Civil Engineering UDSM

Civil Engineering UDSM

Hamna kozi duniani ambayo haina soko kama UNA UJUZI KICHWANI na kama ni mtu wa kujiongeza hasa kwenye kutafuta maarifa na connection.
Kumbe wewe jamaa umesoma CIVIL.
Sasa mbona unakujaga kuchangia nyuzi za programming & software development. Ama ni Mambo ya self-taught.
 
Ok sawa mkuu, ila coet siku hz wameondoa specialization mfano mtu wa civil and water resources, au civil and structural engineering au civil and highway engineering badala yake cheti cha mhitimu kinandikwa civil engineering tu kwa mujibu wa prospectus yao labda waliliona jambo hilo may be
Huyo alimaliza pale udsm mwaka 2011 kama sikosei.. Infact hata bado zingekua zipo ni jina tu maana nyuma ya pazia wanasoma kila kitu kuanzia barabara mpaka majengo! Na huyo jamaa pamoja na kazi yake ila alisimamia sana miradi ya barabara hapo dsm (kama sikosei alikua moja ya mainjinia walio simamia mradi wa barabara za mwendokasi)!!
 
Kumbe wewe jamaa umesoma CIVIL.
Sasa mbona unakujaga kuchangia nyuzi za programming & software development. Ama ni Mambo ya self-taught.
Sijasoma civil as civil japo pamoja na hayo programming tulisoma chuo! Ila kikawaida programming ni kitu kila mtu anatakiwa atleast ajue basics zake na ndio maana wakati sisi tunangoja tufundishwe php na prof chuoni huko nje utakuta mtoto ana miaka 11 lakini humwambii chochote kuhusu python au C programming!!

Programming is science na engineering ni application ya science so usishangae mimi kujua programming!
 
"Civil and irrigation, civil and water resource"

Kwa kifupi hata kama hiyo "civil" isingekuwepo lazima usoma kozi za structural design. Hata ungesoma irrigation eng lazima usoma usome structural design.

So jibu la swali lako, unaajiriwa vizuri kabisa. ILA UJUE KWENYE AJIRA UNAWEZA UKAWA NA DEGREE YA CIVIL NA BADO UKAWA MWEUPE KICHWANI yani mweupe pee!!

Jua chuoni utapewa "ka intro" tu, baada ya hapo utatakiwa ujiongeze mwenyewe kujisomea softwares nk.

Mfano chuoni hutafundishwa kutumia staad pro au prota au etabs ila kwenye ajira(hasa zile zinazo husu design) kama hujui walau moja imekula kwako!!
Kaka unachoongea kina ukweli ata sisi uku wa umeme Kuna vitu hutakaa ufundishwe yaan intro usipojiongeza umeenda
 
Back
Top Bottom