Swali lako ni zuri na Watu wengi hua wanajiuliza Swali hili.
Sina jibu la moja kwa moja ila ningependa kukushirikisha mambo yafuatayo huenda yakasaidia kujibu hilo swali.
1. Nini Malengo na Matarajio yako katika siku za usoni na siku za baadae.
Cisco Certifications
Cisco certifications Zinamuandaa Canditate katika Technical perspective nikimaanisha network engineer katika level tofauti kuanzia assicocate,professional na expert. Zinamjenga mtu mwenye maono ya kuhusika moja kwa moja kwenye kwenye Networking technologies kwa maana ya Configuration &Troubleshooting, Planning and many more.Certification hizi zimegawanya sehemu tofauti tofauti kama routing&switching, service provider, Security,Voice,Data center etc. Hivyo kama lengo malengo yako ni kuwa technical candidate, nikimaanisha any of these (Network Adminstrator/Engineer/manager/planner) nakushauri upitie njia hii.
Pia kamaMalengo yako ya baadae ni kuwa Consultant au Contractor katika mambo ya Networking then hizi certification zitakusaidia ukijumuisha na uzoefu utakao kua umeupata ulipokua unafanya moja ya kazi tajwa zilizo kwenye italic hapo juu.
Kwa upande wa ajira, ni sehemu nyingi wanahitaji candidates wenye hizo sifa, Service Providers,Telecom Operators, Financial Institutions, Education Institutions(waweza kuwa trainer au network engineer)Government and Non goverment agencies Industries, Health sectors and Many More.
Pia unapaswa kujua kwamba sio Cisco tu bali, kuna Vendor wengine wengi tu hutoa devices na Certifiaction. Lakini at entry level haina shida ukisoma CISCO esp CCNA& CCNP itakupa good foundation hata ku enteract na devices za vendor wengine kama Huawei, Alcatel na Juniper.
CISA Certification , and others of similar trend of Certification like CISSP, CISM, CRISC
CISA certification na hizo zingine nilizozitaja hapo juu zinamuandaa Candidate katika Management Side.
CISA humuandaa Auditor in the technical side ambae mara nyingi atahusika moja kwa moja katika kuhakikisha security policies and good practises are adhered by a company as far as ICT is concerned. Pia huamuandaa auditor ili aweze ku-identify current and future risk in ICT na hutakiwa kushauri hatua za kuchukuliwa ili kuhakikisha kampuni ina jiepusha na mianya yoyote ya upotevu wa taarifa na fedha katika domain ya ICT. Kikubwa zaidi humpa maarifa ya kuchunguza, kugundua na kukamata ubaghilifu wa pesa ama taarifa na nyaraka muhimu unaofanyika kwa njia ya ICT.
Pia humpa candidate general knowledge ya ICT system vile inapaswa kuwa inapaswa kuwa kuanzia hardware, software na intergration ya devices tofauti tofauti in ICT so as to come up with a secure and standard ICT sytem.
Kwa upande wa ajira, CISA candidate anahitajika sana kwenye Financial institutions, Telecom operators,Government and Non Government companies and Agencies, Industries etc.
Pia apart from CISA kuna certifiaction nyingine kama CISSP, CISM, CRISC, CRE.
Kwa Telcom companies kuna RA(Revenue assurance Certifications) and FM(Fraud Management).
CISA and CISCO Candidates both being in the Technology side wanahitajika sana na hawana sababu ya ku-compete maana wanafanya majukumu tofauti.
Pia candidates anaweza kuwa na certifications zote mbili na akawa na uhuru mkubwa wa kuamua nini anapenda kufanya kati ya majumu hayo mawili.
Having said that unaweza ukaamua nini ungependelea zaidi baada ya kuona uhalisia na majuku ya candidates hao wawili.
Kwa upande wangu nilikua na maswali mengi kama wewe, bahati nzuri nilibahatika kufanyia kazi majukumu yote mawili katika nyakati tofauti na hapo ndipo nilipojua nilichokua nakipenda zaidi na ndo ninachoendelea nacho mpaka sasa. I'm Certified in CISA and Cisco (CCNA &CCNP R&S)