China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

samahan wakuu kwa ku interrupt topic yenu lakin naomben mnisaidie kwa hili mm nkijan mdogo tu kwasasa npo dsm nmejchang nmepata million moja ivyo naombeni ushaur ni biashara gan itanpatia mapene kwa harak au tafadhal
mkuu usijali, topic kama hiyo yako zipo nyingi sana humu JF, naomba search na utapata nyuzi zinazozungumzia business ideas kwa wenye mtaji mdogo
 
Heshima kwako mkuu Kipilipili!
Asante sana kwa Elimu endelevu ambayo unaitoa hapa jukwaani. Naomba unisaidie kujua kitu kimoja, Kule China kuna sehemu inaitwa YIWU ambapo nasikia kuna International market pia kubwa sana. Ni nini uzoefu wako na hii sehemu kwa kulinganisha na Guangzhou, yaani kwa aina ya vitu, ubora, gharama za kununua na kusafirisha mpaka bongo, pamoja na gharama za maisha kule?? Natanguliza shukran tena....ahsante
Mkuu YIWU soko lake ni kama limetawaliwa na waarabu tofauti na Guanzhou ambapo wachina ndio wamelishika soko. Bei za YIWU kidogo ziko juu ulinganisha na Guanzhou ISIPOKUWA vitu vya YIWU vina quality nzuri SANA tena sana ukilinganisha na GUANZHOU ambapo copy ni nyingi sana. Yiwu ukichukua mzigo mkubwa utafaidi sana kwa sababu wale wauzaji hupenda zaidi wanunuaji wa jumla na hasa kama utanunua moja kwa moja kiwandani-Watakupa bei ya kiwandani ambayo kwa kiasi fulani iko Chini tofauti na kama utanunua kiasi kidogo kwenye maduka ya jumla. Kwa hiyo utakuwa umenunua bidhaa nzuri yenye ubora ambayo haitakusumbua sokoni kuuza.
Changamoto ninayoiona YIWU ni usafirishaji, shipping companies zipo ila NIONAVYO mimi kama hazijachangamka kama Guanzhou.
 
Mkuu kipilipili naomba namba yako tafadhali na je vipi saivi uko china au tz?
 
Mkuu , huo mtaji wa 5000 USD( 5000X6.2 &[HASHTAG]#20803[/HASHTAG];= 31,000 &[HASHTAG]#20803[/HASHTAG];)huo ni mtaji mkubwa tu na unaweza kufanya biashara kwa baadhi ya vitu ikiwa tu hiyo itakuwa ni nje ya nauli na pesa ya kujikimu.
BACK TO YOUR QN. Sina current price ya baadhi ya machines lakini unaweza kununua machine zifuatazo kwa mtaji wako:
1. Machine ya kutengeza bisi(popcorn )
2. Machine ya kutengeneza ice cream/ barafu
3. mashine ya kutengenezea juice mbalimbali(juicer). kama machungwa(ninayo MPYA ambayo haitumii umeme, ukihitaji tuwasiliane)
4. Mashine ya kukaangia chips(ninayo MPYA,ukihitaji tuwasiliane)
5. Mashine ya kutotolea vifaranga
6. Mashine ya kubania glasi za juice km take away(ninayo MPYA, ntafute kama unahitaji )
Nk. Wengine wataongezea



NAHITAJI MASHINE YA POP CORN.
 
Sidhani Kama Nakuelewa.

- Mimi Ninachojua Insecticidal Sprays Huwa Zinawekwa Kwenye Makopo Yenye Ujazo Tofauti Tofaui Kama Ilivyo Rungu, Kiboko Nk
nimekuelewa mkuu,nachouliza ni kiasi kwa maana ya quantity.ukichukua kiasi kikubwa bei zao huwa wana kuwachini tofauti na ukichukua kiasi kidogo
 
nimekuelewa mkuu,nachouliza ni kiasi kwa maana ya quantity.ukichukua kiasi kikubwa bei zao huwa wana kuwachini tofauti na ukichukua kiasi kidogo
Hivi Unamaanisha Sprays Zenyewe Au Mitambo Ya Kutengeneza Kiwanda Cha Sprays ?
 
Skukrani kwa kushare uzoefu, kama mtu akitaka kufanya biashara ya kuagiza mikoba ya kike kutoka huko kuja Tz anaweza fata utaratibu gani? naomba kujua kwa yeyote mwenye uzoefu na biashara hii
Naweza kukusaidia bure,kukuelekeza hata kukuunganisha bure.ntafute inbox.
 
T
Nomba unijuze ni kampuni gani ya usafirishaji naweza itumia kutuma mzigo Tanzania ukafika salama bila usumbufu mi niko Xinyang china mwenye taarifa yoyote anijuze nomba anisaidie.
tumia wale jamaa wa Taobao wakutumie mzigo wako mpaka kampuni ya usafirishaji kule guanzhou,jamaa wa guanzhou wakiupokea watakupigia simu ku comfirm then watatuma bongo,mzigo kwa meli huwa wana charge kwa CCBM,kampuni nayotumia nayo huni charge dola 400 kwa cbm moja
 
Nataka vifaa vidogovidogo kama Empty CD, DVD External drive, Flash disk, wino wa photocopy. Kwa vifaa hivi nafikiri naweza nunua alibaba zen nikasafirisha kwa DHL. Mtaji ni Tsh 1M
DHL ni hasara brother,tumia njia ya meli
 
Back
Top Bottom