Prakatatumba abaabaabaa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2022
- 1,465
- 4,675
Nilienda sehemu moja ugenini, kama ilivyo ada ugenini hata ukae siku mbili Lazima ujibane usiende chooni hovyo hovyo, siku ya tatu nikaona hali sio poa acha niende chooni kufanya harakati muhimu.
Cha kushangaza nikakuta choo cha kukaa, sijawai kukitumia before, nikapiga mahesabu maana nimeshazoea vyoo vyetu vya kulenga, nikasema acha nifanye harakati, baada ya harakati nikaflash fresh maana niliona sehemu ya kubonyeza.
Kimbembe kilikuja namna ya kujitawaza maana tishu sikuiona, nikapiga mahesabu kama dakika kumi namna ya kujisafisha, kwa utabe wangu wa namba kwa kusolve, logarithim, integration, na complex number nilishindwa kung'amua ni kwa jinsi gani naweza kujisafisha kwenye choo cha kukalia nikaona hii sasa ni soo, nikasepa moja kwa moja mpaka nyumba jirani kuomba usaidizi. Jioni ikabidi nimuage mwenyeji kwamba nimepata dharula.
Hivi mlioweka hivi vyoo vya kukaa na hamna tishu huwa mnajisafisha vipi? Nitoeni ushamba.
Cha kushangaza nikakuta choo cha kukaa, sijawai kukitumia before, nikapiga mahesabu maana nimeshazoea vyoo vyetu vya kulenga, nikasema acha nifanye harakati, baada ya harakati nikaflash fresh maana niliona sehemu ya kubonyeza.
Kimbembe kilikuja namna ya kujitawaza maana tishu sikuiona, nikapiga mahesabu kama dakika kumi namna ya kujisafisha, kwa utabe wangu wa namba kwa kusolve, logarithim, integration, na complex number nilishindwa kung'amua ni kwa jinsi gani naweza kujisafisha kwenye choo cha kukalia nikaona hii sasa ni soo, nikasepa moja kwa moja mpaka nyumba jirani kuomba usaidizi. Jioni ikabidi nimuage mwenyeji kwamba nimepata dharula.
Hivi mlioweka hivi vyoo vya kukaa na hamna tishu huwa mnajisafisha vipi? Nitoeni ushamba.