Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,876
China leo imefanya maombolezo ya nchi nzima kuwakumbuka maelfu ya watu waliopoteza maisha kutokana na virusi vya corona. Bendera za taifa zimepepea nusu mlingoti nchi nzima pamoja na kusitisha shughuli zote za burudani.
Siku hii ya maombolezo iliambatana na kuanza kwa sherehe za kila mwaka za kuwakumbuka mababu wa zamani nchini China.
Sherehe za leo zilianza kwa nchi kukaa kimya kwa muda wa dakika tatu, ili kuomboleza waliofariki, wakiwemo wafanyakazi wa afya waliokuwa mstari wa mbele na madaktari.
Magari, treni na meli zilipiga honi na sauti za ving'ora zilisikika hewani. Rais wa China Xi Jinping na viongozi wengine walitoa heshima zao za kimya mbele ya bendera ya taifa mjini Beijing.
Zaidi ya watu 3,000 China bara walifariki dunia kutokana na COVID-19.
Siku hii ya maombolezo iliambatana na kuanza kwa sherehe za kila mwaka za kuwakumbuka mababu wa zamani nchini China.
Sherehe za leo zilianza kwa nchi kukaa kimya kwa muda wa dakika tatu, ili kuomboleza waliofariki, wakiwemo wafanyakazi wa afya waliokuwa mstari wa mbele na madaktari.
Magari, treni na meli zilipiga honi na sauti za ving'ora zilisikika hewani. Rais wa China Xi Jinping na viongozi wengine walitoa heshima zao za kimya mbele ya bendera ya taifa mjini Beijing.
Zaidi ya watu 3,000 China bara walifariki dunia kutokana na COVID-19.