Cleopa D. Msuya: Nimemkubali


Hata mimi nilimuona na mazungumzo yake yalikuwa na mantiki sana.Isipokuwa,si alikuwa waziri mkuu ,alifanya nini,nothing.Hawa watu ni wababaishaji tu.Wanaona uozo wanapotoka madarakani,lakini wanapokuwa madarakani wanakuwa vipofu kabisa.Sijui nani anawapa limbwata.Sumaye,Mkapa,Warioba wote siku hizi wanaona uozo tulio nao, lakini walikuwa hawaoni kabisa,kazi kweli kweli.
 
Hii thread nilivyoiona imekaa sana kusifia tu bila kutoa faida za Msuya! Hakuna cha zaidi hapa watu wanaosifia wengi wao wanatoka sehemu aliotoka Msuya, kwa upande wangu mimi sina cha kumkumbuka namuweka kundi moja na Kikwete tu
 
Hii thread nilivyoiona imekaa sana kusifia tu bila kutoa faida za Msuya! Hakuna cha zaidi hapa watu wanaosifia wengi wao wanatoka sehemu aliotoka Msuya, kwa upande wangu mimi sina cha kumkumbuka namuweka kundi moja na Kikwete tu
In fwakti hapa kuna ka pointi!!
 
Tusiwe wabishi wa kila ki2. Mi naamini kila kitu kina changamoto zake. si vizuri kujadili mtu binafsi, tujadili point zenyewe, make baadhi wanachangiaji mjadala hawakuusikia, so wana hukumu moja kwa moja. Alisema
: Kipindi kile walikuwa na uwezo wa kukusanya kodi na kulipa mahitaji yote ya nchi, na ziada kidogo kwa ajili ya maendeleo je mkuu wa kaya saa hizi huo ubavu anao?
Pia alisema wao walikuwa wakielekeza mabwana shamba kuelimisha jinsi ya kutumia kilimo cha kitaalamu yaani upandaji wa mbegu kwa kutumia vipimo (kilimo bor) wakati wa sasa ni matrekta yamejazana kwenye yadi flani wakati huo utaalam wa kutumia hakuna.
Vilevile akashauri kuwa serikali ingepunguza matumizi ya kutumia magari ya kifahari kmvile Vx na badala yake zitumike gari za kawaida kama vitara. SASA HAPO KUNA KASORO GANI?

Mi ni mpinzani lkn, facts ziko wazi, other wise the problem is individualismiasis
 

You have my admiration Messrs Nyange.
Kuna watu wanaigeuza JF uwanda wa chuki na kumwaga sumu zao, alimradi kuna watu wanawachukia binafsi.
Wanasahau kuwa multiparty democracy means accomodating all dissenting views na kupata common ground.
Mbaya zaidi kuna wale wanofikiri akili inawafurika wasijue kuwa wanakuwaka kama mtu aliye vaa lubega na kufunika his frontal parts leaving his behind naked.
With this type of contibution, this is what I call great thinking is all about.
 

and this is the reason he is proposing the younger president !
 
President Kikwete described Mzee Msuya as a "True reformer," of the Tanzanian economy whose leadership steered successfully, the transition of the country's economy from controlled to liberal market economy from mid to late eighties.

..huwezi kuchambua hatua mbalimbali za maendeleo ya uchumi wa Tanzania bila kumzungumzia CD Msuya in a positive or negative way.

..wakati wa Mwalimu Nyerere, kuanzia mwaka 75 mpaka 1980, Msuya alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. tulijenga viwanda vingi sana wakati huo, lakini by 1983/84 viwanda hivyo vilikuwa vimeanza kusuasua kiuzalishaji.

..kwa msingi huo ukimsifia Mwalimu kwa ujenzi wa viwanda nchi nzima some of the credits goes to CD Msuya ambaye ndiye aliyekuwa mtekelezaji wa policies za Mwalimu ktk uanzishaji viwanda.

..kwa wale ambao wanamlaumu Mwalimu kwa uendeshaji mbaya wa viwanda vyetu nao kwa kiwango kilekile labda lawama hizo ziende kwa msaidizi wa Mwalimu aliyepewa jukumu la kuongoza wizara ya viwanda ambaye ni CD Msuya.

..Raisi Mwinyi anasifiwa kwa kuurekebisha uchumi wa Tanzania na kututoa ktk matatizo ya uhaba wa bidhaa yaliyokuwepo kipindi cha mwisho wa utawala wa Mwalimu Nyerere. kwa kifupi Mwinyi alilazimika kukubali masharti ya IMF/World Bank na Paris donors club. sasa Chief negotiator wa serikali ya Tanzania ktk mazungumzo yaliyopelekea Tanzania kupata msaada wa IMF alikuwa CD Msuya. Waziri aliyekuwa mstari wa mbele kusimamia utekelezaji wa maamuzi magumu ya kiuchumi yaliyofanywa wakati wa Mzee Mwinyi alipoingia madarakani 1985 to 1990 ni CD Msuya.

..kwa mtizamo wangu kipindi cha mahojiano na CD Msuya hakikuwatendea haki wa Tanzania. nasema hivyo kwasababu hakikuendeshwa na mwandishi mweledi ya uchumi wa Tanzania na historia tuliyopitia.

..
 
 
 
wanadamu wote tuna mazuri na mabaya,lakini bado naamini mzee huyu ni mmoja wa wazalendo wa nchi hii,ambaye mchango wake ktk ujenzi wa viwanda na uchumi hautasahulika kamwe. Vijana wengi waliweza kupatata ajira na maisha bora.
 
Wenzetu kama marekani wana sera zinazoliunganisha Taiafa bila ya kujali vyama vyao vya siasa vya republicans na democrats.Na ndiyo maana wako mbali kimaendeleo.Sisi bado sana kwasababu utofauti wa vyama pamoja na uongozi wa kisiasa vinaleta uadui mkubwa na ndio maana wanaoshika madaraka hawataki kuomba ushauri kwa vile wanaogopa ushindani wa kisiasa.Kama hawafuati hata yale mazuri tuliyoachiwa na viongozi waliopita,then usitegemee watawafuata kwa ushauri.

Makundi makundi ndo yametawala na kutokana na hilo,kuna ugumu wa kumfuata kiongozi flani hata kama ana hekima just because yuko kwenye "kundi" la tofauti.Na hayo ni ndani ya chama kinachotawala.Sasa kwa upinzani,uhusiano ulioko ni wa kubomoana kisiasa.Sasa ni muda gani watatumia kujadili yale ya msingi yenye maslahi kwa taifa?Wanatumia miaka mitano ya kwanza kujitayarisha kugombea awamu ya pili.

Na kujitayaraisha kwenye si kufanya yale waliyowaahidi wananchi kwenye sera na ilani zao ie maisha bora kwa kila mtz kama ilivyokuwa kwa ccm uchaguzi wa 2005.Badala yake wanatumia kujikita kimshiko zaidi ie rada,EPA etc....Imean Kifedha.Halafu awamu ya pili wanaitumia kutayarisha wanayeona anafaa na kuanza kucheza michezo michafu ya kisiasa dhidi ya wapinzani wa ndani ya chama pamoja na wale wa vyama vingine.

Tumeyaiga mataifa ya magharibi kwa kila kitu.Lakini tukumbuke kuwa ni sawa na mtoto anayejaribu kufanya kila anachofanya mtu mzima.Hatoweza,kila jambo lina wakati wake.Ni ngazi atakazopitia mtoto.Kwa mfano huwezi kumlisha mtoto ugali,utamlisha uji.Muda wa kula ugali ukifika basi atakula ugali.Mfano wangu huu unamaanisha kuwa bado siasa zetu ni changa sana na kuwaiga mataifa makubwa kwa kila hali,basi ni sawa na mtoto kula ugali.

Kabla ya kubakia kwenye siasa chafu peke yake.Tujiwekee misingi ya kitaifa.Misingi ambayo haina mjadala.Kwamba ukionekana unakwenda kinyume,basi huna haki ya kutawala.Tunataka tuanze na katiba.Katiba inayowashirikisha wananchi.Tuwe taifa moja lenye lengo moja.Chama kinachochemsha kinawekwa kando.Na kama kimekiuka misingi,basi uwajibikaji unatake place.Turudi na kufikiri upya kama binadamu wa kwawaida wenye kutumia common sense.Mambo yanayoendelea nchini mwetu hayaonyeshi hilo.
 
leo anazungumzia kuwawezesha wakulima kutumia mbegu bora, kipindi kile alisema kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe........
wewe ndio bure kabisa kamuulize Christant Maji ya Tanga Mzindakaya ndo anajua Cleopa alifanya nini! Pia nina uhakika haya ulioandika hapa wakati yanatokea lbada hata mama yako alikuwa hajaolewa.
 
wanadamu wote tuna mazuri na mabaya,lakini bado naamini mzee huyu ni mmoja wa wazalendo wa nchi hii,ambaye mchango wake ktk ujenzi wa viwanda na uchumi hautasahulika kamwe. Vijana wengi waliweza kupatata ajira na maisha bora.

Si watu wengi humu jf wanaokumbuka au kujua kuwa chini ya Mwalimu na viongozi kama Msuya Tanzania ilikuwa na viwanda vindi vya umma.
Viwanda kama Bora Shoes,Viwanda vya ngozi(Tanneries),Viwanda vya Korosho,Viwanda vya nguo,Viwanda vya zana za kilimo na vingine vingi.
Pamoja na uendeshaji usioridhisha , juhudi ya kuajiri vijana na kuzalisha mali ilikuwepo kwa dhati.

Leo tumerasimisha sekta ya viwanda kwenda katika sekta binafsi, sekta yenye nguvu ya soko.Strategic Industrial policy bado haieleweki vyema nchini na wakati huo huo viwanda vilivyouzwa karibu vyote vimekufa/kuuwawa ili wafanyabiashara waaigize bidhaa hizohizo nje ya nchi.
Na hapo ndo tuna wakumbuka watu kama CD Msuya
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…