Chonde chonde 'Mafisadi' Msiende Mahakamani-Jaji Bomani

Unajua mkuu heshima mbele,

Yaani sasa nimeanza kuchoshwa na hii drama, I mean ni nchi gani duniani watu wenye ushahidi dhidi ya watuhumiwa, na watuhumiwa wenye ushahidi dhidi ya wanaowatuhumu, wanashauriwa wasiende mahakamani, hivi umemsikia hata balozi mmoja toka nje akisema msiende mahakamani?

Amani itapungua? Hivi ni amani ipi hiyo wanayoisema? Mwananchi anakuwaje na amani wakati haiamini serikali yake? Mimi nilifikiri huu ndio wakati wa CCM kujisafisha na kujiweka sawa maana ni kwenda mahakamani kushinda na kuwamaliza kabisaa upinzani, I mean kweli unahitaji kuwa political science professor kuelewa kuwa kama kweli hawa viongozi waliotuhumiwa hawana makosa as of their claim, basi CCm ni kuwasafisha na kuwa-bulldoze tu upinzani for the rest of their political life au career?

Yes huu ndio utakuwa mwisho wa Zitto, na upinzani kwa ujumla iwapo watashinda mahakamani, maana kama hakuna ushahidi dhidi yao basi ni kuwafungulia Treason Charge kina Dr. slaa na Zitto, tena kwa kuhatarisha amani yetu hebu niambie ni mtu gani duniani atakayelalamika?

Tunawaambia wanayamaze, lakini hawasikiii, what a drama? Hawa walikuwa wamezoea kujificha nyuma ya Mwalimu, that party is over, mambo yawekwe hadharani tu, next stop Mahakamani tukamkome nyani mchana kweupe!

Mkuu, Watanzania wengi tungependa sana kuona hao waliochafuliwa heshima zao wanafungua hii kesi. Kama kweli hakimu atakayeendesha kesi hii akiwapa uhuru pande zote mbili katika kesi hiyo basi tunaweza kusikia mengi mno ambayo yanaweza kabisa kutuacha Watanzania midomo wazi kwa maovu tutakayosikia.

Wakati huo ukumbuke jaji mkuu mstaafu Barnabas Samatta alipokuwa anastaafu alitamka kwamba mahakama imejaa rushwa ya hali ya juu kiasi kwamba alikuwa anakosa usingizi kwa rushwa jinsi ilivyokithiri. Mahakama bado ni zile zile na hakujafanyika chochote ili kupambana na uozo huo. Hivyo rushwa katika kesi hiyo itakuwa kama kazi na mwenye pochi kubwa katika kesi hiyo (tunawajua ni akina nani) watashinda bila matatizo yoyote na kutuacha Watanzania bado na majonzi chungu nzima kuhusiana na hali halisi ya nchi yetu.
 
....huyu bomani naona anatuona wote vilaza,eti anashauri watu waende TAKURURU badala ya mahakamani,hiyo TAKUKURU si ndio wameshindwa hata kusema chochote kuhusu Richmond na kusema hawawezi kumshitaki yule bwana mkubwa...hapa tutakjua watu kama kina Hosea hawasaidii chochote katika rushwa mana ni kama wanamfanyia kazi raisi sio wananchi...kuna umuhimu wa kubadili katiba namna ya kuwapa kazi hawa maofisa badala ya sasa vyeo hivi ni kama asante au ushkaji tuu...kazi tunayo kwelikweli maana kuna mengi ya kubadili
 
Mzee ES,


CCM ina hatia zifuatazo: Ina viongozi wanaopora mali ya uma. Imehodhi madaraka kwa njia za wizi wa kura. Imeuza mali asili za taifa bila ridhaa ya wawakilishi wa wananchi. Ina viongozi wanaowekeana mikataba ya siri na wawekezaji, na wanaokataa hata kuwaonyesha wawakilishi wa wananchi yaliyomo kwenye hiyo mikataba. Ina viongozi wanaoendeleza utawala wa kiimla.

Hawa wanaopora mali ya uma na kulindana ndani ya CCM kwa sasa ni wafungwa wetu watarajiwa.

Salute mkuu. hayo ni maneno mazito sana, naamini siku moja njonzi yako itatimia!
 
Jaji Bomani, naona anakanusha kuwa hakusema hoja ya Slaa ni legelege 'Alinukuliwa vibaya' kwi kwi kwi.


Jaji Bomani ataka Serikali, wapinzani wasiende kortini

*Ataka itafutwe njia bora kupambana na rushwa, ufisadi
*Awanasihi Watanzania kujijengea uvumilivu wa kisiasa


Na Fortunate Sheni, RCT

MWANASHERIA Mkuu wa Serikali mstaafu, Jaji Mark Bomani, amewaomba baadhi ya watu wanaotishia kushitakiana mahakamani kutokana na tuhuma mbalimbali za rushwa kufikiria upya ulazima wa kufanya hivyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dar es Salaam jana, Jaji Bomani alisema sheria za Tanzania zinatoa fursa ya kupiga vita rushwa na ufisadi na kwamba kinachotakiwa ni nia na utashi wa kufanya hivyo.

Alitoa mfano wa sheria iliyopo ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), aliyosema ilikuwapo tangu mwaka 1970 na kuwa imetoa uwezo kwa taasisi hiyo kumtaka kiongozi au mtumishi yeyote, kutoa maelezo ya mali zake ambazo hazilingani na uhalisia wa mapato yake.

Jaji Bomani alieleza kuwa inapotokea kiongozi anashindwa kutoa maelezo ya mali zake, atakuwa ametenda kosa la jinai na kuongeza kuwa TAKUKURU italazimika kufanya kazi yake kweli kweli na ionekane ikifanya hivyo.

"TAKUKURU lazima ifanye kazi yake ili mtu yeyote pamoja na wapinzani wawe na imani, kwamba wakipeleka taarifa zao juu ya tuhuma au hisia za vitendo vya rushwa na ufisadi dhidi ya kiongozi au mtumishi yeyote zitafanyiwa kazi kwa dhati," alisema Jaji Bomani.

Aidha, alikanusha habari zilizotolewa na gazeti moja la kila wiki kuwa alimwonya Katibu Mkuu wa CHADEMA ambaye ni Mbunge wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa na kuongeza kuwa hakusema maneno hayo.

"Sikumwonya Dkt. Slaa na wala sikusema kuwa hoja zake ni legelege! Haya si maneno yangu," alisema Jaji Bomani na kuongeza kuwa hakutaja jina la Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe, kama ilivyokuwa kwenye gazeti hilo.

Alisema katika mahojiano na gazeti hilo, alitoa upungufu wa jinsi tuhuma za rushwa zinavyoshughulikiwa na kueleza baadhi ya sababu zinazoleta rushwa mambo ambayo hayakuandikwa.

Kuhusu uhuru wa mtu yeyote chini ya Katiba kutoa maoni kwa maandishi au kwa mdomo, Jaji Bomani alisema litakuwa jambo la kushangaza kwa mtu kusema kuwa uhuru huo haupo au haufai na kusisitiza, kuwa upo na unapaswa kulindwa.

Kuhusu malumbano yaliyopo juu ya suala la rushwa na ufisadi, Jaji Bomani alisema malumbano hayo yamepamba moto kutokana na ukweli, kwamba vitendo vya rushwa na ufisadi vipo na kwamba havikubaliki katika nchi ambayo inazungumzia au inaamini katika usawa wa binadamu na utawala bora.

Alibainisha, kwamba mtu anayesema vitendo hivyo havipo nchini si mkweli na kwamba kinachotakiwa kuzungumzwa ni juu ya njia bora za kupambana na vitendo hivyo.

Aliunga mkono hoja ya Jaji Joseph Warioba, kwamba malumbano yanayoendelea juu ya rushwa yanaweza kufikia kiwango cha kuleta mfarakano na uhasama ndani ya jamii yakizidi.

"Nakubaliana na Jaji Warioba, kuwa kazi kubwa mbele yetu ni kuendeleza nchi ili itufikishe kwenye maisha bora kwa kila Mtanzania, kwa kuwa maisha na pato la Mtanzania wa kawaida ni duni," alisema Jaji Bomani.

Alisema malumbano ambayo yatayumbisha jitihada za kumpatia Mtanzania maisha bora, hayana budi kuepukwa, lakini akaonya kuwa uhuru uliopo wa kutoa mawazo unatakiwa kulindwa na kuondoa mazingira ya kutisha watu wasitoe maoni yao na kuwasihi Watanzania wote kuwa na uvumilivu wa kisiasa.
Source: Majira 02-10-2007
 
Mkuu heshima mbele, look at this kwa umri walionao sasa hivi Zitto, na DR. Slaaa, wana at least another 30 years ya kutusumbua CCM, sasa what an opportunity kutawala for the next 30 years bila makelele, maana watuhumiwa wanasema wako safi na wanataka kwenda mahakamani, huko wakishinda ina maana utakuwa ndio mwisho wa Zitto, Dr. Slaa na upinzani kwa ujumla, I mean kaput bin finish, maana after that hakuna mbongo mwenye akili timamu atakayewasikiliza tena, wao wala kiongozi yoyote mpya wa upinzani maana kazi yetu CCM itakuwa ni kuwakumbusha tu kila ukifikia uchaguzi kuwa hawa ni wahuni tu kazi yao ni kutengeneza majungu yaliyoenda shule, sasa hizi nyimbo za msiende mahakamani exactly anayezianzisha ni nani? Wasiende mahakamani under who's expense kama sio sisi wananchi walalahoi?


Mkuu Rwabugiri,

Heshima mbele mkuu, I am down na your theory kusiwe na dhamana ili wasiharibu ushahidi:-

Mzee ES,

Nadhani unahitaji kupumzika kama wiki mbili tatu hivi bila ya kuwa na contact na mtandao huu na hata habari za nyumbani maana unapoelekea sio kuzuri kabisa. Bado tunakuthamini na tunahitaji kichwa chako kikiwa kimetulia. Nilidhani wewe ni mwana demokarasia lakini hizi hadithi za kuwamaliza kina Zitto na upinzani ili "wasiwasumbue" zinaumiza kichwa kidogo.


Unaonaje ukajivinjari mitaa ya Belize ama mambo ya Carribean na mama na watoto.


Tanzanianjema
 
Kabla ya kulipuka na kuwavaa wazee wetu hawa wawili yaani Mzee Bomani naJaji Warioba ni vizuri tukawaelewa psych zao na suala zima la mustkabali wa nchi yetu.

Kwanza kabisa ni lazima tujuwe kuwa hawa wote walikuwa katika timu ya walioshindwa mchakato wa CHIMWAGA. Hivyo ni wazi kuna kaenjoyment fulani katika wanayosema hata kama nao pia wameingizwa katika kundi la mafisadi haswa Mzee Warioba ingawa yeye ni kama kafisadi kadogo.

Lakini vilevile ni wazi kuwa hawa wazee wetu ni wanachama waadhimu wa tabaka tawala na wametumia muda wao mwingi wa kuishi ama kujenga au kulinda mfumo kandamizi tulionao hapa nyumbani ambao ndio unaozalisha huu ufisadi tunaoambiwa. Kuwa kwao katika kundi la watawala kunawafanya wawe na wasiwasi sana na mambo yanvyokwenda maana wao wangependa kuona mabadiliko lakini ambayo yataendeleza masiha ya tabaka tawala na sio kubomoa tabaka hilo kama alama za nyakati zinavyoonyesha.

Vilevile wao kama wanachama adhimu wa tabaka tawala ambao kuwepo kwa amani na utulivu kunahakikisha kuedumishwa kwa maslahi yao na familia zao wasingependa kuona kuanguka kwa legitimacy ya nguzo za dola ikiwemo nguzo ya URAIS. Wanajua wazi kuwa kwa hali inavyokwenda hadi kufikia watu kumuita kipenzi cha asilimia 80% ya watanzania kuwa ni fisadi tena mbele ya hadhara na zaidi kutokea magazeti kuandika hayo kwa mapana yake ni wazi legitimacy ya UONGOZI wa nchi na asasi zote za dola inaelekea kuporomoka kwa kasi. Yeyote anayekula kuku kutokana na mahusiano mazuri na tabaka tawala hatakuwa tayari kuona hilo likitokea. Hakuna anayetaka kuambiwa nini matokea ya hali kama hii. Mifano ni mingi.

Bahati mbaya ni kuwa kukubali kwao kuliongelea suala hili na kutumika kwa maneno yao kujaribu kuhalalisha ufisadi unaodaiwa kunakofanywa na WAHANDISI wetu wa habari kunawafanya nao wajipake matope ya ufisadi huo. Mwisho wa siku na pia watakuwa kundi moja na wale wanaohaha kusurvive kimbunga hiki na itafika wakati nchi inahotaji busara zao lakini hakutakuwa na wa kuwasikiliza.

Tusishangae tukaanza kusikia WARLORD ROSTAM AZIZ, WARLORD LOWASSA na Kamanda KARAMAGI wakipita vifua mbele huku hatima ya Tanzania ikawa mikononi mwao. Kina MZee Bomani wanayaajua haya na wanajua kuwa ikifika hapo nyumba za mwanzo kugongwa hodi ni zao. Hawako tayari kwa hilo.

Tanzanianjema
 
Nafikiri tumeshafika point of no return. Wananchi hawana imani tena na mahakama,Bunge chama tawala na serikali yake. Imani kwa vyombo vya dola alikadhalika, watu hawataki kujisumbua kwenda mahakamani, tume ya kuzuia rushwa wala polisi. Hivi tumebakiza nini wakuu...?


Kuingia msituni, then heshima itakuwa mbele
 
Bomani na Warioba wanajua kuwa kwenda mahakamani, matokeo yake yatachukua muda (not less than two years). Waliotajwa wanajua hilo. They are buying time. Nahisi hawa wazee wanajaribu kutoa ujumbe kwa Mkuu wao kuwa anahitajika kufanya kitu kurejesha imani ya chama chake na vilevile yeye mwenyewe kwa umma kwa ujumla. Siyo busara kutuma mwawaziri kwenda mkoani kujaribu kutetea walichofanya.

Wakati Zitto alipopeleka motion yake bungeni, kilichotakiwa kufanyika ilikuwa kujadili hoja kikamilifu na kutoa maamuzi baada ya hapo ndiyo iletwe hoja ya kusema kama amedanganya.
 
Kuambiwa kapewa fedha na Irani ilikuwa ni KUCHAFULIWA JINA (ndivyo alivyong'aka JK), nawe wasema halikuwa jambo baya?

Mkuu Moshi,

Heshima mbele mkuu, nimesema kuchukua hela Iran, ni sawa na kuchukua hela London, unless kuna something sielewi?

halafu viongozi wezi wa CCm unawakomalia nyani mchana ni pamoja na mstaafu ambaye huwa unamtetea kwa nguvu zako zote, kwa sababu ni mkatoliki na ameoa nyumbani!

Cool down mkuu, haya ni mapambano ya kifikra haya!
 
Thamani ya shilingi, katika siku za karibuni, inaonekana kupanda kulinganisha na dola.

Possible reasons:

A. Kutokuwepo kwa Gavana - akijiuguza;
B. Kazi nzuri ya Profesa Ndulu & Co. kwa muda mfupi;
C. Moto wa ufisadi uliopo kwa sasa
D. None of the above.

Any comment?
 
Mwewe,
Dola imeporomoka katika soko la dunia. Pia huenda Tanzania ina export bidhaa zaidi nje. Hizo zinaweza kuwa baadhi ya sababu.
 
Heshima mbele mkuu, nimesema kuchukua hela Iran, ni sawa na kuchukua hela London, unless kuna something sielewi?

Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuchukua hela kutoka Iran (ambayo Inaitwa na US outpost of tyrany, member wa axis of evil na sponsor of terror) na kuchukua hela kutoka London, kilichosawa ni kuwa hela ni zilezile, watu wa London at least tunajua pesa zinavyolipwa kwao. wanaweza kuataka kuchimba madini kiulaini au watataka kitu ambacho hakitatutia matatani. Lakini watu wa Iran hatuna uhakika. Unaweza kushangaa siku wanataka Tanzania iwe nchi ya kiislamu na tuanze kufuata sheria ya sharia. Na hata siku moja siwezi kukubali kuwa wa-Iran wanatupenda sana, ndio maana wanasaidia hata Chama cha mapinduzi na wagombea wao. Hapa ukijiuliza unakuwa na wasiwasi
 
Ukiona mtu aliekuwa mwanasheria mkuu anashauri watu wasitumie mahakama kudai haki zao, ninachokiona hapo ni kuwa tupo ktk hali mbaya sana bora turudi zama za ujima.........
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuchukua hela kutoka Iran (ambayo Inaitwa na US outpost of tyrany, member wa axis of evil na sponsor of terror) na kuchukua hela kutoka London,

Heshima mbele mkuu, kama ninakupata vizuri ni afadhali mkoloni mzungu kuliko mwarabu, na kwamba US wakisema Mobutu ni safi basi ni safi tuuu, wakisema Chavez hafai basi hafai kabisaa,

Ahsante Mkuu Wangu!
 
Mtu mwenye akili timamu anaposimama mbele ya waandishi wa habari au waandishi wa habari wakisimama mbele yake, naye akasema kuwa taarifa fulani zimemchafulia jina, na watu fulani wamemshushia hadhi katika jamii; halafu akatangaza kwa kujiamini kuwa atakwenda mahakamani ili haki itendeke na ili "asafishe jina lake" basi watu wanatarajia kuwa mtu huyo mwenye akili alikuwa anamaanisha alichosema.

Wakati Rais Kikwete alipodaiwa kuwa amepokea fedha karibu milioni 20 kwa ajili ya kampeni yake toka Iran, alikana tuhuma hizo na akasema atakwenda mahakamani. Hakwenda.

Sasa kina Karamagi, Mgonja, na Rutabanzibwa wanapotishia kuwa watakwenda mahakamani, sioni sababu kwanini kuna mtu anawashauri wasiende. Naelewa motivation ya kufanya hivyo (kulindana) lakini sioni sababu ya msingi ya kutofanya hivyo. Kama kweli wanaamini maneno ya Dr. Slaa yamewakashfu na kuwaharibia sifa mbele ya jamii wanayo haki ya kwenda kutafuta uamuzi wa kisheria ili Dr. Slaa athibitishe madai yake.

sasa watu hawa wenye akili timamu waliotishia kwenda mahamani, na bila sababu ya maana wakaamua kutokwenda mahakamani, basi wataonekana hawakumaanisha walichosema.
 
Isije ikawa ni janja yake paka, wanamtuma Bomani anajifanya kuwashauri wasiende mahakamani, kumbe walikuwa hawana mpango wa kwenda huko ilikuwa ni njia ya kujikosha tu!, sasa wanatafuta pa kutokea kwamba tumeacha kwenda mahakamani kwa vile tumeshauriwa hivo!!

Hebu nendeni muache kutuchezea akili ebo!

Rwabugiri,
nakubaliana na mawazo yako,huyu Bomani katumwa na hao watu,maana nguvu ya kwenda mahakamani hawana,japo wametangaza kwenda ili kuhadaa wadanganyika.
 
Mtu mwenye akili timamu anaposimama mbele ya waandishi wa habari au waandishi wa habari wakisimama mbele yake, naye akasema kuwa taarifa fulani zimemchafulia jina, na watu fulani wamemshushia hadhi katika jamii; halafu akatangaza kwa kujiamini kuwa atakwenda mahakamani ili haki itendeke na ili "asafishe jina lake" basi watu wanatarajia kuwa mtu huyo mwenye akili alikuwa anamaanisha alichosema.

Wakati Rais Kikwete alipodaiwa kuwa amepokea fedha karibu milioni 20 kwa ajili ya kampeni yake toka Iran, alikana tuhuma hizo na akasema atakwenda mahakamani. Hakwenda.

Mkuu MMJ,

1. Heshima mbele, hawa viongozi wetu na vyama vyetu vya siasa wana matatizo makubwa sana inapokuja kwenye ushauri wanaopewa na washauri wao. Ukiangalia kwa makini sana utaliona hilo kuwa ni tatizo kubwa sana, hawa walizoea enzi za Mwalimu, hakukuwa na maswali na hata yalipokuwepo Mwalimu aliweza kuyazima bila kelele,

2. Mwinyi, alikuwa the most smartest wa ku-deal na maswali, ambapo pia alinifundisha the best startegy ya kuongoza, yaani kutishia kujiuzulu au kwamba utaachia ngazi, ndio hasa njia aliyoitumia kututawala, viongozi wengi wa juuu walikuwa wakiogopa kuwa akijiuzulu itakuwa sio sawa politically, maana itaonekana ameshinikizwa na bara, na hivyo kutia dosari muungano, halafu besides, wananchi tulikuwa bado hatujaamuka kama sasa kwa hiyo yeye alipata mteremko sana katika term zake mbili.

3. Kwa mara ya kwanza kuonja sumu ya wananchi, alikuwa Mkapa, sasa kutokana na kutokuwa na mazoea ya kujibu maswali ya kukosolewa kisiasa, na the fact kwamba yeye sio mwanasiasa yeye alileta ubabe tu, na hivyo kuwafanya wananchi kuwa more curious kuwa anaficha nini na huu ubabe wake? Yeye aka-manage ku-survive kwa kuutengenza uchumi aliokuwa anauchukua mwenyewe na familia yake, lakini akafanya one good thing iliyonusuru urais wake, aka-create middle-class, kwa hiyo bongo ikawa kama ni njaaa ni yako peke yako sio na mimi, the only problem aliyoi-create in the process ni kuongeza gharama za kugombea uongozi wa CCM,

4. Now ikawa zamu ya transition, Muungwana aakamua kuchukua hela kila mahali alipoweza kuweka mikono yake kwa ajili ya kampeni, na one of them ikawa Iran, sasa kama nilivyosema kuwa hakuwa na sababu ya yeye kukataa kabisaa, isipokuwa ni washauri wapuuzi ambao hawakuzoea kuulizwa ndio waliomshauri ujinga huo wa kukanusha, it was pure nonesense on his part Muungwana kukanusha kuwa hachukui hela toka Iran, kwa sababu shirika la ujajusi la Uk na yote mengine ya nje yalikuwa yakifuatilia kwa makini ule uchaguzi na kampeni nzima kwa ujumla, walijua kuwa Rostam ambaye ana asili ya ki-Iran ndiye aliyekuwa akizileta hela hizo, na walikasirishwa sana pale Salim, alipoanza kushambuliwa na kambi ya Mtandao kuwa ni Mhizbu, ndio wakaamua kuachilia zile nformation kule London maana walisemakuwa wantaka balance kwenye uchaguzi ambao wao waliouona kuwa hauna balance kwa jinsi Mtandao walivyokuwa wakiwabamiza wapinzani wao,

5. Na pia kwenye kikao cha wawekezaji wa nje na Mkapa, walimwambia wazi wazi kuwa hawategemei, Rostam kuwa one of the powers wa serikali inayokuja, ingawa ni the power anyways sasa hivi, my point ni kwamba Muungwana hakuwa na sababu yoyote ya kukanusha ilikuwa ni error ya washauri wake, kwa sababu vyama vyote vilikuwa vikichukuwa hela toka nje, sasa what was wrong na yeye kuchukua hela toka nje?

Mpaka pale tutakapokuwa na campaign finance laws ambazo sijui hata kama tunazo so far, na hili tatizo la ushuri wa siasa unaliona hata sasa serikali inavyohangaika na a very simple ishu ya Dr. Slaaa, walichohitaji kufanya ni Muungwana kukaa chini na kuwaita viongozi wote waliotuhumiwa kuwa waseme ukweli kama kweli wanahusika na hizo tuhuma au hapana, wakikataa basi waende mahakamani wakikubali basi wafukuzwe kazi, na ikibidi wapelekwe mahkamani, lakini wanachofanya sasa hivi binafsi sielewi bado, sielewi Warioba na Bomani, wanatokea angle gani wanaposema wasiende mahakamani, kinachoendelea sasa hivi ni pure insanity!

Anything les ya kwenda mahakamani ni upuuzi hata kuujadili, ni waste of time, wanasheria wakuu wa serikali yetu wa zamani wanpokataa kwenda mahakamani na ishu nzito kama hii ya sheria, inakwambia nini kuhusu miaka yote ya nyuma tulivyokuwa tukiongozwa? Ina maana tulikuwa tukiongozwa na magoi goi!
 
Kama hawaendi mahakamani kujisafisha, ni vyema wakajiuzulu, hatuwezi kulea majizi, mafisadi na majambazi ya mali ya umma.

Bomani ana-act smart na akili zetu tu hapa anataka kutupumbaza. Hellllll noooo!!!!! Chungu kisha vunjwa kazi kubwa!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom