Chonde chonde wabunge wa mkoa wa Kagera

Chonde chonde wabunge wa mkoa wa Kagera

ngonani

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2012
Posts
1,366
Reaction score
598
Mkoa wa Kagera na hasahasa wilaya ya Bukoba vijijini ina matatizo makubwa ya maji, mkoa wa Kagera ni kati ya mikoa michache sana Tanzania ambayo wananchi wanagombea maji na mifugo,katika karne hii kukosa maji ya bomba au Kisima ni aibu.

Katika vijiji vya wilaya ya Bukoba vijijini, Nkenge na Muleba maji usombwa na bodaboda na ndoo ni mpaka sh 700.

Najua mkoa huu una wabunge japo ni aina ya Wabunge ambao kwao ni Dar Es Salaam, hawajui matatizo na mahitaji halisi ya majimboni mwao, na ndio maana michango yao ni kuulizia viwanja vya ndege so and so kitajengwa lini etc.

Nilitegemea katika bajeti ya wizara ya maji wabunge hao wapigie sana kelele na kuondoa mashilingi kuhusu suala la maji majimboni mwao, lakini as usual walikuwa kimya tu na kuachia wengine wa mikoa mingine na ambao wengi wao wana maji tayari wakiongezewa mitandao ya maji majimboni mwao.

Honestly kama by 2015 hakuna maji ya uhakika na salama katika mkoa wa Kagera especially wilaya za Bukoba vijijini na Muleba, Nkenge basi ni bora waheshimiwa wetu msichukue fomu kabisa kwani hata mimi nitatumia hela yangu kufanya malicious campaign.
 
Kweli Kagera hasa Bukoba vijijini kuna changamto kubwa sana ya maji pamoja na kuwepo mito mingi pamoja na maziwa mtatu (Ikimba, Victoria au Rweru na Buligi) lakini tatizo la maji ni kubwa sana,na sijawahi sikia mbuge hata mmoja akitetea wananchi wake. Kwa kweli inauma sana
 
Nilikuwa Kyaka, kwa kweli wanaishi maisha ya shida. Ukienda na nguo nyeupe lazima zibadilike. Maji ya kuswaki wamanunua ya chupa. Sijui mbunge wa eneo la Kyaka ni nani? Inasikitisha sana. Hapo ndipo mto mkubwa unapita, wakati wakai wa Bukoba hawana maji.
 
hapa ni kufanya mabadiliko si hatutaki siasa Bali vitendo ndo tunataka,mnapumulia mashine.
 
Nilikuwa Kyaka, kwa kweli wanaishi maisha ya shida. Ukienda na nguo nyeupe lazima zibadilike. Maji ya kuswaki wamanunua ya chupa. Sijui mbunge wa eneo la Kyaka ni nani? Inasikitisha sana. Hapo ndipo mto mkubwa unapita, wakati wakai wa Bukoba hawana maji.

Mbunge ni Asumpter Nshunju kama sikoesi
 
Bwana Ngonani,awali naomba upokee pole zangu kwa kilio chako.Ushauri wangu kwako ningeomba uwekeze zaidi jinsi gani utasaidia kupunguza makali ya tatizo husika badala ya kusubili 2015. Mfano hizo pesa za Malicious campein zinaweza saidia kuchimba kisima kimoja kijijini kwenu.
 
Mtaongea sana hapa alafu kesho mnaishia kuwachagua walewale wa CCM ...nilisikia pale Muleba pana mradi wa maji nikasikia pale B.vijijini kuna mradi wa visima na pale manispaa nimesikia kuna pesa ya miji 3 musoma,bukoba na mwanza sasa sijuhi imefikia wapi

Kuna mda kinachokosa ni msukumo ama wa halmashauri zenyewe ama wabunge pamoja na wananchi kwa ujumla,washauri wananchi wawabane watendaji wao lakini pia 2015 mnatakiwa kufanya mabadiliko makubwa sana kwa kuwaondoa viongozi wote wa CCM,pelekeni harakati
 
Huyo mbunge wenu anapenda totoz sana

Heh ilo nalo neno,kwahiyo zinammaliza akiri? tukiwa na conclusions kama zako nina hakika tutaishia kujaza server hapa kwa majina ila kula mademu hakumzuii mbunge kufanya kazi yake mkuu, kama anashindwa ni matatizo binafsi/chama ambayo yanahitaji tiba mbadala ikifika 2015
 
Wana JF, Shumalamu.

Sasa ninaanza kuamini kwa nini Kagera imepotea katika ramani ya uchumi wa wa nchi hii tofauti na muda baada ya mkoloni (1960-1980). Imekuwa haipati wawakilishi wa kuitetea ukiondoa nyakati za Kassano, Kaneno na Bakampenja. Muleba kusini tulipompata Anna Tibaijuka tukaamini ana vision ya kimarekani. Yeye ndie ameboronga kuliko. Mwijage amebaki kujisifia alivyomtaalamu wa mambo ya mafuta. Wote hawajui sisi tunahitaji nini ili Kagera iendelee.

KITU MUHIMU NI UCHUMI WA KAGERA. FULL STOP.
Tuliwachagua kwa elimu zao ili watafiti la kutetea nalo ni ku-influence mfumo uwe katika kumpatia unafuu mkulima wa Kagera. Kagera wanahitaji kupata kutokana na kahawa yao. Mfumo umekuwa kwa muda mrefu unawanyanganya pato la kahawa na hawa watetezi wetu wakiwa wamebuma tuuuu, KCU,chama chetu cha ushirika kimefanywa kitengo cha CCM watetezi wetu kimyaaaa. Ndio maana hata bei iweje, serikali inakata asilimia kubwa yake kwanza, mkoa na CCM nao wanakatapo, wafanyakazi wa KCU hao wanakomba na kuacha kiduchu kwa mkulima maana hana mtetezi. Sijawahi kumsikia mbunge anatumia nguvu na busara zake kuona hili la chama cha ushirika kuwa mzigo kwa wana Kagera linafumbuliwa. Kama KCU ingekuwa inatenda kama BCU walau kwa asilimia 50 Kagera tusingekuwa tunakuwa nafasi za mwisho kama tulivyo kwa sasa katika Tanzania kimaendeleo.
Hawa wabunge wetu wakifika ni kutuzodoa kwa kuweka mikutano na kuruhusu magendo ya kahawa yafanyike bila kuzuiwa. Hatupendi kuuza magendo bali tunakimbia bei mbovu yak KCU. Wanafika na manoti yao mifukoni kwa kutoa misaada mara vikoba , mara nini sijui ili waendelee kuchaguliwa, sisi hatukuwachagua wawe wanatugawia pesa, tuliwachagua waiambie serikali iwe ndio iwe enanaleta pesa maana serikali haiwezi kufuliska lakini wao wanaweza kufiliska.

Pili ni mnyauko wa migomba. Tungekuwa na wawakilishi Kagera ingekuwa imeishatangazwa eneo la janga kitaifa na kila nguvu yote ya serikali kuelekezwa huko. Ninyi wabunge wa Kagera mbona mumelala?

Make Kagera to be in the priority of the nation na sababu zipo, wake up!
 
Haa haa tibaijuka ni tabaka lilelile la wanyonyaji! Poleni wana muleba!
 
Wana JF, Shumalamu.

Sasa ninaanza kuamini kwa nini Kagera imepotea katika ramani ya uchumi wa wa nchi hii tofauti na muda baada ya mkoloni (1960-1980). Imekuwa haipati wawakilishi wa kuitetea ukiondoa nyakati za Kassano, Kaneno na Bakampenja. Muleba kusini tulipompata Anna Tibaijuka tukaamini ana vision ya kimarekani. Yeye ndie ameboronga kuliko. Mwijage amebaki kujisifia alivyomtaalamu wa mambo ya mafuta. Wote hawajui sisi tunahitaji nini ili Kagera iendelee.

KITU MUHIMU NI UCHUMI WA KAGERA. FULL STOP.
Tuliwachagua kwa elimu zao ili watafiti la kutetea nalo ni ku-influence mfumo uwe katika kumpatia unafuu mkulima wa Kagera. Kagera wanahitaji kupata kutokana na kahawa yao. Mfumo umekuwa kwa muda mrefu unawanyanganya pato la kahawa na hawa watetezi wetu wakiwa wamebuma tuuuu, KCU,chama chetu cha ushirika kimefanywa kitengo cha CCM watetezi wetu kimyaaaa. Ndio maana hata bei iweje, serikali inakata asilimia kubwa yake kwanza, mkoa na CCM nao wanakatapo, wafanyakazi wa KCU hao wanakomba na kuacha kiduchu kwa mkulima maana hana mtetezi. Sijawahi kumsikia mbunge anatumia nguvu na busara zake kuona hili la chama cha ushirika kuwa mzigo kwa wana Kagera linafumbuliwa. Kama KCU ingekuwa inatenda kama BCU walau kwa asilimia 50 Kagera tusingekuwa tunakuwa nafasi za mwisho kama tulivyo kwa sasa katika Tanzania kimaendeleo.
Hawa wabunge wetu wakifika ni kutuzodoa kwa kuweka mikutano na kuruhusu magendo ya kahawa yafanyike bila kuzuiwa. Hatupendi kuuza magendo bali tunakimbia bei mbovu yak KCU. Wanafika na manoti yao mifukoni kwa kutoa misaada mara vikoba , mara nini sijui ili waendelee kuchaguliwa, sisi hatukuwachagua wawe wanatugawia pesa, tuliwachagua waiambie serikali iwe ndio iwe enanaleta pesa maana serikali haiwezi kufuliska lakini wao wanaweza kufiliska.

Pili ni mnyauko wa migomba. Tungekuwa na wawakilishi Kagera ingekuwa imeishatangazwa eneo la janga kitaifa na kila nguvu yote ya serikali kuelekezwa huko. Ninyi wabunge wa Kagera mbona mumelala?

Make Kagera to be in the priority of the nation na sababu zipo, wake up!
Tumekusikia mkuu,na hoja yako ina mashiko lakini,wakulima wa huko bukoba wanayajua hayo?
kama wanayajua,kwanini kwa miaka yote hii wameendelea kuwachangua wabunge hao? Fikiria daraja la kaja na kyamugera toka enzi za rwegasira mpaka kamala na wote walikuwa mawaziri ni majanga,njoo muleba Kinyondo ,masilingi walikuwa mawaziri walifanya nini na hao hao wakulima wameendelea kuchagua chama chetu.
Binafsi naona mnyauko umeletwa na Mungu ili wakulima waamke,maana ndizi zilitufanya tuwe tunasubiria hela ya rushwa kwenye uchaguzi tununue mboga tu maana chakula ndizi kilikuwepo,kwa sasa kumekucha chakula hakuna kitaeleweka kama mtu atapokea 500/= ya dagaa ndo hivyo tena.Kinachotakiwa hapa ni wakulima kujitambua
Angalia wenzao moshi wanavyokula maisha
Mbunge wao Mrema enzi hizo akiwa waziri alienda nje akawatafutia soka la kahawa wa kwetu wamelala.
 
Kwa kweli inasikitisha Huko Kagera hakuna wabunge bali mizigo ya CCM ndo maana imekaa tu bungeni.
 
Nyie si nshomile

Si mnasema Anna Kajumulo Tibaijuka anafaa kuwa RAIS kwani ataondoa umaskini nchini; mwambieni aanzie kuwapatia maji huko Bukoba kwanza ili iwe ndio hatua ya kwanza ya kuwaondolea umaskini!!!
 
Mkoa wa Kagera na hasahasa wilaya ya Bukoba vijijini ina matatizo makubwa ya maji, mkoa wa Kagera ni kati ya mikoa michache sana Tanzania ambayo wananchi wanagombea maji na mifugo,katika karne hii kukosa maji ya bomba au Kisima ni aibu.

Katika vijiji vya wilaya ya Bukoba vijijini, Nkenge na Muleba maji usombwa na bodaboda na ndoo ni mpaka sh 700.

Najua mkoa huu una wabunge japo ni aina ya Wabunge ambao kwao ni Dar Es Salaam, hawajui matatizo na mahitaji halisi ya majimboni mwao, na ndio maana michango yao ni kuulizia viwanja vya ndege so and so kitajengwa lini etc.

Nilitegemea katika bajeti ya wizara ya maji wabunge hao wapigie sana kelele na kuondoa mashilingi kuhusu suala la maji majimboni mwao, lakini as usual walikuwa kimya tu na kuachia wengine wa mikoa mingine na ambao wengi wao wana maji tayari wakiongezewa mitandao ya maji majimboni mwao.

Honestly kama by 2015 hakuna maji ya uhakika na salama katika mkoa wa Kagera especially wilaya za Bukoba vijijini na Muleba, Nkenge basi ni bora waheshimiwa wetu msichukue fomu kabisa kwani hata mimi nitatumia hela yangu kufanya malicious campaign.

Mhe. Ngonani, Wilaya mpya ya Kyerwa iliokuwa sehemu ya Karagwe ina wakazi zaidi ya 400,000 (Sensa 012). Hadi sasa, hakuna hata kaya moja yenye umeme au maji. Katika eneo zima la wilaya hiyo hakuna hata mita moja ya barabara ya rami. Hakuna hata shule moja yenye A-level ya Serikali. Hakuna Hospitali hata moja ya Serikali. Hakuna hata kachuo ka-ufundi. Mbunge wa Jimbo Mhe. Eustace Katagira ndiye mnunuzi mkuu wa Kahawa za wapiga kura wake! Kweli, ukishangaa ya Muleba, BK-Vijijini na Nkenge, utayaona ya Kyerwa!
 
Umeshasema wilaya mpya. unalalamika hivyo kama vile tanzania ni huko tu. Kyerwa ni wilaya imetoka karagwe ambako hiyo lami sio kihivyo. Wabunge wenu ni ndio tu pale bungeni.
 
Back
Top Bottom