Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,869
Mtunzi Juma hiza 01
Suzani alikuwa amejifungia chumbani kwake, wakati huo alikuwa akilia kwa uchungu. Hakutaka kuamini kile kilichokuwa kimetokea katika maisha yake.Mkononi mwake alikuwaameishikilia picha ya mwanaume mmoja. Aliitazama picha hiyo kwa muda wa dakika kadhaa huku machozi yakiendelea kumbubujika mashavuni mwake.
Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali mno, kila alipokuwa akiendelea kuitazama picha ya mwanaume huyo ndivyo ambavyo maumivu yalizidi kuongezeka moyoni mwake.
Alijisikia vibaya sana, alijutia mambo mengi mno aliyoyafanya katika maisha yake na mwanaume huyo.Kuna muda aliona kama alionewa, hakustahili kabisa kupitia maumivu yale aliyokuwa nayo katika kipindi hicho.
Kitendo cha kuendelea kuitazama picha ya mwanaume huyo ambayo kiukweli iliendelea kumuumiza tu! aliona sio jambo zuri hivyo alichoamua kukifanya ni kuigeuza upande wa pili. Alifanya hivyo ili asiendelee kuumia.
Hilo bado halikuwa suluhisho la maumivu ambayo alikuwa nayo moyoni mwake. Kichwani mwake bado taswira na kumbukumbu za mwanaume huyo zilimjia.
Alikumbuka mambo mengi mno aliyoyafanya na mwanaume huyo aliyekutana naye katika mtandao wa Facebook na kuanzisha mahusiano naye ya kimapenzi.
Katika kipindi hicho hakuwa naye, alimtelekeza tena na mimba ya miezi miwili. Hilo lilizidi kumuumiza mno.
Hakukuwa kuna kipindi ambacho moyo wake uliwahi kupata maumivu kama katika kipindi hicho, yalikuwa ni maumivu makali sana yaliyochanganyika na kumbukumbu zilizomuumiza kupita kawaida.
Muda mfupi kabla ya kuingia ndani ya chumba chake na kuanza kulia, alitoka kuzungumza na baba yake ambaye alimuweka kikao na kuanza kumuhoji juu ya ujauzito huo.
Baba yake aliyejulikana kwa jina la Mzee Mushi hakuonekana kupendezewa na tukio hilo hata kidogo na ndiyo sababu iliyompelekea mpaka akamuita mwanaye na kuanza kumuuliza juu ya mtu anayehusika kumpa ujauzito huo.
“Nakuuliza huu ujauzito ni wa nani?” aliuliza Mzee Mushihuku akimtazama binti yake kwa macho ya ukali.Suzani hakujibu kitu, alianza kulia kilio cha kwikwi.
Kilio hicho cha Suzani wala hakikumuingia akilini Mzee huyo ambaye tayari hasira zilikuwa zimempanda. Alichokuwa akihitaji kukifahamu ni mtu aliyehusika kumpa ujauzito mwanaye.
“Mwanangu baba yako si anakuuliza lakini mbona humjibu?” aliuliza Mama yake Suzani baada ya kumuona mumewe amezidi kupandwa na hasira.
“Mama na Baba naomba mnisamehee,” alisema Suzani huku akiendelea kulia.
“Jibu lako na swali langu ni vitu viwili tofauti, nimekuuliza huo ujauzito ni wa nani?” aliuliza Mzee Mushi huku macho yakimtoka.
Suzani hakujua ni wapi ambapo alitakiwa kuanza kuzungumza, hakujua ni lugha ipi ambayo alitakiwa kuitumia kuwaeleza wazazi wake juu ya mwanaume huyoambaye alihusika kumpa ujauzito.
Aliendelea kubaki kimya kitendo ambacho kilizidi kumuudhi mno Baba yake, akainuka pale kwenye kochi alipokuwa amekaa, akamsogelea mwanaye.
“Nakupa siku tatu uwe umeshaniambia mwanaume huyo aliyekupa ujauzito ni nani la sivyo hii nyumba utaiona ni chungu. Haiwezekani maana hii ni dharau kabisa yaani upo chuo tena nakusomesha kwa pesa zangu mwenyewe halafu unaniletea mimba kweli?” alisema Mzee huyo huku akimnyooshea kidole cha shahada mwanaye.
Baada ya Mzee Mushi kuzungumza hayo Suzani akainuka na kukimbilia chumbani kwake ambapo akajifungia mlango.Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali mno, akakumbuka kuichukua picha ya mwanaume huyo aliyempa ujauzito na kuanza kuiangalia. Kila alipokuwa akiendelea kuitazama picha hiyo ndivyo ambavyo maumivu yalizidi kuongezeka moyoni mwake.
Baada ya kupita siku tatu Mzee Mushi alimuita tena mwanaye na kumuuliza. Hakutaka utani hata kidogo. Siku hiyo ndiyo siku ambayo alihitaji kumfahamu mtu huyo aliyehusika kumpa ujauzito mwanaye. Kama kawaida yake, macho ya ukali yakamtoka, akamtazama mwanaye ambaye ndiyo alikuwa akijiweka sawa kuzungumza, hofu ilikuwa imemtawala.
“Sema.”
“Anaitwa Enock,” alijibu Suzani huku akionekana kuwa ni mwenye wasiwasi.
“Anaishi wapi?” aliuliza Mzee Mushi kwa sauti ya ukali.
“Mwanza,” alijibu Suzani.
“Unapafahamu mpaka kwake?”
“Hapana.”
“Kivipi?”
“TulikutanaFacebook tukaanzisha mahusiano, alipanga kuja kuniona hivyo akafunga safari kutoka Mwanza akanifuata huku Moshi,” alijibu Suzani huku akionekana kuwa wasiwasi.
Wote wawili wakachoka, hawakutaka kuamini kile walichokuwa wakikisikia.Aliposikia jina la Facebook Mzee Mushi akaonekana kushangaa zaidi kushinda mke wake.
“Eti! mlikutana Facebook?” aliuliza kana kwamba hakusikia vizuri hapo mwanzo.
“Ndiyo.”
“Halafu ikawaje?”
“Tukaanzisha mahusiano na mwisho wa siku mpaka tukapanga kukutana,” alijibu Suzani kisha hapohapo Mzee Mushi akainuka na kumpiga kofi zito ambalo likamuacha na alama ya vidole shavuni mwake.
Kile kilichokuwa kimetokea kwa binti yake huyo kilikuwa ni aibu kubwa kwa upande wakehasa ukizingatia katika mtaa huo aliyokuwa akiishi Moshi mjini, Majengo kwa Mtei yeye ndiye Mzee aliyekuwa akisifika kuwana binti mrembo ambaye alijitunza na kuwa na hofu ya Mungu.
Kutokana na uzuri aliyokuwa nao Suzani kila mwanaume aliyemuona alimtamani na kuanza kumfuatilia.
Mpaka kufikia kipindi hicho hakukuwa kuna mwanaume hata mmoja katika mtaa huowala chuoniambaye alifanikiwa kuiona hata nguo yake ya ndani.Hilo lilizidi kuwachanganya sana wanaume ambao walitamani kufanya naye mapenzi tu!.
Kwa kile kilichokuwa kimetokea kwa binti yake huyo Mzee Mushi kilimuumiza sana, kilimchanganya mno. Kuna muda alitamani mpaka kulia kwa kufikiria ni wapi ambapo angeificha sura yake kutokana na aibu kubwa aliyoipata katika maisha yake.
Moyo wake uliingiwa na chuki kubwa, kila alipokuwa akimwangalia mwananye alihisi kumchukia vibaya mno. Hakutaka kumuona mbele ya macho yake kwani aliamini kwa kuendelea kumuona kuna jambo baya ambalo angeweza kumfanyia na dunia ingemshangaa.
Mke wake aliyejulikana kwa jina laBi Anna huruma ikamuingia,hakupenda kuona binti yake akiendelea kulia na kusononeka kila siku, kama ni kosa tayari alikuwa ameshalifanya hivyo hakukuwa na jinsi tena zaidi ya kusaidiwa.
Alichokuwa akihitaji kwa wakati huo ni kuona mume wake akimsamehe Suzani na kumsaidia kutokana na hali ambayo alikuwa nayo. Alimpenda mno binti yake huyo ambaye ndiye mtoto wa pekee ambaye alijaaliwa kumpata katika kipindi chote cha ndoa yake.
Hilo lilikuwa ni jambo gumu mno, Mzee Mushi hakutaka kukubali kirahisi msamaha huo kwa binti yake.
“Mume wanu lakini..”
“Nimesema sitaki kumuona hapa nyumbani kwangu. Nitamuua,” alisema Mzee Mushi huku uso wake ukiwa tayari umebadilika.
Kwa jinsi ambavyo alikuwa akionekana Mzee huyo na maneno aliyokuwa akiyazungumza. Vilikuwa ni vitu viwili vilivyofanana.Yaani kile alichokuwa akikizungumza ndicho hicho hicho ambacho alikimaanisha.
Uamuzi ambao aliamua kuuchukua ni kumfukuza binti yake huyo. Hakutaka kumuona.
Japokuwa mkewe Bi Anna alimsisitiza na kumuomba zaidi na zaidi asichukua uamuzi huo wa kumfukuzwa binti yaohuyo ambaye kwao alikuwa kama mboni ya jicho lakini hakutaka kumsikiliza. Aliamua kumfukuza Suzani.
Suzani hakutaka kuamini kama kweli alifukuzwa nyumbani kwao tena na Baba yake mzazi.
Machozi yalikuwa yakimdondoka. Kuna muda alianza kujutiayale yote aliyoyafanya katika maisha yake. Kitendo cha kukutana na mwanaume Facebook mpaka akamuamini na kumkabidhi moyo wake ambao aliuumiza.
Muda huo tayari alikuwa amechelewa kwani hata kama angeendelea kujutia kosa alilokuwa amelifanya bado ukweli usingeweza kubadilika.
*Je, nini kitaendelea?*
*Tukutane Jumamosi mahali hapahapa.*
Suzani alikuwa amejifungia chumbani kwake, wakati huo alikuwa akilia kwa uchungu. Hakutaka kuamini kile kilichokuwa kimetokea katika maisha yake.Mkononi mwake alikuwaameishikilia picha ya mwanaume mmoja. Aliitazama picha hiyo kwa muda wa dakika kadhaa huku machozi yakiendelea kumbubujika mashavuni mwake.
Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali mno, kila alipokuwa akiendelea kuitazama picha ya mwanaume huyo ndivyo ambavyo maumivu yalizidi kuongezeka moyoni mwake.
Alijisikia vibaya sana, alijutia mambo mengi mno aliyoyafanya katika maisha yake na mwanaume huyo.Kuna muda aliona kama alionewa, hakustahili kabisa kupitia maumivu yale aliyokuwa nayo katika kipindi hicho.
Kitendo cha kuendelea kuitazama picha ya mwanaume huyo ambayo kiukweli iliendelea kumuumiza tu! aliona sio jambo zuri hivyo alichoamua kukifanya ni kuigeuza upande wa pili. Alifanya hivyo ili asiendelee kuumia.
Hilo bado halikuwa suluhisho la maumivu ambayo alikuwa nayo moyoni mwake. Kichwani mwake bado taswira na kumbukumbu za mwanaume huyo zilimjia.
Alikumbuka mambo mengi mno aliyoyafanya na mwanaume huyo aliyekutana naye katika mtandao wa Facebook na kuanzisha mahusiano naye ya kimapenzi.
Katika kipindi hicho hakuwa naye, alimtelekeza tena na mimba ya miezi miwili. Hilo lilizidi kumuumiza mno.
Hakukuwa kuna kipindi ambacho moyo wake uliwahi kupata maumivu kama katika kipindi hicho, yalikuwa ni maumivu makali sana yaliyochanganyika na kumbukumbu zilizomuumiza kupita kawaida.
Muda mfupi kabla ya kuingia ndani ya chumba chake na kuanza kulia, alitoka kuzungumza na baba yake ambaye alimuweka kikao na kuanza kumuhoji juu ya ujauzito huo.
Baba yake aliyejulikana kwa jina la Mzee Mushi hakuonekana kupendezewa na tukio hilo hata kidogo na ndiyo sababu iliyompelekea mpaka akamuita mwanaye na kuanza kumuuliza juu ya mtu anayehusika kumpa ujauzito huo.
“Nakuuliza huu ujauzito ni wa nani?” aliuliza Mzee Mushihuku akimtazama binti yake kwa macho ya ukali.Suzani hakujibu kitu, alianza kulia kilio cha kwikwi.
Kilio hicho cha Suzani wala hakikumuingia akilini Mzee huyo ambaye tayari hasira zilikuwa zimempanda. Alichokuwa akihitaji kukifahamu ni mtu aliyehusika kumpa ujauzito mwanaye.
“Mwanangu baba yako si anakuuliza lakini mbona humjibu?” aliuliza Mama yake Suzani baada ya kumuona mumewe amezidi kupandwa na hasira.
“Mama na Baba naomba mnisamehee,” alisema Suzani huku akiendelea kulia.
“Jibu lako na swali langu ni vitu viwili tofauti, nimekuuliza huo ujauzito ni wa nani?” aliuliza Mzee Mushi huku macho yakimtoka.
Suzani hakujua ni wapi ambapo alitakiwa kuanza kuzungumza, hakujua ni lugha ipi ambayo alitakiwa kuitumia kuwaeleza wazazi wake juu ya mwanaume huyoambaye alihusika kumpa ujauzito.
Aliendelea kubaki kimya kitendo ambacho kilizidi kumuudhi mno Baba yake, akainuka pale kwenye kochi alipokuwa amekaa, akamsogelea mwanaye.
“Nakupa siku tatu uwe umeshaniambia mwanaume huyo aliyekupa ujauzito ni nani la sivyo hii nyumba utaiona ni chungu. Haiwezekani maana hii ni dharau kabisa yaani upo chuo tena nakusomesha kwa pesa zangu mwenyewe halafu unaniletea mimba kweli?” alisema Mzee huyo huku akimnyooshea kidole cha shahada mwanaye.
Baada ya Mzee Mushi kuzungumza hayo Suzani akainuka na kukimbilia chumbani kwake ambapo akajifungia mlango.Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali mno, akakumbuka kuichukua picha ya mwanaume huyo aliyempa ujauzito na kuanza kuiangalia. Kila alipokuwa akiendelea kuitazama picha hiyo ndivyo ambavyo maumivu yalizidi kuongezeka moyoni mwake.
Baada ya kupita siku tatu Mzee Mushi alimuita tena mwanaye na kumuuliza. Hakutaka utani hata kidogo. Siku hiyo ndiyo siku ambayo alihitaji kumfahamu mtu huyo aliyehusika kumpa ujauzito mwanaye. Kama kawaida yake, macho ya ukali yakamtoka, akamtazama mwanaye ambaye ndiyo alikuwa akijiweka sawa kuzungumza, hofu ilikuwa imemtawala.
“Sema.”
“Anaitwa Enock,” alijibu Suzani huku akionekana kuwa ni mwenye wasiwasi.
“Anaishi wapi?” aliuliza Mzee Mushi kwa sauti ya ukali.
“Mwanza,” alijibu Suzani.
“Unapafahamu mpaka kwake?”
“Hapana.”
“Kivipi?”
“TulikutanaFacebook tukaanzisha mahusiano, alipanga kuja kuniona hivyo akafunga safari kutoka Mwanza akanifuata huku Moshi,” alijibu Suzani huku akionekana kuwa wasiwasi.
Wote wawili wakachoka, hawakutaka kuamini kile walichokuwa wakikisikia.Aliposikia jina la Facebook Mzee Mushi akaonekana kushangaa zaidi kushinda mke wake.
“Eti! mlikutana Facebook?” aliuliza kana kwamba hakusikia vizuri hapo mwanzo.
“Ndiyo.”
“Halafu ikawaje?”
“Tukaanzisha mahusiano na mwisho wa siku mpaka tukapanga kukutana,” alijibu Suzani kisha hapohapo Mzee Mushi akainuka na kumpiga kofi zito ambalo likamuacha na alama ya vidole shavuni mwake.
Kile kilichokuwa kimetokea kwa binti yake huyo kilikuwa ni aibu kubwa kwa upande wakehasa ukizingatia katika mtaa huo aliyokuwa akiishi Moshi mjini, Majengo kwa Mtei yeye ndiye Mzee aliyekuwa akisifika kuwana binti mrembo ambaye alijitunza na kuwa na hofu ya Mungu.
Kutokana na uzuri aliyokuwa nao Suzani kila mwanaume aliyemuona alimtamani na kuanza kumfuatilia.
Mpaka kufikia kipindi hicho hakukuwa kuna mwanaume hata mmoja katika mtaa huowala chuoniambaye alifanikiwa kuiona hata nguo yake ya ndani.Hilo lilizidi kuwachanganya sana wanaume ambao walitamani kufanya naye mapenzi tu!.
Kwa kile kilichokuwa kimetokea kwa binti yake huyo Mzee Mushi kilimuumiza sana, kilimchanganya mno. Kuna muda alitamani mpaka kulia kwa kufikiria ni wapi ambapo angeificha sura yake kutokana na aibu kubwa aliyoipata katika maisha yake.
Moyo wake uliingiwa na chuki kubwa, kila alipokuwa akimwangalia mwananye alihisi kumchukia vibaya mno. Hakutaka kumuona mbele ya macho yake kwani aliamini kwa kuendelea kumuona kuna jambo baya ambalo angeweza kumfanyia na dunia ingemshangaa.
Mke wake aliyejulikana kwa jina laBi Anna huruma ikamuingia,hakupenda kuona binti yake akiendelea kulia na kusononeka kila siku, kama ni kosa tayari alikuwa ameshalifanya hivyo hakukuwa na jinsi tena zaidi ya kusaidiwa.
Alichokuwa akihitaji kwa wakati huo ni kuona mume wake akimsamehe Suzani na kumsaidia kutokana na hali ambayo alikuwa nayo. Alimpenda mno binti yake huyo ambaye ndiye mtoto wa pekee ambaye alijaaliwa kumpata katika kipindi chote cha ndoa yake.
Hilo lilikuwa ni jambo gumu mno, Mzee Mushi hakutaka kukubali kirahisi msamaha huo kwa binti yake.
“Mume wanu lakini..”
“Nimesema sitaki kumuona hapa nyumbani kwangu. Nitamuua,” alisema Mzee Mushi huku uso wake ukiwa tayari umebadilika.
Kwa jinsi ambavyo alikuwa akionekana Mzee huyo na maneno aliyokuwa akiyazungumza. Vilikuwa ni vitu viwili vilivyofanana.Yaani kile alichokuwa akikizungumza ndicho hicho hicho ambacho alikimaanisha.
Uamuzi ambao aliamua kuuchukua ni kumfukuza binti yake huyo. Hakutaka kumuona.
Japokuwa mkewe Bi Anna alimsisitiza na kumuomba zaidi na zaidi asichukua uamuzi huo wa kumfukuzwa binti yaohuyo ambaye kwao alikuwa kama mboni ya jicho lakini hakutaka kumsikiliza. Aliamua kumfukuza Suzani.
Suzani hakutaka kuamini kama kweli alifukuzwa nyumbani kwao tena na Baba yake mzazi.
Machozi yalikuwa yakimdondoka. Kuna muda alianza kujutiayale yote aliyoyafanya katika maisha yake. Kitendo cha kukutana na mwanaume Facebook mpaka akamuamini na kumkabidhi moyo wake ambao aliuumiza.
Muda huo tayari alikuwa amechelewa kwani hata kama angeendelea kujutia kosa alilokuwa amelifanya bado ukweli usingeweza kubadilika.
*Je, nini kitaendelea?*
*Tukutane Jumamosi mahali hapahapa.*