Huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani. Wakati wa uchaguzi mkuu kama huu,chama kinapaswa kuwa safi na imara kama chuma cha pua. Chama cha Mapinduzi kitaathiriwa vya kutosha na sarakasi za Andrew John Chenge na Anna Kajumulo Tibaijuka juu ya sakata la Escrow. Sarakasi wanazozicheza mbele ya Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma chini ya Jaji Kiongozi Mstaafu,Hamisi Msumi.
CCM iliamua vyema.Ilipokea ubunifu/ushauri toka kitengo cha Itikadi/Propaganda kwamba ni vyema Chenge na Tibaijuka 'washughulikiwe' ili kukisafisha na kukinusuru chama kuelekea Oktoba. Lengo lilikuwa zuri.Ni kuwaaminisha watanzania kwa CCM hailei wakiuka maadili ya chama na kiuongozi wa nchi. Kushughulikiwa kwa Chenge na Tibaijuka kungekuwa msaada mkubwa kwa chama.
Mpango wa chama unaelekea kubuma. Kukwama hadi kiama. Matendo na maneno ya Chenge na Tibaijuka mbele ya Tume ya Jaji Msumi yanadhihirisha kukwama kwa mpango huo. Ijulikane kuwa CCM ina faili la kila mmoja wao lenye nyaraka zote. Tume ya Jaji Msumi itaishia kutoa mapendekezo ya siri kwa mamlaka za kiserikali juu ya Chenge na Tibajuka ambayo pia si msaada kwa chama.
Bado Ngeleja!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
You are absolutely right; Chenge na Anna watakigharimu Chama; nionavyo mimi hayo yatakuwa malipo sahihi kwa Chama chenu kutokana na tabia, mila na desturi ya CHAMA ya kulindana; kufumbia macho maovu; kukosa uthubutu wa kukemea maovu na kuchukua maamuzi magumu na wanachama wote kujihusisha na uovu; kwa kuwa hakuna aliye msafi wa kuweza kumfunga paka mwenzie kengele shingoni; ndio maana Anna na Chenge wanafanya wanayoyafanya kwenye tume!
Tatizo viongozi wetu si wasikivu)
Mzee Tupatupa
Hakuna athari yeyote kwa sababu majimboni kwao wananchi wamejaa tongotongo..nlikuwepo jimbon kwa chenge(Bariadi Magharibi) kule jamaa ni nyoka kweli kweli..mikutano yake ya hadhara ni kufuru,watu wanamshangilia mwanzo mwisho hata alipotoa kauli ya nyoka msaka pesa wasukuma wamemsifu na kumshangilia wanasema ubunge ni mali yake hadi atakapoamua kuacha mwenyewe
Wewe ndiye yule Mwalimu wa Kibasila?
Aliewaloga wananchi jimboni kwa chenge alikufa bila kuacha dawa
Ukweli ndiyo huo,zile hela walipiga wengi, chenge na mwenzie tibaijuka Hilo wanalijua na ndiyo maana wanakomaa.hela zilizopigwa stanbic bank mpaka Leo hakuna majina yaliyowekwa hadharani na ndiyo noma,Tunafahamu tu wa mkombozi bank
Mkuu hapa cchenge hamwagi ugali bali anatumia sheria mbovu walizozitunga wao kujilinda,iliChenge na Tibaijuka wako sahihi kabisa,na waendelee kufanya hivyo..hawezi kuendelea kufanywa kafala wakati wengine walipiga hela ndefu kabisa wameachwa,waitwe wote mpaka wale wa STANBIC,waitwe wapwa na wakwee,,sio kumuonea mama wa watu na Chenge,,,Chenge mwaga ugali ,,wao si wanataka kumwaga mboga
Mkuu hapa cchenge hamwagi ugali bali anatumia sheria mbovu walizozitunga wao kujilinda,ili
kuwalinda wenzake,angelikubali kuhojiwa na kusema au kuhoji wengine wako wapi? tungesema anamwaga
mboga.Huyu ameishajitaja kuwa ni joka lenye makengeza anatumia ujanja wa nyoka
kujiokoa na kuokoa wenzake.
Ni afadhali mama Tibaijuka ameanza vizuri kwa kusema milioni kumi ni hela ya
mboga,kwa wanafasihi watamwelewa kwamba kama hiyo ni ya mboga basi
kuna waliochukua za kununua nyumba mbona hawapo hapa?
Huyu wakimhoji vizuri ndo anaweza kumwaga ugali,
Huyo mwenzake anayekataa kuhojiwa anatumia dhana ya ''Ni upepo tu utapita''.
Mkuu tunataka kuwaona hawa watu kizimbani kisutu.Uliyotaka yameshakuwa. Nini kitafuata?
Huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani. Wakati wa uchaguzi mkuu kama huu,chama kinapaswa kuwa safi na imara kama chuma cha pua. Chama cha Mapinduzi kitaathiriwa vya kutosha na sarakasi za Andrew John Chenge na Anna Kajumulo Tibaijuka juu ya sakata la Escrow. Sarakasi wanazozicheza mbele ya Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma chini ya Jaji Kiongozi Mstaafu,Hamisi Msumi.
CCM iliamua vyema.Ilipokea ubunifu/ushauri toka kitengo cha Itikadi/Propaganda kwamba ni vyema Chenge na Tibaijuka 'washughulikiwe' ili kukisafisha na kukinusuru chama kuelekea Oktoba. Lengo lilikuwa zuri.Ni kuwaaminisha watanzania kwa CCM hailei wakiuka maadili ya chama na kiuongozi wa nchi. Kushughulikiwa kwa Chenge na Tibaijuka kungekuwa msaada mkubwa kwa chama.
Mpango wa chama unaelekea kubuma. Kukwama hadi kiama. Matendo na maneno ya Chenge na Tibaijuka mbele ya Tume ya Jaji Msumi yanadhihirisha kukwama kwa mpango huo. Ijulikane kuwa CCM ina faili la kila mmoja wao lenye nyaraka zote. Tume ya Jaji Msumi itaishia kutoa mapendekezo ya siri kwa mamlaka za kiserikali juu ya Chenge na Tibajuka ambayo pia si msaada kwa chama.
Bado Ngeleja!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Wassira ana uwezo mkubwa kuliko Lowasa,Dr Slaa,Mbowe na Lipumba. Akipewa Nchi leo ataiweka sawa. hakuna Ufisadi wala lelemama.CCM bado Tuko imara sana hasa tukimchagua huyu Tanzania itakuwa nchi ya neema maana watoto wetu watakuwa wanavimbiwa kwa kunywa maziwa , mikate na siaji
![]()
Mada ya kinafiki kutoka kwa mnafiki