KERO Chuo cha Ukutubi, Uhifadhi wa Nyaraka (SLADS) ni cha Serikali lakini baadhi ya Wahitimu tukiomba ajira tunaambiwa hatuna vigezo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Wanafunzi wa Chuo cha Ukutubi, Uhifadhi wa Nyaraka na Tafiti (SLADS) kilichopo Bagamoyo chini ya Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB) tunapitia changamoto kadhaa:-

Nawasilisha kero hii kwa niaba ya wengine tumehitimu masomo ya Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka (Library Records and Documentation Studies) Bagamoyo awamu tofautitofauti.

Chuo hicho ni cha Serikali lakini tumekuwa tukiomba ajira, kupitia Ajira Portal kwenye Kada ya Uhifadhi Kumbukumbu, tukienda kwenye usaili tunatolewa kuambiwa hatuna vigezo, hawa wale wahitimu ya Diploma tunapitia vipindi vigumu.

Tumeenda hadi mamlaka husika lakini majibu yao tusubiri, tangu 2025 mpaka leo tunashindwa kupaza sauti kwa kuwa wengi wetu hatuna uwezo maswali tunayojiuliza ni kwamba:-

1. Ikiwa chuo ni cha Serikali na kipindi tunasoma tumesoma uhifadhi kumbukumbu iweje leo hii tunatolewa kwa kigezo hatuna sifa?

2. Je, vipi kuhusu jasho la wazazi wetu wametusomesha kwa shida sana leo hii tunaishia hapa.

3. Ngazi ya Diploma Library ajira hazitoki kabisa BODI YA MAKTABA TANZANIA, kila Mwaka wanaajiri level ya cheti ni ipi hatima yetu sisi wengine?

Naomba msaada wa kupaza sauti kwenye hili labda tutaonekana barua zetu tumeandika zimefika hadi UTUMISHI lakini mpaka leo hakuna majibu tunazidi kuteketea tunaumia sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…