Civil Engineering Special Thread!

Ndio maana nikasema "or deep foundation"!!

Nikimaanisha pile or any other kind of deep foundation!!

Rejea swali langu mkuu..
Kwa deep foundation kuna pile foundation & raft or mat foundation so yote yanawezekana kuna moja imetumika kati ya hizi mbili ila pia kama water table ipo juu ndio lazima watatumia pile foundation
 
Mkuu acha kabisa mimi nimetumia zote...hizo...ila nitarecommend Autocad yaani kama unaijua vizuri utaenjoy sanaa
Mkuu masemea kwenye ku design nyumba na sio structural design.

Nimekua nikitumia autocad kwa mda ila juzi juzi tu nimeanza jifunza archcad. Kwa kweli naona utofauti sana...

Kwenye autocad ni lazima uchore plan, section, elevation ect... Wakati archcad ukichora tu plan basi elevation inajileta, so simple yani!!
 
Kuna Kazi tofauti kati ya ArchCad na AutoCAD.. Structure lazima udesign na AutoCAD
Structual design kwenye auto mbona kama naona ni issue, nnavyojua kudesign structures STAAD na nyingine kama hizo ndio zinatumika!!
 
Yoote hayo nayafahamu ila mimi niko flexible sana kwenye AutoCad kuliko ArchiCAD, nilianza kuitumia ArchiCad ndio nikajifunza AutoCad....

Kumbuka kuna AutoCad Architechure hii inafanya kazi kama ArchiCAD...yaani ukichora plan election na section zipo
 
Nilikua sijui hili, nimekua nikitumia autocad "auto desk" ya kawaida. Ngoja nitaifwatilia hiyo nikisha imasta archcad....
 
Tatizo ni kwamba Ukichora kwa ArchCard lazima uje uhamishie kwenye AutoCad ndio ufanye baadhi ya Marekebisho tena
 
Ni matumaini yangu kuna mafundi,wahandisi na watu wengine ambao kwa namna moja ma nyingine watajihusisha na ujenzi!

Katika ujenzi kuna kitu kinaitwa zege au kitaalamu "Concrete", sasa ili zege lipatikane kunakuwa na mchanganyiko wa simenti (cement), Maji, Mchanga (Fine aggregates), Kokoto(Coarse aggregates)!

Mchanganyo unafanywa katika uwiano maalum labda 1:3:6 kwa zege la Gredi 15, sasa maji yanayofaa kwa huo Mchanganyo yanatakiwa yawe maji safi ambayo yanafaa kunywa, Maji ambayo hata wewe uliyepo site ukiambiwa kunywa unayanywa.. yasiwe ya Chumvi!

Nyongeza: Kiasi chote cha maji kinachotakiwa kwenye mchanganyo, kumwagilia zege (Curing, matumizi ya wafanyakazi yanatakiwa yawe kati ya Lita 300 mpaka 500 kwa M^3 moja ya Zege!
 
1:3:6 ni grade 10 mkuu, grade 15 ni 1:2:4

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…