Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimeshindwa kuzimalizia Hosteli za Magufuli?

Hayati Rais Magufuli aliwajengea UDSM hosteli za kulala wanachuo nzuri na za kisasa kabisa, cha kushangaza nimerudi baada ya miaka miwili hostel bado hazijafanyiwa finishing kwenye flat zake za juu. Juu ya hizo hosteli Kuna mirunda na magogo Kwa kweli inashangaza.

Ikumbukwe kabla ya hostel za Magufuli kujengwa wanafunzi wa chuo kikuu Cha Dar es Salaam walikuwa wanateseka sana na wengine kubakwa kila wakienda kupanga mitaani lakini Sasa shida hiyo haipo lakini hazimaliziwi vizuri mpaka leo.

Shida ni nini wakati uongozi wa UDSM wanakusanya hela kutoka Kwa kila mwanafunzi?
Bwana yule alichota pesa hazina tu akapeleka hapo chuo sasa hizi za kumalizia au kuendeleza ujenzi zinaenda kwa hatua na kwa budget..
 
Back
Top Bottom