Niliambiwa jana na mama watoto kuhusu hili swala. Nilichokifanya nikapiga simu TFDA-mamlaka ya chakula na dawa. Nikapata fursa ya kumuuliza one of the Directors kama kuna ukweli kuhusu hili swala. Nikaambiwa kwamba ni uongo. Hiyo chumvi iko salama kwa matumizi ya binadamu.
Ushauri: Wananchi wenzangu tupende kufanya utafiti kabla ya kulaumu serikali na watendaji wake. Kuna mambo hayahitaji kuingiza siasa. Wengi humu tunauelewa na tuna simu..tupende kufanya utafiti kwa wahusika. Itatusaidia.
Asanteni.