Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
SEHEMU YA 01
“Wewe una hoja Martha, kumbe unajua chakula kizuri...nikuambie kitu mke wangu.”
Martha alipoisoma meseji hiyo, akaguna kwanza, akamjibu”
“Mh! Nimekuwa mkea mara hii jamani?”
“Kwani umeboreka kukuita hivyo?”
JIACHIE MWENYEWE SASA…
Martha hakujibu haraka, Roi akawa na presha kubwa ya kutaka kuiona meseji iliyofuatia msichana huyo angejibu nini...
“Si vibaya ila....”
“Ila nini tena?”
“Basi tuyaache kwanza.”
“Sawa, nahitaji nikuone leo jamani,” aliandika Roi.
“Leo?”
“Ndiyo! Mbona umeshtuka hivyo mke wangu?”
“Kwa leo hapana.”
“Mpaka lini?”
“Labda siku nyingine.”
“Ndiyo nataka kuijua hiyo siku nyingine.
“Ila si nimekwambia nitakwambia jamani!”
“Basi sawa, hakuna tatizo.”
Katika kila hatua aliyokuwa akipiga, Roi alijiona kuwa mshindi, uzuri wa Martha ulikichanganya kichwa chake mpaka kufikia hatua ya kumuona mjinga mwanaume aliyezaa naye na kisha kuuacha mzigo mzuri kama ule ukiondoka zake...
Siku hiyo alifanya kazi harakaharaka, kitu pekee alichokuwa akikihitaji ni kutaka kuzungumza na msichana huyo tu. Alipomaliza kazi zake, akaondoka. Ilipofika usiku kama kawaida yake akachukua simu yake na kumtumia meseji.
“Jamaniiiiiii....” alianza kumchokoza...
“Nini tena kababaaaa?”
“Hata kunikumbuka!”
“Nilikuwa bize kidogo.”
“Naomba nikupigie basi niisikie sauti yako.”
“Nipo kwenye kelele, nitakushtua.”
“Sawa.”
Roi akabaki akiwa na presha kubwa, kila wakati alipokuwa akimkumbuka Martha, mwili wake ulikuwa unamsisimka kupita kawaida. Hakujua kama alikuwa amempenda mwanamke huyo au alimtamani, lakini kila wakati alihisi kuwa na hamu ya kutaka kuwasiliana naye..
Alisubiri meseji ya Martha mpaka zilipopita dakika thelathini, akasikia mlio wa meseji, kwa haraka sana huku akiwa na presha tena akikenua meno yake akaiwahi simu, akaichukua na kufungua meseji. Hakuwa Martha, alikuwa rafiki yake Sudi ambaye alimshtua kwenda kuchukua hela yake aliyokuwa akimdai.
“Mjinga kweli huyu mtu, watu tupo kwenye presha, yeye anatushtua tu, na hiyo hela abaki nayo,” alisema Roi kwa hasira na kumalizia na msonyo mkubwa. Baada ya hapo, wala hazikupita dakika nyingi, Martha huyo simuni.
“Nipigie sasa,” ilisema meseji aliyotuma Martha.
Roi hakutaka kupoteza muda, alijiona kama angechelewa vile, kwa haraka sana akaanza kumpigia Martha simu, ikapokelewa, Roi akashusha pumzi ndefu na nzito.
“Mambo,” ilisikika sauti nyororo ya Martha....
“Poa, mzima mke wangu...”
“Mi mzima sijui wewe kababaa.”
“Nipo poa. Nimekumisi sana wangu, unanibania kweli kukuona,” alisema Roi.
“Unasema kweli?”
“Ndiyo. Nimekukumbuka mno. Nataka nikuone, lini utakuwa tayari?”
“Sijajua, nina kazi zinanibana sana kwa sasa.”
“Kwa hiyo hatutaweza kuonana?”
“Nitaangalia.”
“Ushaanza.”
“Nimeanza nini tena?”
“Tangu siku ile umesema utaangalia, huko kuangalia hakuishi tu?”
“Hahaha! Sawa, nitakujibu kesho, usijali.”
“Sawa. Ila nikwambie kitu?”
“Niambie tu.”
Una sauti nzuri sana, nampa pongezi mama aliyekuzaa, hata Mungu kakupendelea sana,” alisema Roi, sauti yake ilisikika kimahaba....
“Hahaha! Nashukuru jamaniiii...”
“Upo wapi sasa hivi?”
“Nipo kitandani, nimejiachia tu.”
“Upo na nani?”
“Peke yangu, halafu kuna kibaridi, si unajua mvua zinazoendelea, natamani ningekuwa na mtu hapa,” alisema Martha maneno yaliyompagawisha Roi...
“Nielekeze nije.”
“Mmh! Hapana. Usiku sana sasa hivi!”
“Si nachukua bodaboda tu...”
“Hapana bwanaaaa, usiku ushaingia,” alisema Martha, wakati akiongea na Roi kipindi hicho, tayari mwanaume huyo alishainuka kitandani, alikuwa akivitafuta viatu vyake kwa kuona kwamba angekubaliwa kwenda...
“Sawa. Basi tutazidi kuwasiliana.”
“Hakuna tatizo kababaa...”
Roi akakata simu, alikuwa hoi bin taabani, alipojiangalia, hakujiona kama alikuwa vizuri, akainuka pale alipokuwa na kwenda bafuni kuoga. Sauti ya Martha iliutetemesha moyo wake, mwili wake ulisisimka sana...
Kila alipokuwa akizungumza naye alichanganyikiwa zaidi mpaka kufikia kipindi akawa halali vizuri kwa kumkumbuka msichana huyo...
“Yaani simuelewielewi, anaingia bandani, anatoka, anaingia, anatoka, ila poa tu, akiingia tena, nafunga banda,” alijisemea Roi huku akijiandaa kulala na kichwa chake kikiwa kimechanganyikiwa kwa mwanamke huyo.
ITAENDELEA