Cliniki za Dawa mbadala zichunguzwe, tunaibiwa

Cliniki za Dawa mbadala zichunguzwe, tunaibiwa

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,447
Reaction score
10,785
Ndugu yangu mmoja alipata ajali ya gari akaumia kifuani. Hospitali za kawaida ikashindikana. Tukampeleka hizi cliniki za tiba mbadala. Dah, jamaa wanatoza mahela mengi, tulichoambuliwa ni maumivu mpaka leo mpaka tulipompata Dr Bingwa wa hosp za kisasa na mgonjwa ana nafuu.

Hizi clinic za Fore planning, Sigwa herbal, Life, na nyingine za akina Ndodi, Dr Ndulu na wengine zichunguzwe maana zinaishia kutuibia wananchi. Sina hakika na Elimu ya wale wamiliki. Kama zinatibu basi ni asilimia ndooogo sana, iliyobaki ni uongo na utapeli.

Sina hakika na vipimo vyao sijui kwa kompyuta, maana ile ni system ya kuwapofusha watu hasa wanaoisikia tu kompyuta wahadaike na kuliwa pesa. Pia nyingi ni magonjwa ya wanawake au mambo ya uzazi, ugumba n.k

Serikali chunguzeni hili.
 
Hahahahaha...sema wewe labda watasikia...nishasema siku nyingi huwezi kushindana na sayansi...hii alternative medicine ni majanga sana
 
Sio kweli,wewe kama ulienda kununua Dawa za kurefusha uume ukapigwa basi imekula kwako.

Foreplan wapo vizuri sana,uliza uambiwe.
Na mfumo wa kutumia Computer Diagnosis haujaanzia humu Nchi,Sasa wewe Teknolojia inakimbia wewe unatambaa.Utaachwa Mkuu,

Sasa kama unataka kupiga promo au kuharibia watu biashara,tafuta kwingine.
Maana watu wanaushuhuda utaumbuka bure

Ila sio kila ugonjwa uaonenda nao Hospitali lazima upone.
Kuna watu Wameenda mpaka India,na wakarudi hapa hali ikawa ile ile.

Mungu anapokupa ugonjwa huwa anakupa akili umtambue kwamba yeye yupo,sasa wewe unapata tiba bila maombi unategemea nini.
Muweke Mungu karibu,hizo tiba nyingine zozote ni nyepesi tu,kuna watu wanatibiwa kwa maji ya kunywa tu kwa kuamini.
 
sio kweli,wewe kama ulienda kununua dawa za kurefusha uume ukapigwa basi imekula kwako.

Foreplan wapo vizuri sana,uliza uambiwe.
Na mfumo wa kutumia computer diagnosis haujaanzia humu nchi,sasa wewe teknolojia inakimbia wewe unatambaa.utaachwa mkuu,

sasa kama unataka kupiga promo au kuharibia watu biashara,tafuta kwingine.
Maana watu wanaushuhuda utaumbuka bure

ila sio kila ugonjwa uaonenda nao hospitali lazima upone.
Kuna watu wameenda mpaka india,na wakarudi hapa hali ikawa ile ile.

Mungu anapokupa ugonjwa huwa anakupa akili umtambue kwamba yeye yupo,sasa wewe unapata tiba bila maombi unategemea nini.
Muweke mungu karibu,hizo tiba nyingine zozote ni nyepesi tu,kuna watu wanatibiwa kwa maji ya kunywa tu kwa kuamini.

mkuu usimpinge mtoa hoja saana.yeye ameamini hivyo na wewe una amini hivyo unavyoamini.hao mashuhuda unaosema yawezekana ni walewale watoto wa familia moja.
Angalia hata bahati nasibu za mtaani wale wanaopata ni wale wenzao kukuvuta
 
Back
Top Bottom