..jamani hiki ni chuo kikuu cha Afrika cha kimataifa.
..kingekuwa kinajengwa na serikali ya Tanzania basi tungekuwa na uwezo wa kuulizana kwanini hakijengwi Kigoma,Sumbawanga,Rufiji,Mafia etc.
..binafsi nadhani kilichozingatiwa hapo ni kuangalia eneo lenye miundombinu ya ku-support chuo kikuu. Arusha tayari miundombinu ya namna hiyo ipo mfano uwanja ndege, mawasiliano ya uhakika, mji wenye hadhi etc etc.
..sehemu kama Kigoma hata Watanzania wenyewe tunapakimbia. kuna maeneo kama Rufiji ambayo mtumishi wa serikali akihamishiwa anaamua kuacha kazi kabisa.
..sasa hawa wasomi/wahadhiri wa kimataifa ambao watafanya kazi kwenye chuo cha Mandela tuna uhakika kweli watavumilia kukaa eneo kama Kigoma, au Rufiji, au Mafia, au Sumbawanga, au Pemba?
..mngependekeza chuo kijengwa Mwanza kidogo ningewaelewa.
Masanja,
..nakubaliana na wewe kwamba kuna maeneo serikali imeyatelekeza.
..cha kusikitisha zaidi hata wananchi wa maeneo hayo nao kama wameunga tela la serikali ktk kuyatelekeza maeneo walikuzaliwa na kukulia.
..iliwahi kuletwa hoja hapa ikizungumzia utendaji wa Zitto Kabwe jimboni kwake.
..wana jamii forums wengi waliizima hoja hiyo wakisema Zitto halazimiki kuweka juhudi zozote zile kuchochea maendeleo ya Kigoma.
..sasa kama Zitto hana uchungu wowote na Kigoma mnategemea JK, Pinda, Masanja,jokaKuu etc ndiyo wawe na uchungu na Kigoma?
..hebu fikiria mkoa wa Kagera pamoja na kuonekana "nshomile sana" waliitana na kuchangishana 1.5 bilion kwa ajili ya elimu.
..umesikia wabunge toka Kigoma waki-organise mkutano wowote ule kuchangisha kwa ajili ya maendeleo ya Kigoma? na mikutano ya namna hiyo siyo lazima uite wana Kigoma peke yake.