KERO Chuo Kikuu cha Iringa hakijali afya za Wanafunzi, tumelipia mwezi nne sasa hakuna huduma ya Bima

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Chuo Kikuu cha Iringa kina ubabaishaji, hawajali afya za Wateja wao (Wanafunzi) haiwezekani mwanafunzi kafanya usajili kuanzia Novemba mpaka Desemba, lakini bima yake haijawa activated.

Mnufaika akienda hospitali kupata matibabu anaambiwa bima haiko active inabidi atumie pesa yake ya akiba, na kibaya zaidi ni kuwa akifuatilia kwa wahusika hawana majibu ya kueleweka.

Wanakera sana, mamlaka za Afya zifuatilie hili, kuna vitu havipo sawa, fedha tumelipa lakini kila siku tunatumia kile tulichobaki nacho mfukoni.

Majibu ya Chuo, soma hapa - Madai ya Chuo Kikuu cha Iringa kutojali afya za Wanafunzi, uongozi wasema kuanzia mwakani Wanafunzi watalipa Bima moja kwa moja NHIF
 
Hizo bima zenyewe hata zikiwa active hakuna la maana. Mpaka syringe unalipia cash. Kuwa na bima ni sawa na kutokuwa nayo tu. Tafuteni kero nyingine.
 
Back
Top Bottom