China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

safi mkuu. vip kwenye swala la exportation unauzoefu....!?
Hapana , sina uzoefu wa kutosha japokuwa nimeeleza ABC za kuexport na mambo ya kuzingatia. Fuatilia uzi huu comments zilizopita. AHSANTE
 
Ninataka kutengeneza√ print nguo za clothline yangu pamoja na stationary line.Nimejaribu kufuatilia Nikaambiwa wasanii wengi wanafanyia China.Unaweza kusaidia kunipa mwanga kuhusu hili na gharama zake zikoje mkuu.
Unataka kununua materials na uje ufanye printing mwenyewe Tanzania au unataka kila kitu kifanyike China ,wewe ubebe tu mzigo baada ya kutengenezwa?
 
Mimi sijafika China lakini haiwezekani upewe viza ya kuingia Tanzania uende Dodoma eti Arusha usiruhusiwe siyo kweli, kwanza kwa maelezo yake nakataa kabisa kama huyu mtu kweli aliwahi kusafiri nchi hizo unless atuambie wakati anaandika alikuwa amelewa.

Ngoja nijibu Hii kama ulishawahi jibiwa sorry... Nikwamba hongkong iko ndani Ya china ila ina mambo Yake na sheria zake Tofauti na mainland so ukitaka kwenda Guanzoh kutokea hongkong Lazima uwe na viza tena ulichukua Tanzania ..zamani walikua wanatoa hapo hongkong lakini baada Ya watanzania wengi kupata matatizo ya unga wakazistopisha ..so wengi uwamua kutumia za Shenzhen ili kuingia Guanzoh ....anatoka hongkong anajifanya anaenda Shenzhen so akishuka Shenzhen hatoki nje anapata treni hapo hapo Ya kwenda Guanzoh ila wanatoa visa Ya siku tano tu...sasa omba usipate msala huko Guanzoh ukikutwa na Iyo visa ya Shenzhen ni majanga kwako
 
Unataka kununua materials na uje ufanye printing mwenyewe Tanzania au unataka kila kitu kifanyike China ,wewe ubebe tu mzigo baada ya kutengenezwa?
Yaani mimi ninataka mzigo uliokamilika tu.Kila kitu kifanyike China.
 
Habari wana jukwaa,

Kumekuwa na ongezeko kubwa la wafanyabishara kutoka Tanzania kwenda China kufanya biashara mbalimbali kama nguo, vipuri vya magari na pikipiki, vifaa vya electronics nk. Najua kuna thread nyingi zimewahi kuzungumzia biashara za China, lakini nimuombe mkuu Invisible aifanye hii iwe sticky thread ili iwe refernce point kwa kila anaehitaji kufanya biashara China.

Nitaeleza KIDOGO Kuhusu biashara za China.

BIASHARA YA NGUO:
hii inapendwa sana kufanywa na kina dada japo wanaume pia wapo. Wengi walio wageni na biashara hii wamejikuta wakipata hasara hasa wanapofika tu miji kama Guanzhou na kuanza kununua nguo bila kuangalia hali ya soko Tanzania ikoje.

Hujikuta wakinunua nguo on their perspective and not customers perspective! Kinachowavutia machoni mwao ndicho wanachonunua kwa matarajio watauza tu. Wengine wananunua na wanapofika na mzigo kariakoo wanakuta mzigo kama huo uloshaingia a week/month before hivyo kujikuta wanauza kwa bei ya hasara.

Ushauri: Jaribu kutafuta wateja kabla Tanzania , wakupe order na sample kisha ukifika China nunua kile walichokuagiza.Pia jitahidi ujue ni fashion gani bongo iko sokoni na mpaka mzigo umefika bongo,je bado hiyo fashion ulionunua itakuwa inauza? Mind you kwamba biashara ya nguo hasa za WANAWAKE zinaendeshwa kwa nguvu ya soko na fashion hubadilika mara kwa mara!Biashara ya nguo za watoto au wanaume kidogo fashion zake zinakaa muda mrefu ukilinganisha na za wanawake.

BIASHARA YA VIFAA VYA ELEKTRONIKI
kama simu na accessories zake, music system n.k

Miji mizuri ya kununua mzigo kwa biashara hii ni Shenzhen na Honkong ,japo mji wa Guanzhou pia ni maarufu isipokuwa fake products kwa Guanzhou ni kubwa zaidi. Changamoto kubwa ya biashara hii ni FAKE PRODUCTS. Angalia wateja wako ni watu wa namna gani. Most low income earners ambao kwa Tanzania ndio wengi, wanapenda cheap price.

Kwahiyo, ukinunua genuine products huwezi kuuza bongo kwa sababu bei itakuwa iko juu na wao watashindwa. Kwa hiyo jua needs and wants za customers wako kabla hujaamua kununua mzigo. Kwa mtu mwenye mtaji mdogo unaweza kuanza na kununua phone acssesories na simu chache tu za bei ya chini, utakuwa unaongeza idadi ya simu kidogo kidogo kadri mtaji unavyokua. Pia kama una mtaji mkubwa unaweza kuingiza used products kama photocopier machines ila jitahidi uwe na orders kabla hujaleta kwa sababu ukija nazo nyingi bila order zinaweza kukaa muda mrefu ukajikuta unaanza kula mtaji.

Wakati unasafirisha photocopier machines jitahidi ununue vitu vidogo vidogo kama vile memory cards, USB cards, power banks nk na uviweke pamoja ndani ili ukija bongo wakati unasubiri kuuza photocopier machines unauza hivyo vitu vidogo vidogo ili kupata faida kidogo kidogo na kuhakikisha huli mtaji.

Kumbuka hapa utasafirisha kwa meli na huwa wanapima CBM na sio uzito kwa hiyo hivyo vitu vidogo vidogo cost yake ya kusafirisha itakuwa imemezwa na hizo machines.Photocopier machines nimetoa kama mfano wa moja ya bidhaa lakini vipo vimashine vingi tu ambavyo unaweza kusafirisha kama: Mashine za juice ya miwa, hizi zimekuwa na demand kubwa sana kwa sasa Tanzania. Wateja wake wapo , kama utakuwa na mtaji mzuri unaweza kununua hizi na kuleta. Nyingi ni portable na modern. Ni kiasi cha kutafuta orders na kisha kuleta.

Kuangalia bei mbalimbali za bidhaa tembelea:
Find quality Manufacturers, Suppliers, Exporters, Importers, Buyers, Wholesalers, Products and Trade Leads from our award-winning International Trade Site. Import & Export on alibaba.com

Made-in-China.com mobile- Connecting Buyers with China Manufacturers, Suppliers & Products

www.taobao.com (hii ni ya kichina, tumia browser ya google chrome na tumia kitufe cha translation ili ije kwa kingereza)

USAFIRI NA USHAURI:
Zipo kampuni nyingi zinazosafirisha mizigo kwa njia ya ndege na meli. Kampuni kama THE LAND, SILENT OCEAN ni baadhi tu na hizi zina ofisi zao pale pale Guanzhou na bei zake zinatofautiana kutegemeana unasafirisha kwa njia gani yaani ndege au meli. Na unapolipia wao ndio huhusika na clearance na kila kitu, wewe ukifika bongo unachukua tu mzigo wako kwenye Ghala lao.

Website ya baadhi ya makampuni ni:
Silent Ocean Limited - Specialized in International Cargo Shipping

Kampuni hizi nilizozitaja hapa zinahusika na usafiri lakini pia kama utakuwa na lolote unalotaka kujua kuhusu biashara ya China watafute na uwaulize.

Pia wapo hawa jamaa wanaitwa THE BRIDGE wao wamejikita katika kutoa consultancy service kwenye masuala ya biashara na ujasiriamali na wanauzoefu na biashara za china,watafute ikiwa unahitaji kujua lolote kuhusu biashara za china na ujasiriamali kwa ujumla.
Mawasiliano yao ni:
WhatsApp: +8613125094947
Email: thebridgetz@yahoo.com
Facebook & instagram thebridgetz

NAULI: Nauli zinategemea season na pia unataka kusafiri lini. Kipindi cha high season kama, July, August bei zinakuwa juu. Kama kwa mfano unatarajia kusafiri July basi ikifika april kata tiketi mapema . Mara nyingi kunakuwa na offer kwenye mashirika ya ndege kwa hiyo pendelea kutembelea website zao.

Pia nauli inategemea na shirika la ndege unalotaka kusafiria na pia daraja unalotaka kukaa.

Kwa wafanyabiashara wengi hutumia ethiopian airline kwa sababu huwa wanatoa kg nyingi kuliko wengine.

Pita kwa mawakala posta na kariakoo au search google kupata bei mbalimbali za nauli. Unaweza kutenga bajeti ya USD 900-1200 Kwa nauli kwa economy class
Angalia bei za NAULI hapa:
International Flights, Airfares, Tickets - Fly Ethiopian
Qatar Airways
KLM Royal Dutch Airlines – Flights | Vliegtickets | Flüge

MALAZI: Hapa nitazungumzia mji wa Guanzhou ambao ndio wenye wafanyabiashara wengi wa mataifa mbalimbali hasa Afrika. Zipo hoteli za hadhi tofauti, bei kutoka 120 yuan(36,000 Tsh) ikiwa ni bei ya chini labisa na kuendelea kutegemeana na mfuko wako. Maeneo kama "shaobei lu" ni maarufu kwa watu weusi na utakisikia kiswahili kila baada ya hatua kadhaa. Hoteli za pembeni ya mji bei huweza kuwa chini mpaka yuan 100.

Angalia range ya bei za hoteli hapa: GuangZhou hotels: cheap rates in GuangZhou by China Hotels Reservation


CHAKULA: Zipo hoteli nyingi Guanzhou na shenzen zinazomilikiwa na foreigners na wanauza chakula kizuri japo kiko ghali kidogo, ila kama unahitaji chakula cha bei ya chini na ambacho ni HALAL (wengi huhofia kulishwa mbwa,kitimoto,nk) unaweza kula kwenye sehemu nyingi ambazo huuza wachina waislamu wenye asili ya Xinjiang ambao huuza HALAL food kwa bei poa kuanzia Yuan 15(4500 Tsh) na kuendelea kutegemea na aina ya chakula ulichoagiza. Kuwa makini na vyakula mana wale wenzetu huwa wanakula vyakula vingi vya "ajabu ajabu".

LUGHA: Wachina hutumia lugha yao kwa kila kitu. Katika miji ya biashara kama Guangzhou wachina wafanyabiashara huongea kingereza cha mawasiliano(kibovu) ila mnawasiliana na kuelewana. Pia lugha ya ishara inatumika pale panapokuwa na language barrier.

Hata kama hujui kabisa kingereza unaweza kuchagua bidhaa na kisha mkapatana bei. Wenzetu wana utaratibu wa kutumia calculator kukuandikia bei, hivyo na wewe utaandika ya kwako mpaka mtafikia makubaliano. Nashauri download application yoyote ya TRANSLATION kama pleco nk ili ikusaidie kwenye mawasiliano unapokwama andika neno unslohitaji kwa kingereza kisha tafsiri kwa kichina na muoneshe mchina hilo neno, itasaidia kurahisisha mawasiliano

Nimegusa juu juu vitu vichache mno kuchokoza mada ili wengine waongezee uzoefu na iwe msaada kwa kila anaetaka kufanya biashara China.

Karibuni tujadili na kusaidia wengine


Walio sio wachoyo wa mafanikio hivi mbarikiwe....
 
Mkuu shukrani kwa kuorodhesha baadhi ya mashine ila mifano ya mashine ulizotoa ni za kawaida sana,Nilitegemea kwa uzoefu wako ungeniambia mashine simple ya kutengenezea mifuko laini,mifuko ya kaki,mashine ndogo ya kutengenezea vitu kama take-away,mashine ya kutengenezea bic,mashine ndogo za kutengenezea viatu etc,hiyo ni mifano ila nategemea baada ya kusoma uzi huu utanielewa zaidi,Natanguliza shukrani
Naitaji hiyo machine ya kubania glass za juice 0762825501 tuwasiliane nipo mwanza unaweza kunitumia picha zake whatsup
 
Yaani mimi ninataka mzigo uliokamilika tu.Kila kitu kifanyike China.
sawa. Hii kwa kifupi ni kwamba T-shirt zipo itategemea unataka ubora gani, watu wa printing wapo, inategemea tu wewe unataka design ikoje. Naweza kukusaidia katika hilo ukinipa quality, na sample ya design yako kisha nitawasiliana na wauzaji na watatupa makadirio ya gharama zao. Tuwasiliane mkuu.
 
kwa wale wenye uhitaji wa viwanda vya uhakika vya
toothpaste
lotions
hair shampoo/oil/stiming
spray insecticides'

tuwasiliane
 
Much appreciation kwa Kipilipili, mtu kutoa details kama hizi hakuna dought kwamba sio mbinafsi. Tukipata wengi kama Kipilipili naamini tutapiga hatua
 
Habari wana jukwaa,

Kumekuwa na ongezeko kubwa la wafanyabishara kutoka Tanzania kwenda China kufanya biashara mbalimbali kama nguo, vipuri vya magari na pikipiki, vifaa vya electronics nk. Najua kuna thread nyingi zimewahi kuzungumzia biashara za China, lakini nimuombe mkuu Invisible aifanye hii iwe sticky thread ili iwe refernce point kwa kila anaehitaji kufanya biashara China.

Nitaeleza KIDOGO Kuhusu biashara za China.

BIASHARA YA NGUO:
hii inapendwa sana kufanywa na kina dada japo wanaume pia wapo. Wengi walio wageni na biashara hii wamejikuta wakipata hasara hasa wanapofika tu miji kama Guanzhou na kuanza kununua nguo bila kuangalia hali ya soko Tanzania ikoje.

Hujikuta wakinunua nguo on their perspective and not customers perspective! Kinachowavutia machoni mwao ndicho wanachonunua kwa matarajio watauza tu. Wengine wananunua na wanapofika na mzigo kariakoo wanakuta mzigo kama huo uloshaingia a week/month before hivyo kujikuta wanauza kwa bei ya hasara.

Ushauri: Jaribu kutafuta wateja kabla Tanzania , wakupe order na sample kisha ukifika China nunua kile walichokuagiza.Pia jitahidi ujue ni fashion gani bongo iko sokoni na mpaka mzigo umefika bongo,je bado hiyo fashion ulionunua itakuwa inauza? Mind you kwamba biashara ya nguo hasa za WANAWAKE zinaendeshwa kwa nguvu ya soko na fashion hubadilika mara kwa mara!Biashara ya nguo za watoto au wanaume kidogo fashion zake zinakaa muda mrefu ukilinganisha na za wanawake.

BIASHARA YA VIFAA VYA ELEKTRONIKI
kama simu na accessories zake, music system n.k

Miji mizuri ya kununua mzigo kwa biashara hii ni Shenzhen na Honkong ,japo mji wa Guanzhou pia ni maarufu isipokuwa fake products kwa Guanzhou ni kubwa zaidi. Changamoto kubwa ya biashara hii ni FAKE PRODUCTS. Angalia wateja wako ni watu wa namna gani. Most low income earners ambao kwa Tanzania ndio wengi, wanapenda cheap price.

Kwahiyo, ukinunua genuine products huwezi kuuza bongo kwa sababu bei itakuwa iko juu na wao watashindwa. Kwa hiyo jua needs and wants za customers wako kabla hujaamua kununua mzigo. Kwa mtu mwenye mtaji mdogo unaweza kuanza na kununua phone acssesories na simu chache tu za bei ya chini, utakuwa unaongeza idadi ya simu kidogo kidogo kadri mtaji unavyokua. Pia kama una mtaji mkubwa unaweza kuingiza used products kama photocopier machines ila jitahidi uwe na orders kabla hujaleta kwa sababu ukija nazo nyingi bila order zinaweza kukaa muda mrefu ukajikuta unaanza kula mtaji.

Wakati unasafirisha photocopier machines jitahidi ununue vitu vidogo vidogo kama vile memory cards, USB cards, power banks nk na uviweke pamoja ndani ili ukija bongo wakati unasubiri kuuza photocopier machines unauza hivyo vitu vidogo vidogo ili kupata faida kidogo kidogo na kuhakikisha huli mtaji.

Kumbuka hapa utasafirisha kwa meli na huwa wanapima CBM na sio uzito kwa hiyo hivyo vitu vidogo vidogo cost yake ya kusafirisha itakuwa imemezwa na hizo machines.Photocopier machines nimetoa kama mfano wa moja ya bidhaa lakini vipo vimashine vingi tu ambavyo unaweza kusafirisha kama: Mashine za juice ya miwa, hizi zimekuwa na demand kubwa sana kwa sasa Tanzania. Wateja wake wapo , kama utakuwa na mtaji mzuri unaweza kununua hizi na kuleta. Nyingi ni portable na modern. Ni kiasi cha kutafuta orders na kisha kuleta.

Kuangalia bei mbalimbali za bidhaa tembelea:
Find quality Manufacturers, Suppliers, Exporters, Importers, Buyers, Wholesalers, Products and Trade Leads from our award-winning International Trade Site. Import & Export on alibaba.com

Made-in-China.com mobile- Connecting Buyers with China Manufacturers, Suppliers & Products

www.taobao.com (hii ni ya kichina, tumia browser ya google chrome na tumia kitufe cha translation ili ije kwa kingereza)

USAFIRI NA USHAURI:
Zipo kampuni nyingi zinazosafirisha mizigo kwa njia ya ndege na meli. Kampuni kama THE LAND, SILENT OCEAN ni baadhi tu na hizi zina ofisi zao pale pale Guanzhou na bei zake zinatofautiana kutegemeana unasafirisha kwa njia gani yaani ndege au meli. Na unapolipia wao ndio huhusika na clearance na kila kitu, wewe ukifika bongo unachukua tu mzigo wako kwenye Ghala lao.

Website ya baadhi ya makampuni ni:
Silent Ocean Limited - Specialized in International Cargo Shipping

Kampuni hizi nilizozitaja hapa zinahusika na usafiri lakini pia kama utakuwa na lolote unalotaka kujua kuhusu biashara ya China watafute na uwaulize.

Pia wapo hawa jamaa wanaitwa THE BRIDGE wao wamejikita katika kutoa consultancy service kwenye masuala ya biashara na ujasiriamali na wanauzoefu na biashara za china,watafute ikiwa unahitaji kujua lolote kuhusu biashara za china na ujasiriamali kwa ujumla.
Mawasiliano yao ni:
WhatsApp: +8613125094947
Email: thebridgetz@yahoo.com
Facebook & instagram thebridgetz

NAULI: Nauli zinategemea season na pia unataka kusafiri lini. Kipindi cha high season kama, July, August bei zinakuwa juu. Kama kwa mfano unatarajia kusafiri July basi ikifika april kata tiketi mapema . Mara nyingi kunakuwa na offer kwenye mashirika ya ndege kwa hiyo pendelea kutembelea website zao.

Pia nauli inategemea na shirika la ndege unalotaka kusafiria na pia daraja unalotaka kukaa.

Kwa wafanyabiashara wengi hutumia ethiopian airline kwa sababu huwa wanatoa kg nyingi kuliko wengine.

Pita kwa mawakala posta na kariakoo au search google kupata bei mbalimbali za nauli. Unaweza kutenga bajeti ya USD 900-1200 Kwa nauli kwa economy class
Angalia bei za NAULI hapa:
International Flights, Airfares, Tickets - Fly Ethiopian
Qatar Airways
KLM Royal Dutch Airlines – Flights | Vliegtickets | Flüge

MALAZI: Hapa nitazungumzia mji wa Guanzhou ambao ndio wenye wafanyabiashara wengi wa mataifa mbalimbali hasa Afrika. Zipo hoteli za hadhi tofauti, bei kutoka 120 yuan(36,000 Tsh) ikiwa ni bei ya chini labisa na kuendelea kutegemeana na mfuko wako. Maeneo kama "shaobei lu" ni maarufu kwa watu weusi na utakisikia kiswahili kila baada ya hatua kadhaa. Hoteli za pembeni ya mji bei huweza kuwa chini mpaka yuan 100.

Angalia range ya bei za hoteli hapa: GuangZhou hotels: cheap rates in GuangZhou by China Hotels Reservation


CHAKULA: Zipo hoteli nyingi Guanzhou na shenzen zinazomilikiwa na foreigners na wanauza chakula kizuri japo kiko ghali kidogo, ila kama unahitaji chakula cha bei ya chini na ambacho ni HALAL (wengi huhofia kulishwa mbwa,kitimoto,nk) unaweza kula kwenye sehemu nyingi ambazo huuza wachina waislamu wenye asili ya Xinjiang ambao huuza HALAL food kwa bei poa kuanzia Yuan 15(4500 Tsh) na kuendelea kutegemea na aina ya chakula ulichoagiza. Kuwa makini na vyakula mana wale wenzetu huwa wanakula vyakula vingi vya "ajabu ajabu".

LUGHA: Wachina hutumia lugha yao kwa kila kitu. Katika miji ya biashara kama Guangzhou wachina wafanyabiashara huongea kingereza cha mawasiliano(kibovu) ila mnawasiliana na kuelewana. Pia lugha ya ishara inatumika pale panapokuwa na language barrier.

Hata kama hujui kabisa kingereza unaweza kuchagua bidhaa na kisha mkapatana bei. Wenzetu wana utaratibu wa kutumia calculator kukuandikia bei, hivyo na wewe utaandika ya kwako mpaka mtafikia makubaliano. Nashauri download application yoyote ya TRANSLATION kama pleco nk ili ikusaidie kwenye mawasiliano unapokwama andika neno unslohitaji kwa kingereza kisha tafsiri kwa kichina na muoneshe mchina hilo neno, itasaidia kurahisisha mawasiliano

Nimegusa juu juu vitu vichache mno kuchokoza mada ili wengine waongezee uzoefu na iwe msaada kwa kila anaetaka kufanya biashara China.

Karibuni tujadili na kusaidia wengine

Heshima kwako mkuu Kipilipili!
Asante sana kwa Elimu endelevu ambayo unaitoa hapa jukwaani. Naomba unisaidie kujua kitu kimoja, Kule China kuna sehemu inaitwa YIWU ambapo nasikia kuna International market pia kubwa sana. Ni nini uzoefu wako na hii sehemu kwa kulinganisha na Guangzhou, yaani kwa aina ya vitu, ubora, gharama za kununua na kusafirisha mpaka bongo, pamoja na gharama za maisha kule?? Natanguliza shukran tena....ahsante
 
samahan wakuu kwa ku interrupt topic yenu lakin naomben mnisaidie kwa hili mm nkijan mdogo tu kwasasa npo dsm nmejchang nmepata million moja ivyo naombeni ushaur ni biashara gan itanpatia mapene kwa harak au tafadhal
 
Back
Top Bottom