Nilikuwa naomba mawazo yenu. Linapokuja swala la bidhaa feki yaani (counterfeit goods), watu wengi tunanyooshea kidole China. Na hii imeharibu sana image ya China kwa kuharibu fikra za watu kwamba kila kitokacho China ni feki. Ukweli ni kwamba China inasupply ulimwengu mzima na kwa mjibu wa tafiti inaelekea wanatengeneza bidhaa zinazozidiana ubora. Zile za soko la Ulaya na Marekan bora zaidi na za nchi ya dunia ya tatu duni. Kwa Tanzania nini tunaweza kufanya kuepukana na tatizo hili kama walaji(consumers), na serikali ifanye nini. Kuna wadau huwa wanapendekeza kugomea bidhaa za China, hii inawezekana bila athari yoyote? Nawasilisha