Dar ni kubwa mnoo huwezi sema tu sehemu yoyote. We elezea malengo yako tukushauri
Nahitaji chumba kimoja cha kupanga maeneo yoyote ya jiji la Dar es salaam yenye sehemu tulivu. Kodi 30,000 kwa mwezi na nitalipa kodi ya miezi 6 ili kuangalia mazingira kwanza. Mwenye nacho anipigie simu namba 0717577755 au anaweza kuni PM.
Sehemu tulivu halafu utalipa tshs ngapi vile.....?..plz come again
kaka umenifurahisha sanaaa....huyu jamaa inabidi ajipange kwelikweli...kwa huko anakotaka inabidi asipungukiwe tshs 100,000/= kwa mwezi na lazma alipe kodi ya mwaka mzima.... AJIPANGE SANAAAAAAA.
kaka umenifurahisha sanaaa....huyu jamaa inabidi ajipange kwelikweli...kwa huko anakotaka inabidi asipungukiwe tshs 100,000/= kwa mwezi na lazma alipe kodi ya mwaka mzima.... AJIPANGE SANAAAAAAA.
dar unapata chumba hata cha elfu nane (8000). inategemeana na uwezo wako. kwa hiyo elfu 30 yake atapata chumba sehemu aliyo taja. kitu mhimu ni kutafuta bila kuchoka. mia
malengo gani kaka? Mi nahitaji chumba cha kuishi na kama chumba kitapatikana maeneo haya kijitonyama, kimara, magomeni, kinondoni, changanyikeni, ilala na mabibo itakuwa poa sana.
kaka nadhani dar bado hujaijua-
haya maeneo uliyotaja ni tulivu lakini sio kwa bei hiyo na kama ni kwa bei hiyo ni kwa nyumba isiyo na umeme..
Maeneo hayo hasa kijitonyama, magomeni, ilala na kinondoni yametokea kuwa mijini na watu wanafanya biashara zaidi ya kupangisha vyumba..huko changanyikeni ndio kumegeuzwa hostels za wanavyuo ambako wenye vyumba wanatoza kodi kwa kichwa na chumba kimoja wanakaa hadi watu wanne.
Kwa maeneo kama mansese, tandale, mbagala charambe, yombo dovya hizo room zipo ila sio kwa utulivu uutakao kama wa haya maeneo.
Pole kama nitakuwa nimekukwaza.
Acha maneno ya kipuuzi wewe!? Au wewe ni taahira?
wewe dar unaijua vyema? Au unajishaua kama mwenzio?
dar unapata chumba hata cha elfu nane (8000). Inategemeana na uwezo wako. kwa hiyo elfu 30 yake atapata chumba sehemu aliyo taja. Kitu mhimu ni kutafuta bila kuchoka. Mia
dar unapata chumba hata cha elfu nane (8000). inategemeana na uwezo wako. kwa hiyo elfu 30 yake atapata chumba sehemu aliyo taja. kitu mhimu ni kutafuta bila kuchoka. mia
kaka usiweke jazba mbele...umekuja hapa jamvini kuomba msaada wa mawazo..so uwe mstaarabu kwa kila jibu unalopewa...au hupendi kuambiwa ukweli unaoumiza?....au unapenda kudanganywa kama mtoto mdogo?
Anyway tafuta madalali waulize bei za nyumba kwa hayo maeneo tulivu unayoyataka wewe then tembea nao ukaone utakachokutana nacho n
a pia ujue kuna gharama za kumlipa dalali kwa kuzunguka na wewe na pia kuna gharama za kumlipa dalali kama atakupatia chumba...kodi ya mwezi mmoja ni mali ya dalali...
Ukuwe ujuwe..acha jazbaaa usaidiwe mawazo ili wewe ukayachambuwe kwa wakati wako.
kaka jamaa yangu m1 mwaka 2000 aliwahi kuhama maeneo ya kijitonyama makumbusho alikokuwa analipa tshs 30,000 kwa mwezi akahamia mbagala alikokuwa analipa tsh 5000 kwa mwezi....lakini aliingia gharama za usafiri kuja kazini maeneo ya makumbusho na usumbufu wa kuamka saa 10.00 usiku ili awahi kazini na kuepukana na kupanda gari na kuchelewa ofcn...mwaka uliofuatia alihama na kurudi tena maeneo ya makumbusho.
Somo hapa ni kuwa cha bure aghali...unapolipia gharama kidogo unapata gharama zingine za ziada nyuma ya ubure wa kile kitu...huyu ndugu anataka maeneo tulivu ambayo kila mtu anayataka then bei inakuwa juu plus madalali wanapandisha bei na wenyenyumba wanapenda hilo....na maeneo hayo kodi hupanda kila mwaka au baada ya miaka miwili.