Nimeshangazwa sana na jinsi gani walivyo unprofessional. Mambo serious wanachekacheka tu. Haikuwa sehemu sahihi kwa Feisal kwenda kuyajadili. Angetafuta mwandishi mmoja anayeheshimika akapiga naye exclusive.
Tatizo wasanii na wachezaji wa michezo wanaamini hapo ndio sehemu sahihi ya kutobolea mambo yao, na sifa nyingi sijui Ruge alikuwa hivi ooh kama Mungu mtu, radio haina weledi wa kutosha
Sikiliza ea radio utaona kuna tofauti kubwa ya standard hasa maadili, ila haohao watangazaji wakienda clouds wanabadilika sana
 
feisal usije ukakubali kurudi yanga.kama ni mizigo uliyobeba hawana wa kumpa wampe hata jisiem mwenyewe abebe.kijana nyota yako kali sana.ndo maana wanaogopa ukiondoka watafeli.
Wewe ni chizi na mjinga kwelikweli, Yanga iko fainali CAF bila huyo Feisal.
 
Wewe ni chizi na mjinga kwelikweli, Yanga iko fainali CAF bila huyo Feisal.
marumo galants kashuka zake daraja,wydad casablanca yupo fainali klab bingwa.wewe ni mpumbavu wa mwisho unayeamini yanga inaweza bila feisal.ila wenzio wanajua umuhimu wake
 
Back
Top Bottom