Raphael Thedomiri
JF-Expert Member
- Sep 1, 2019
- 442
- 728
Wizara ya Ulinzi ya Taiwan imesema jeshi la China limetuma ndege 71 za kivita na meli saba katika kile ilichokiita "maonesho ya saa 24 ya uchokozi" dhidi ya kisiwa hicho.
Taiwan imesema ilifuatilia hatua za China kupitia mifumo ya makombora ya ardhini na kwenye vyombo vyake vya majini.
Beijing imekasirishwa na namna ambavyo Rais wa Marekani Joe Biden anavyoichukulia Taiwan hasa baada ya kusema kwamba Washington itailinda Taiwan kijeshi.
Hapo jana, China ilifanya luteka za kijeshi karibu na Taiwan kujibu kile inachosema ni "chokochoko na njama" kati ya Marekani na kisiwa hicho kinachojitawala.
China inadai Taiwan ni sehemu ya milki yake na imeweka wazi kwamba ikibidi itakinyakua kwa nguvu na katika siku za karibuni imeongeza shinikizo la kijeshi, kidiplomasia na kiuchumi dhidi kisiwa hicho.
chanzo
dw.
Taiwan imesema ilifuatilia hatua za China kupitia mifumo ya makombora ya ardhini na kwenye vyombo vyake vya majini.
Beijing imekasirishwa na namna ambavyo Rais wa Marekani Joe Biden anavyoichukulia Taiwan hasa baada ya kusema kwamba Washington itailinda Taiwan kijeshi.
Hapo jana, China ilifanya luteka za kijeshi karibu na Taiwan kujibu kile inachosema ni "chokochoko na njama" kati ya Marekani na kisiwa hicho kinachojitawala.
China inadai Taiwan ni sehemu ya milki yake na imeweka wazi kwamba ikibidi itakinyakua kwa nguvu na katika siku za karibuni imeongeza shinikizo la kijeshi, kidiplomasia na kiuchumi dhidi kisiwa hicho.
chanzo
dw.