Chuma ulete. Nimejichanganya

Chuma ulete. Nimejichanganya

Nisaidieni mawazo jamani.

Sijawahi kwenda kwa mganga.

Juzi natoka geto kwenda kwenye kibanda changu nikakutana na buku mbili njiani. Nikarudi geto nikachukua chumvi ya mawe nikaimwagia nikaiokota. Kwanzia hapi kila jioni nikipiga hesabu. Pesa zinapelea. Pesa ukirudia kuhesabu zunapelea tena kila siku. Nisaidieni kabla sijaanza kwenda sehem zisizo sahihi.
Kutumia chumvi pekee bila kuwa na mamlaka ya kiroho huwezi kufanikiwa kitu. Basi sema kwa Jina la Yesu navunja nguvu zote za chumaulete kwenye maisha yangu. Ita Damu ya Yesu mara 7 na sema natakasa uchumi wangu kwa Damu ya Yesu. Rudia kuliita Jina la Yesu na Damu ya Yesu na kuelekeza nguvu hizi za ajabu kwenye roho ya chumaulete ukitamka kuivunja kwa Jina la Yesu. Usisahau kunipa mrejesho. Pia funika uchumi na fedha zako kwa Damu ya Yesu kila wakati.
 
Back
Top Bottom