Chelewa, Uzikwe

Kudo

JF-Expert Member
Nov 2, 2017
1,809
6,081
RIWAYA; CHELEWA UZIKWE!

NA; BAHATI K MWAMBA

SIMU; 0758573660/0624155629.

DAR ES SALAAM….

Kelele za muito wa simu zilimuamsha katikati ya usiku mnene. Alijivuta kivivu huku akijaribu kushindana na uzito wa macho yake. Aliifikia simu yake na kutazama mpigaji.
Haraka alinyanyuka kitandani na kukaa kitako, huku akibonyeza kitufe cha kupokelea na usingizi ukiwa umempaa.

Masikio yake yalinasa sauti za hekaheka na mihemo ya hofu kutoka kwa mtu aliyepiga simu usiku huo. Licha ya kusikia hekaheka hizo, lakini aliamua kukaa kimya kama alivyokuwa amefanya mpigaji.
Udadisi mwingi kuhusu kilichokuwa kikiendelea upande wa pili, ulimfanya atulie kama aliyekuwa amepigwa na shoti ya umeme usingizini, hata mapigo yake ya moyo yalipunguza kasi ya kudunda, ili mradi aweze kusikia kila kilichokuwa kinaendelea.

Licha ya kusikia purukushani nyingi, lakini hakuweza kuelewa ni tukio gani hasa, lililokuwa linaendelea.

Alijikuta akisimama bila kupenda, huku tamaa ya kutaka kuelewa, ikizidi kuichota nafsi yake.

“Nipo matatizoni bwana Zuki!” Hatimae sauti ya mtu upande wa pili ilisema kwa kitetemeshi.

“Unaweza kunieleza kwa uchache?” Zuki aliuliza huku akijaribu kuweka umakini mkubwa, ili aweze kusikia jambo.

“Nimevamiwa nyumbani usiku huu, walinzi wangu wameuawa, familia yangu ipo matatizoni Zuki!” Sauti upande wa pili ilisikika kwa mbali sana, dhahiri muongeaji alikuwa hataki kuongea kwa sauti.

Kuvamiwa kwa yule mtu aliyepiga simu, kulimfanya Zuki Gado p.a.k Miguu ya kuku, apigwe na ganzi kwa sekunde kadhaa.
Kwa nini?

Kwa sababu alimfahamu vema mtu huyo, alifahamu ulinzi mkali aliyokuwa nao pia alifahamu nyumba yake ililindwa saa ishirini na nne tena kwa ulinzi wa kisasa kabisa. Ilikuwa ni ajabu kusikia kumefanyika uvamizi nyumbani kwake, kiasi cha kumfanya akimbia na kujificha.

Ilimshangaza!

“Uvamizi umetokeaje na….” Hakumalizia swali lake, jamaa upande wa pili aliingilia..
“Sijui kilichotokea, lakini kiufupi nimevamiwa na hapa muda wowote watanifikia.. Wanaonekana kuijua vema nyumba yangu” Jamaa aliongea kwa hofu huku dhahiri, akisikika akitetemeka kiasi cha kufanya taya zake zigongane.

“Hapo ulipo unaweza kutoka na ukakimbia?” Miguu ya kuku alimuuliza, huku haraka akichomoka chumbani kwake, akiwa amevaa boksa tu na wala hakujali.

“Naweza na sipo mbali na gari langu”

“Good! Ingia kwenye hilo gari na uondoke hapo haraka sana, lakini usikate simu yako, funga vioo vizuri na ukimbize gari kama umetoka kuiba benki”

“Sawa!” Jamaa alijibu na kukaa kimya. Upande wa pili Miguu ya kuku aliendelea kusikia harakati za yule bwana, akifuata maelekezo aliyompa.

Wakati simu yake ikiwa sikioni, miguu yake ilikuwa inapishana kwa kasi kuelekea kwenye chumba chake cha siri.

Sekunde chache baadae, alikuwa anatungua funguo za gari lake na kuanza kurejea sebuleni kwake.

Wakati wote huo, bado hakuwa amevaa nguo zake na alikuwa amesitiriwa na boksa pekee lakini, mwili wake wote ulikuwa wazi bila nguo.

Alipofika sebuleni akaitua simu yake kwenye sofa, kisha akachukua kompyuta yake iliyokuwa kwenye sofa jingine na kuiwasha.

Ilipowaka, alibonyeza hapa na pale na kisha akaingiza namba za simu yake na namba za yule mtu aliyempigia.

Sekunde chache baadae, aliweza kuona mahali ilipokuwa simu iliyompigia, kupitia ramani ndani ya simu yake.

“Wameniungia kwa nyuma, wako kasi sana….” Jamaa aliongea kwa hofu huku akiwa anatetemeka. Sauti yake ilimfikia vema Miguu ya kuku, kupitia simu yake.

“Vuta pumzi mara tatu na uziachie mara moja, kisha endesha gari bila kutazama viona nyuma” Alimwambia huku yeye akielekea nje.

“Wako kasi sana na wameanza kunishambulia kwa risasi..” Jamaa alilalamika tena.

“Unatumia gari gani?” Miguu ya kuku aliuliza huku akiingia kwenye gari lake na kuliwasha.

“Natumia Vx V8!”

“ Wao umeona wanatumia gari za aina gani?”
“Nahisi ni V8 zile!”

“Sasa tulia na usukani, waachie manyoya. Hawawezi kukupata na vigari vyao!”

“Natetemeka tatizo!”

“Fanya nilivyokwambia, ondoa hofu, nipo njiani”

“Nielekee wapi? Wako nyuma kwa kasi sana aisee!”

Miguu ya kuku aliwaza kidogo, kisha alimiiliza huku akiangalia kwenye simu yake ambayo aliunganisha ili aweze kuona aliyempigia alikuwa sehemu gani.

“Umefika sehemu gani sasa hivi?”

“Niko Moroko, Kinondoni!”

“Basi, elekea Koko”

“Whaat!!”

“Usishangae, elekea Koko beach kisha nisubiri hapo”

“Utatoka Tegeta saa ngapi hadi ufike huku mzee, huoni nitauawa hapohapo Koko!?”

“Leo nililala kwenye nyumba yangu ya Magomeni, ninahakika nitafika kabla hawajakuua!”

“Com'oon Zukii!”

“Sasa utafuata maagizo yangu au nirudi kulala?”
“No! Nitafuata! Nitafuata!”

“Good! Sasa endesha na usiangalie wanaokufuata na usizime simu yako!”

“Lakini hujanambia nikifika huko nifanye nini!”

“Zamisha gari kwenye maji!”

“Eeh!!?”

“Ndiyo! Nenda uingize gari baharini hadi injini yake izime yenyewe”

“Nitakufa Zuki!”

“Hautakufa, ukikaribia kufika washa kiyoyozi hadi mwisho, kisha funga vioo vyote na ukanyage mafuta hadi mwisho ili iwahi kupotelea majini”

“Nitakufa bwana!”

“Unaniamini au huniami?”

“Nakuamini!”

“Fanya niliyokuelekeza. Hutakufa kwa sababu itakuchukua dakika kumi na tano kuanza kupoteza hewa ukiwa ndani ya gari lililoko majini na itakuchukua dakika ishirini zaidi, gari kuingiza maji baada ya vioo kuzidiwa uwezo. Hivyo basi, fanya ninayokuelekeza ila kikubwa, usizime simu yako na ukiizima kweli utakufa, maana sitaweza kukuona ulipo” Miguu ya kuku aliongea huku akiweka simu pembeni na kuongeza mwendo wa gari lake.

Lilikuwa ni jambo la hatari aliloamua kulifanya ili kuweza kuokoa maisha ya mtu aliyempigia simu usiku huo, lakini hakuwa na la kufanya zaidi ya hilo jambo.
“Hatari lakini salama!” Alijisemea huku akiongeza kasi kuelekea kinondoni.

“Nimekaribia kufika, jamaa na wao naona hawajakata tamaa!” Jamaa aliongea kwa kitetemeshi cha uoga.

“Washangaze hao jamaa!” Miguu ya kuku alimwambia huku akikunja kona kupita maeneo ya ubalozi wa Marekani, maeneo ambayo yalitawaliwa na ukimywa mkubwa, lakini yeye hakujali. Ilikuwa ni lazima awahi kufika kwenye fukwe za Koko ili atoe msaada kwa mtu aliyempigia simu.

Gari lake aliliendesha kwa kasi kubwa huku mara chache ikimlazimu kupunguza kasi, ili aweze kumudu kukunja kona. Kila mara macho yake yalikuwa yanatizama simu yake, ili kuweza kupima umbali aliobakiza kufika ufukweni.

Zikiwa zimesalia mita kadhaa ili afike sehemu alipokuwa mtu wake, masikio yake yalinasa sauti za risasi mfululizo. Haraka alizima taa za gari lake, kisha alipapasa kwenye kiti, kushoto kwake na kuibuka na bastola aliyoipenda kuliko bastola zote alizowahi kumiliki.

Ilikuwa ni bastola aina ya USA Colt M1911, bastola ambayo ilikuwa na uwezo anaouhitaji kwenye misukosuko ya aina yoyote ile.

Alipokwisha kuitwaa, alirudisha umakini kwenye kwenye gari, kisha alianza kupunguza kasi ya gari lake huku masikio yake yakizidi kusikia sauti za risasi zikirindima bila mpangilio.

Alisimamisha gari akiwa amebakiza mita mia moja tu, ili awafikie wale waliokuwa wakipiga risasi upande wa bahari.

Aliegesha gari kandoni mwa barabara, kisha aliinyakua simu yake na kushuka ndani ya gari huku bastola ikiwa mkononi, tayari kwa lolote.

Alianza kupiga hatua zake huku macho yake yakiwa makini, kutazama kioo cha simu yake. Lengo lake ajue uelekeo wa ilipokuwa simu iliyompigia.

Alijikuta akisimama baada ya kuona uelekeo wa simu aliyoiunganisha. Uelekeo ulisomeka ni mita zaidi ya mia mbili kutoka pale alipokuwa.

Aliinua macho yake na kutazama kule alikoona mtu wake atakuwepo. Makadirio yake yalionesha tayari mtu yule atakuwa amelitosa gari ndani ya maji, hivyo alikuwa anasubiri msaada wake.

“Kumekucha!” Alisema huku akijaribu kuiweka simu mfukoni.

“Heh!” Alishangaa baada ya mkono kukosa mfuko na alipojitazama, aligundua alikurupuka kitandani bila kuvaa nguo zaidi ya boksa aliyokuwa nayo.

Alitamani kujicheka, lakini wakati haukuruhusu. Alichoamua kufanya ni kupindua pindo la boksa yake na kuipachika simu yake ili aingie mapambanoni kabla ya dakika kumi na tano kuisha.

Wakati akikimbia kwa kuambaa na ufukwe, huku akili yake ikiwa kwa wale jamaa waliokuwa wamesimama na kishambulia baharini, bila kumuona waliemshambulia, masikio yake yaliendelea kumpa tahadhari ambayo tangu awali, hakuwa ameizingatia.

Alisimama na kufumba macho na kuyaruhusu masikio yake yasikie kile ambacho hakuwa amekizingatia.

Gafla alifumbua macho mithili ya mtu aliyeona kibwengo gizani, tayari alikuwa ameshatambua kile kilichosikilizwa na masikio yake.

Milio ya risasi!

Risasi zilikuwa zinatoka kwenye bunduki kubwa na za kisasa, bunduki ambazo hazikuwa zikipatikana hapa nchini na hata kama zilikuwepo, si rahisi kuingia mikononi mwa walugaluga.
“Automatic Riffleman!?” Alishangaa na kujiuliza bila majibu, lakini hakuwahi kutilia shaka uwezo wa masikio yake na utambuzi wa silaha.

“Huu ni mziki ambao unavuka kina!” Alijisemea huku akijaribu kuwaza njia mbadala ili kutokuingia kwenye mapambano ya risasi na watu wale, ambao walionekana kutumia silaha za kisasa zaidi na kwamwe isingelikuwa busara kutupiana risasi.

Alitazama kushoto kwake na kuiona barabara, kulia kwake kukiwa na kingo za maji. Alipotizama mbele aliona gari za wale watu ambao walikuwa bado wanarusha risasi.

Akawaza kufanya jambo!

ENDELEA KUWA NAMI
 
RIWAYA; CHELEWA UZIKWE.

NA; BAHATI K MWAMBA.

SIMU; 0758573660/0624155629.

SEHEMU YA PILI...


Risasi zilikuwa zinatoka kwenye bunduki kubwa na za kisasa, bunduki ambazo hazikuwa zikipatikana hapa nchini na hata kama zilikuwepo, si rahisi kuingia mikononi mwa walugaluga.
“Automatic Riffleman!?” Alishangaa na kujiuliza bila majibu, lakini hakuwahi kutilia shaka uwezo wa masikio yake na utambuzi wa silaha.

“Huu ni mziki ambao unavuka kina!” Alijisemea huku akijaribu kuwaza njia mbadala ili kutokuingia kwenye mapambano ya risasi na watu wale, ambao walionekana kutumia silaha za kisasa zaidi na kwamwe isingelikuwa busara kutupiana risasi.

Alitazama kushoto kwake na kuiona barabara, kulia kwake kukiwa na kingo za maji. Alipotizama mbele aliona gari za wale watu ambao walikuwa bado wanarusha risasi.

Akawaza kufanya jambo!

Haraka na kwa kasi kubwa, alikimbia kuelekea upande wa barabara. Alipofika barabarani alipiga risasi mbili hewani, kisha kwa kasi ile ile aliondoka kuelekea ukingoni mwa bahari na kuachia risasi nyingine mbili.

Alikuwa anacheza patapotea na hisia za watu ambao hakujua walivyojiandaa kuzikabili changamoto. Lengo la mchezo alioufanya ni kuwafanya jamaa waondoke pale na kuacha kushambulia. Alifanya vile ili kuwachanganya na wasijue aliyerusha risasi ni mlinzi wa makuti pub iliyokuwa pale ufukweni, ama ni maofisa wa jeshi la polisi ambao waliamua kujihami, huku wakiwa wanasogea kuwakabili.

Licha ya kucheza mchezo huo ambo ni sawa na mchezo wa kubeti bila kujua matokeo, lakini hakuacha kuendelea kukimbia kuelekea hukohuko walipokuwa adui zake.

Asingeliweza kusubiri matokeo ya alichokifanya, huku akiwa anazidi kupoteza dakika za kumwokoa mtu aliyekuwa amempigia simu.
Kasi yake ilikuwa haipimiki, huku akihema kila baada ya hatua tano. Bastola yake ilikuwa tayari kwa lolote, macho yake yalikuwa sambamba na zile gari za wale watu ambao walikuwa wameacha kushambulia na hakujua walikuwa wameamua kuchukua hatua gani, baada ya kusikia risasi alizorusha.

Akiwa amebakiza mita kadhaa ili afike zilipokuwa gari za wavamizi, masikio yake yaliweza kusikia sauti za miungurumo ya injini za gari, kisha macho yake yaliona taa zikiwashwa na magari kuondolewa kwa kasi kubwa pale ufukweni.

“Oops!!” Alipumua kwa ahueni baada ya zile gari kuondoka na risasi kukoma. Alipumua kwa sababu alijihakikishia kufanya uokozi bila kashikashi yoyote ile. Pia alijihakikishia usalama kwa asilimia zote, licha ya kwamba alikuwa tayari kwa mapambano ya aina yoyote na wale wavamizi.

Miguu ya kuku alichomoa simu kwenye pindo la boksa yake na kutazama umbali ambao alibakiza, kuweza kumfikia mhusika wake.

Kulikuwa na mita kumi tu kutoka nchi kavu. Huo ndiyo umbali ambao ulibaki ili aweze kumfikia. Lakini ili aweze kuzimaliza hizo mita kumi, ilihitaji ajitose kwenye maji na kuanza uokozi.

Miguu ya kuku alikuwa anaweza kuogelea umbali mrefu bila kupumzika, hivyo umbali ambao alitakiwa kufanya uokozi haukuwa kigezo cha kuweza kumzuia kutumbukia ndani ya maji.

Aliitazama simu yake, kisha aliitupia ndani ya maji na hakuwa akiihitaji tena.

Kwa nini?

Kwa sababu alihitaji kuzama majini na asingeliweza kuiacha nchi kavu ili aipitie baadae. Aliona anaweza kuiacha na ikaokotwa na maafisa usalama ambao wangeliweza kumletea matatizo ambayo hakuwa anayahitaji.

Alipohakikisha simu imepotelea chini ya maji na isingeliweza kupatikana kirahisi, nae aliamua kujitosa majini na kuanza kuyakata maji kuelekea sehemu ambayo alikadiria kungelikuwa na gari la yule mtu aliyekuwa amempigia simu.

Alitumia dakika mbili hadi alipoweza kuliona lile gari, ambalo lilikuwa linazama na kuibuka mithili ya kiboko anaekimbiza mtumbwi.

Baada ya kuliona, alizama majini na kuogelea mithili ya Papa hadi alipolifikia gari ambalo bado lilikuwa linazama na kuibuka taratibu sana. Aliligusa hapa na pale na kisha alitoa bastola yake na kulenga loki ya mlango, kisha aliachia risasi moja na mlango ukaachia na kufanya maji yaingie kwa kasi ndani ya gari.

Haraka aliingia na kukutana na mtu ambae alikuwa anahangaika kujitoa kwenye mikanda iliyokuwa imemzuia. Miguu ya kuku alimfikia na kukutanisha midomo yake na ya yule mtu ambae, hakuonekana kuwa mtaalamu wa kuyakabiri maji.

Walihemeana taratibu kwa lengo la kurejesha pumzi zilizokuwa zinaanza kuwaishia kwa wingi wa maji, kiasi walishindwa kuwa na pumzi.

Baada ya kusaidiana kupeana uhai kwa kugusanisha midomo yao, Zuki Gado p.a.k Miguu ya kuku alianza kufanya harakati za kumnasua mwenzake kwenye mikanda.

Sekunde chache baadae alifanikiwa kumnasua na kuanza kutoka nae nje ya lile gari. Alimweka mgongoni kwake kisha alianza kuyakataka maji kuelekea nchi kavu, huku bastola yake ikiwa imebanwa vema na pindo la nguo yake ya ndani.

Miguu ya kuku alitumia dakika sita pekee hadi kufika nchi kavu, kisha alimlaza chali mtu wake na kuanza kumkanda tumboni ili kumsaidia kuondoa kiasi cha maji alichokuwa amekunywa wakati alipokuwa akijaribu kujiokoa.

Alimkanda hadi alipohakikisha ametapika maji na kuanza kukohoa mfululizo.

“Pole komredi!” Miguu ya kuku alimwambia yule jamaa ambae alikuwa akimshangaa Miguu ya kuku.

“Ahsante kamanda..” Alijibu huku bado akiwa amemkodolea macho.

“Vipi unanishangaa kuwa uchi namna hii?” Miguu ya kuku alimuuliza huku akijitizama na kutabasamu.

“Unajua mtu akitukutuka hapa ufukweni namna hii, anaweza hisi tunawanga eti!” Jamaa alimjibu huku akionesha mashaka yake.

“Kikubwa upo hai hayo mengine ni kama yatatokea…. Vipi unaweza kutembea?” Alimjibu na kumalizia kwa swali.

“Naweza!” Jamaa alisema huku akijiinua chini kwa taabu.

“Kuna tatizo!?” Miguu ya kuku alimuuliza huku akimtazama kwa mashaka.

“Wajinga walifanikiwa kunichapa risasi ya bega” Jamaa alijibu huku akimwonesha bega alilochapwa risasi.

Baada ya kuambiwa hivyo, aliamua kumkokota na kuanza kuelekea ilipokuwa gari yake umbali wa mita mia mbili hivi.

“Vipi kuhusu gari langu!?” Jamaa aliuliza huku akimtazama Miguu ya kuku.

Lile swali lilikuwa ni kama limemkumbusha kitu, alitaka kusita kuendelea mbele lakini alipomtizama mtu aliyekuwa nae, aliamua kuendelea kusonga mbele huku akili yake ikifanya kazi kubwa kuwaza namna ambavyo wangeliweza kuondoa ushahidi wa lile gari.

“Nilifikiria uhai wako kwanza, yaani sikuwaza kabisa kuhusu kupoteza ushahidi aisee!” Alijitetea huku akiongeza kasi ya miguu yake, licha ya kuwa na mtu mgonjwa.

“Kwa hiyo umewaza kuliacha?” Jamaa alihoji.

“Hapana!”

“Utalifanya nini wakati lipo kwenye maji?”

“Ni ngumu kuamua ila inabidi kufanya ninavyofikiria….”Alinyamaza kidogo kisha aliendelea…

“Una uhakika polisi wakilikuta utaweza kuimaliza kesi?”

“Hapana sitaweza! Zimetumika risasi pale na pia kutakuwa na maswali mengi sana ambayo nina hakika sitaweza kuyajibu. Lakini kubwa zaidi ni kuhusu waandishi wa habari, sitaki nifike huko Zuki” Jamaa alijibu kwa kirefu.

“Lina bei gani lile gari?” Miguu ya kuku aliuliza.

“Milioni mia nne hivi.. Lile ni spesho oda”

“Sasa itabidi ulisahau…”

“Kivipi!?”

“Liondoe kwenye hesabu zako kabisa”

“Milioni mia nne kirahisi hivyo!” Jamaa alisema huku akisimama na kumtazama Miguu ya kuku.

“Sasa ni uamuzi wako, gari ilirudi au ahsubuhi uamkie kituo cha polisi kutoa maelezo ya kilichotokea usiku huu” Miguu ya kuku alimuonya.

“Heh!” Jamaa alishangaa.

“Habari ndo hiyo, utatoa maelezo yote kuhusu zile bunduki na watu wake wote, lakini kikubwa ujue wataanza kufuatilia uhalali wa mali zako na wenzako wote…” Miguu ya kuku alizidi kuonya.

“No way, fanya unavyoweza, kwa sasa sitaki kuingia kwenye rada za serikali..” Jamaa alisema kinyonge.

“Good boy… Lazima ukubali kupoteza ili upate kingine ukiwa huru na..” Miguu ya kuku hakumalizia kauli yake baada ya kukatishwa na sauti za ving'ora vya magari ya polisi.

“Jamaa wamefika kabla sijafanya nilichopanga!” Aliongea huku akianza kumkokota mwenzake kuelekea sehemu alipokuwa ameacha gari lake.

“Sina hakika kama nitachomoka safari hii!” Jamaa aliongea kwa kitetemeshi huku dhahiri akionekana kugwaya.

Walikokotana hadi ilipokuwa gari ya Miguu ya kuku. Haraka haraka mlango wa nyuma ulifunguliwa, kisha yule mtu aliyeokolewa alisaidiwa kuingia na kulala kwenye viti vya nyuma.

Baada ya kummweka vema kule nyuma, alizunguka upande wa mbele na kufungua mlango kisha alisakuasakua kidogo na kutoka na saa.

“Zuki tuondoke hapa!” Jamaa aliongea huku akigugumia kwa maumivu na baridi iliyokuwa imejenga kibanda na mwili wake.

“Ile gari itageuka kuwa mwiba utakaotuchoma wote. Na unajua sitaki kuingia kwenye msafara wa polisi na kufungiwa tela.” Miguu ya kuku alisema huku akifungua mfuniko wa saa aliyokuwa ameshika mkononi.

“Utafanya nini ikiwa bado ipo ndani ya maji na polisi wameshafika!?”

“Ni bora nife, lakini nisiingie matatizo na serikali. Sitaki kabisa kuwa mfungwa na sitaki kuua polisi wa nchi yangu. Kifupi sitaki kugeuka mkimbizi ndani ya nchi yangu na ndiyo sababu sijawahi kupokea tenda ya kumuua kiongozi wa nchi yangu hata mmoja na haitakaa itokee!”

“Kwa hiyo unaenda kuifanyaje!?”

“Naenda kuilipua!”

“Heh! Si iko ndani ya maji!!”

“Bomu halichagui sehemu ya kulipukia…”

“Bomu lenyewe unalo!?”

“Unaona hii saa? Hii inaweza kulilipua jengo lenye urefu wowote na kuacha madhara makubwa tu, sasa jiulize hilo gari litapasuka vipi”

“Aisee! Kweli wewe ni Miguu ya kuku”

“Kama unajua naitwa hivyo, basi ondoa shaka kuhusu mimi… Ila ukiona nachelewa sana kurejea, jitahidi uwezavyo uondoke na hili gari na kama ukiona hatari inazidi kuwa kubwa na hutataka kukamatwa, chini ya kila kiti ndani ya hili gari kuna kitufe cha kuilipua gari….”

“Ina maana unaongelea kujiua!?”

“Ndiyo! Jiue ili uwe salama, au kamatwa uteswe na usipofanya hayo yote, watakuzika wakavyo”
Miguu ya kuku aliongea huku akiondoka na saa yake kuelekea kule ambako kulikuwa na gari la yule mtu ambae alienda kumsaidia.

Licha ya kuwa na maofisa wengi wa jeshi la polisi, lakini yeye alitaka kuelekea huko huko kuharibu ushahidi. Alitaka kwenda kulilipua gari lililokuwa ndani ya maji.

Alitalilipua vipi, hilo alijua yeye.
.
.
.
.
.
ENDELEA KUWA NAMI.
 
RIWAYA; CHELEWA UZIKWE.

NA; BAHATI K MWAMBA.

SIMU; 0758573660/0624155629.

SEHEMU YA PILI...


Risasi zilikuwa zinatoka kwenye bunduki kubwa na za kisasa, bunduki ambazo hazikuwa zikipatikana hapa nchini na hata kama zilikuwepo, si rahisi kuingia mikononi mwa walugaluga.
“Automatic Riffleman!?” Alishangaa na kujiuliza bila majibu, lakini hakuwahi kutilia shaka uwezo wa masikio yake na utambuzi wa silaha.

“Huu ni mziki ambao unavuka kina!” Alijisemea huku akijaribu kuwaza njia mbadala ili kutokuingia kwenye mapambano ya risasi na watu wale, ambao walionekana kutumia silaha za kisasa zaidi na kwamwe isingelikuwa busara kutupiana risasi.

Alitazama kushoto kwake na kuiona barabara, kulia kwake kukiwa na kingo za maji. Alipotizama mbele aliona gari za wale watu ambao walikuwa bado wanarusha risasi.

Akawaza kufanya jambo!

Haraka na kwa kasi kubwa, alikimbia kuelekea upande wa barabara. Alipofika barabarani alipiga risasi mbili hewani, kisha kwa kasi ile ile aliondoka kuelekea ukingoni mwa bahari na kuachia risasi nyingine mbili.

Alikuwa anacheza patapotea na hisia za watu ambao hakujua walivyojiandaa kuzikabili changamoto. Lengo la mchezo alioufanya ni kuwafanya jamaa waondoke pale na kuacha kushambulia. Alifanya vile ili kuwachanganya na wasijue aliyerusha risasi ni mlinzi wa makuti pub iliyokuwa pale ufukweni, ama ni maofisa wa jeshi la polisi ambao waliamua kujihami, huku wakiwa wanasogea kuwakabili.

Licha ya kucheza mchezo huo ambo ni sawa na mchezo wa kubeti bila kujua matokeo, lakini hakuacha kuendelea kukimbia kuelekea hukohuko walipokuwa adui zake.

Asingeliweza kusubiri matokeo ya alichokifanya, huku akiwa anazidi kupoteza dakika za kumwokoa mtu aliyekuwa amempigia simu.
Kasi yake ilikuwa haipimiki, huku akihema kila baada ya hatua tano. Bastola yake ilikuwa tayari kwa lolote, macho yake yalikuwa sambamba na zile gari za wale watu ambao walikuwa wameacha kushambulia na hakujua walikuwa wameamua kuchukua hatua gani, baada ya kusikia risasi alizorusha.

Akiwa amebakiza mita kadhaa ili afike zilipokuwa gari za wavamizi, masikio yake yaliweza kusikia sauti za miungurumo ya injini za gari, kisha macho yake yaliona taa zikiwashwa na magari kuondolewa kwa kasi kubwa pale ufukweni.

“Oops!!” Alipumua kwa ahueni baada ya zile gari kuondoka na risasi kukoma. Alipumua kwa sababu alijihakikishia kufanya uokozi bila kashikashi yoyote ile. Pia alijihakikishia usalama kwa asilimia zote, licha ya kwamba alikuwa tayari kwa mapambano ya aina yoyote na wale wavamizi.

Miguu ya kuku alichomoa simu kwenye pindo la boksa yake na kutazama umbali ambao alibakiza, kuweza kumfikia mhusika wake.

Kulikuwa na mita kumi tu kutoka nchi kavu. Huo ndiyo umbali ambao ulibaki ili aweze kumfikia. Lakini ili aweze kuzimaliza hizo mita kumi, ilihitaji ajitose kwenye maji na kuanza uokozi.

Miguu ya kuku alikuwa anaweza kuogelea umbali mrefu bila kupumzika, hivyo umbali ambao alitakiwa kufanya uokozi haukuwa kigezo cha kuweza kumzuia kutumbukia ndani ya maji.

Aliitazama simu yake, kisha aliitupia ndani ya maji na hakuwa akiihitaji tena.

Kwa nini?

Kwa sababu alihitaji kuzama majini na asingeliweza kuiacha nchi kavu ili aipitie baadae. Aliona anaweza kuiacha na ikaokotwa na maafisa usalama ambao wangeliweza kumletea matatizo ambayo hakuwa anayahitaji.

Alipohakikisha simu imepotelea chini ya maji na isingeliweza kupatikana kirahisi, nae aliamua kujitosa majini na kuanza kuyakata maji kuelekea sehemu ambayo alikadiria kungelikuwa na gari la yule mtu aliyekuwa amempigia simu.

Alitumia dakika mbili hadi alipoweza kuliona lile gari, ambalo lilikuwa linazama na kuibuka mithili ya kiboko anaekimbiza mtumbwi.

Baada ya kuliona, alizama majini na kuogelea mithili ya Papa hadi alipolifikia gari ambalo bado lilikuwa linazama na kuibuka taratibu sana. Aliligusa hapa na pale na kisha alitoa bastola yake na kulenga loki ya mlango, kisha aliachia risasi moja na mlango ukaachia na kufanya maji yaingie kwa kasi ndani ya gari.

Haraka aliingia na kukutana na mtu ambae alikuwa anahangaika kujitoa kwenye mikanda iliyokuwa imemzuia. Miguu ya kuku alimfikia na kukutanisha midomo yake na ya yule mtu ambae, hakuonekana kuwa mtaalamu wa kuyakabiri maji.

Walihemeana taratibu kwa lengo la kurejesha pumzi zilizokuwa zinaanza kuwaishia kwa wingi wa maji, kiasi walishindwa kuwa na pumzi.

Baada ya kusaidiana kupeana uhai kwa kugusanisha midomo yao, Zuki Gado p.a.k Miguu ya kuku alianza kufanya harakati za kumnasua mwenzake kwenye mikanda.

Sekunde chache baadae alifanikiwa kumnasua na kuanza kutoka nae nje ya lile gari. Alimweka mgongoni kwake kisha alianza kuyakataka maji kuelekea nchi kavu, huku bastola yake ikiwa imebanwa vema na pindo la nguo yake ya ndani.

Miguu ya kuku alitumia dakika sita pekee hadi kufika nchi kavu, kisha alimlaza chali mtu wake na kuanza kumkanda tumboni ili kumsaidia kuondoa kiasi cha maji alichokuwa amekunywa wakati alipokuwa akijaribu kujiokoa.

Alimkanda hadi alipohakikisha ametapika maji na kuanza kukohoa mfululizo.

“Pole komredi!” Miguu ya kuku alimwambia yule jamaa ambae alikuwa akimshangaa Miguu ya kuku.

“Ahsante kamanda..” Alijibu huku bado akiwa amemkodolea macho.

“Vipi unanishangaa kuwa uchi namna hii?” Miguu ya kuku alimuuliza huku akijitizama na kutabasamu.

“Unajua mtu akitukutuka hapa ufukweni namna hii, anaweza hisi tunawanga eti!” Jamaa alimjibu huku akionesha mashaka yake.

“Kikubwa upo hai hayo mengine ni kama yatatokea…. Vipi unaweza kutembea?” Alimjibu na kumalizia kwa swali.

“Naweza!” Jamaa alisema huku akijiinua chini kwa taabu.

“Kuna tatizo!?” Miguu ya kuku alimuuliza huku akimtazama kwa mashaka.

“Wajinga walifanikiwa kunichapa risasi ya bega” Jamaa alijibu huku akimwonesha bega alilochapwa risasi.

Baada ya kuambiwa hivyo, aliamua kumkokota na kuanza kuelekea ilipokuwa gari yake umbali wa mita mia mbili hivi.

“Vipi kuhusu gari langu!?” Jamaa aliuliza huku akimtazama Miguu ya kuku.

Lile swali lilikuwa ni kama limemkumbusha kitu, alitaka kusita kuendelea mbele lakini alipomtizama mtu aliyekuwa nae, aliamua kuendelea kusonga mbele huku akili yake ikifanya kazi kubwa kuwaza namna ambavyo wangeliweza kuondoa ushahidi wa lile gari.

“Nilifikiria uhai wako kwanza, yaani sikuwaza kabisa kuhusu kupoteza ushahidi aisee!” Alijitetea huku akiongeza kasi ya miguu yake, licha ya kuwa na mtu mgonjwa.

“Kwa hiyo umewaza kuliacha?” Jamaa alihoji.

“Hapana!”

“Utalifanya nini wakati lipo kwenye maji?”

“Ni ngumu kuamua ila inabidi kufanya ninavyofikiria….”Alinyamaza kidogo kisha aliendelea…

“Una uhakika polisi wakilikuta utaweza kuimaliza kesi?”

“Hapana sitaweza! Zimetumika risasi pale na pia kutakuwa na maswali mengi sana ambayo nina hakika sitaweza kuyajibu. Lakini kubwa zaidi ni kuhusu waandishi wa habari, sitaki nifike huko Zuki” Jamaa alijibu kwa kirefu.

“Lina bei gani lile gari?” Miguu ya kuku aliuliza.

“Milioni mia nne hivi.. Lile ni spesho oda”

“Sasa itabidi ulisahau…”

“Kivipi!?”

“Liondoe kwenye hesabu zako kabisa”

“Milioni mia nne kirahisi hivyo!” Jamaa alisema huku akisimama na kumtazama Miguu ya kuku.

“Sasa ni uamuzi wako, gari ilirudi au ahsubuhi uamkie kituo cha polisi kutoa maelezo ya kilichotokea usiku huu” Miguu ya kuku alimuonya.

“Heh!” Jamaa alishangaa.

“Habari ndo hiyo, utatoa maelezo yote kuhusu zile bunduki na watu wake wote, lakini kikubwa ujue wataanza kufuatilia uhalali wa mali zako na wenzako wote…” Miguu ya kuku alizidi kuonya.

“No way, fanya unavyoweza, kwa sasa sitaki kuingia kwenye rada za serikali..” Jamaa alisema kinyonge.

“Good boy… Lazima ukubali kupoteza ili upate kingine ukiwa huru na..” Miguu ya kuku hakumalizia kauli yake baada ya kukatishwa na sauti za ving'ora vya magari ya polisi.

“Jamaa wamefika kabla sijafanya nilichopanga!” Aliongea huku akianza kumkokota mwenzake kuelekea sehemu alipokuwa ameacha gari lake.

“Sina hakika kama nitachomoka safari hii!” Jamaa aliongea kwa kitetemeshi huku dhahiri akionekana kugwaya.

Walikokotana hadi ilipokuwa gari ya Miguu ya kuku. Haraka haraka mlango wa nyuma ulifunguliwa, kisha yule mtu aliyeokolewa alisaidiwa kuingia na kulala kwenye viti vya nyuma.

Baada ya kummweka vema kule nyuma, alizunguka upande wa mbele na kufungua mlango kisha alisakuasakua kidogo na kutoka na saa.

“Zuki tuondoke hapa!” Jamaa aliongea huku akigugumia kwa maumivu na baridi iliyokuwa imejenga kibanda na mwili wake.

“Ile gari itageuka kuwa mwiba utakaotuchoma wote. Na unajua sitaki kuingia kwenye msafara wa polisi na kufungiwa tela.” Miguu ya kuku alisema huku akifungua mfuniko wa saa aliyokuwa ameshika mkononi.

“Utafanya nini ikiwa bado ipo ndani ya maji na polisi wameshafika!?”

“Ni bora nife, lakini nisiingie matatizo na serikali. Sitaki kabisa kuwa mfungwa na sitaki kuua polisi wa nchi yangu. Kifupi sitaki kugeuka mkimbizi ndani ya nchi yangu na ndiyo sababu sijawahi kupokea tenda ya kumuua kiongozi wa nchi yangu hata mmoja na haitakaa itokee!”

“Kwa hiyo unaenda kuifanyaje!?”

“Naenda kuilipua!”

“Heh! Si iko ndani ya maji!!”

“Bomu halichagui sehemu ya kulipukia…”

“Bomu lenyewe unalo!?”

“Unaona hii saa? Hii inaweza kulilipua jengo lenye urefu wowote na kuacha madhara makubwa tu, sasa jiulize hilo gari litapasuka vipi”

“Aisee! Kweli wewe ni Miguu ya kuku”

“Kama unajua naitwa hivyo, basi ondoa shaka kuhusu mimi… Ila ukiona nachelewa sana kurejea, jitahidi uwezavyo uondoke na hili gari na kama ukiona hatari inazidi kuwa kubwa na hutataka kukamatwa, chini ya kila kiti ndani ya hili gari kuna kitufe cha kuilipua gari….”

“Ina maana unaongelea kujiua!?”

“Ndiyo! Jiue ili uwe salama, au kamatwa uteswe na usipofanya hayo yote, watakuzika wakavyo”
Miguu ya kuku aliongea huku akiondoka na saa yake kuelekea kule ambako kulikuwa na gari la yule mtu ambae alienda kumsaidia.

Licha ya kuwa na maofisa wengi wa jeshi la polisi, lakini yeye alitaka kuelekea huko huko kuharibu ushahidi. Alitaka kwenda kulilipua gari lililokuwa ndani ya maji.

Alitalilipua vipi, hilo alijua yeye.
.
.
.
.
.
ENDELEA KUWA NAMI.
Asante sana
 
RIWAYA; CHELEWA UZIKWE.

NA; BAHATI K MWAMBA.

SIMU; 0758573660.

SEHEMU YA TATU.


*****

Alikuwa akikimbia kwa kasi kubwa kuelekea ilipokuwa Makuti Pub. Alikimbia huku saa yake akiwa ameibana vema katikati ya kiganja cha mkono wake.

Wakati akikimbia macho yake hayakuacha kutizama upande ambao kulikuwa na magari ya polisi, yakiwa yamewasha taa.
Alikimbia akiwa na lengo la kufanya jambo la kuwachanganya polisi na alitaka kuwachanya kuanzia Makuti Pub.

Dakika chache zilitosha kumfikisha Makuti Pub. Kwa kutumia uzoefu wake, aliweza kuwaona walinzi wakiwa wamesimama umbali fulani wakishangaa kule walipokuwa maofisa wa jeshi la polisi.

Kwake ilikuwa ni nafasi aliyoihitaji. Haraka aliruka viti vichache vilivyokuwa vimepangwa kwa mpangilio na kwenda hadi lilipokuwa jukwaa la Pub ile ya wazi.

Pembeni ya jukwaa kulikuwa na spika kubwa zilizokuwa zimeunganishwa na kubebeshwa kwa mpangilio maalumu.

Alitoa saa yake na kuigeuza, kisha aliifungua na kubaki akitizama utumbo wa saa ambao ulikuwa umebeba betri tatu zenye ukubwa sawa. Alichukua betri moja na kuibandua karatasi laini iliyokuwa imehifadhi kitu alichokihitaji.

Alipohakikisha karatasi ile imetoka vema, alichukua betri ile na kuibandika kwenye sehemu ambayo kulikutana nyaya nyingi zilizokuwa na kazi mbalimbali kwenye spika.

Alipohakikisha kila kitu kimekaa vile alivyotaka, aliondoka haraka kwenye lile eneo na kurejea ufukweni kupitia njia aliyokuwa ameingilia.

Betri aliyoiacha ilikuwa ni bomu endapo karatasi iliyokuwa imezungushiwa juu, ingelitolewa na bomu lile lingeweza kulipuka baada ya dakika moja na sekunde thelathini pekee.

Alipotoka ndani ya Makuti Pub, alianza kukimbia kuelekea kule kulikokuwa na gari nyingi za polisi, huku akianza kusikia sauti za maofisa wakifanya mawasiliano ya hapa na pale na makao makuu yao.

Hakuzijali sauti hizo, badala yake alizidi kuwasogelea huku akingoja matokeo ya kile alichokuwa amekifanya sekunde chache zilizopita.

‘Booom!!’ Kishindo kizito kilisikika kutokea Makuti Pub.
Kishindo kile kilitetemesha eneo kubwa na kuwaacha wakazi wa maeneo jirani wakijiuliza bila majibu.

Maofisa wa jeshi la polisi walijua kuna tukio lilikuwa linaendelea upande huo, haraka walipanda kwenye magari yao na kuelekea huko.

Waliingia kwenye mtego uliokusudiwa bila kutarajia.

Kuondoka kwao kulimpa nafasi Miguu ya kuku ambae nae hakuhitaji kuichezea nafasi ile.

Haraka alijitosa majini na kuanza kuogelea kwa kasi kubwa na dakika moja baadae, alikuwa amelifikia gari lililokuwa linazama na kuibuka bila mpangilio maalumu.

Alitoa zile betri mbili zilizokuwa zimesalia na kuzipachika ndani ya kile gari kisha alianza kuogelea kujiondoa lile eneo, huku akitarajia ndani ya muda mfupi, karatasi laini zitakuwa zimelowana na kulipa nafasi bomu kulipuka.

Aliogelea kwa kasi akiwa na nia ya kuwawahi maafisa wa jeshi la polisi, ambao hakuwa anajua watarejea wakati gani.

Dakika moja ilitosha kumuondoa ndani ya maji, kisha alianza kukimbia kurejea alikokuwa ameacha gari lake.

Kama alivyotarajia, ndivyo ilivyotokea; mlipuko mkubwa ulitokea baharini na kiyafanya maji yatengeneze wimbi kubwa lilosambaa sehemu kubwa ya bahari.

“Done!” Alijisemea huku akifungua mlango wa gari lake.

Baada ya kufungua mlango na kukaa kwenye kiti, yule jamaa aliyekuwa amelala viti vya nyuma alikurupuka kwa woga.

“Nani!!” Aliuliza kwa wahka.

“Usitie shaka, kila kitu kimefanyika ilivyotakiwa.” Alimjibu huku akizungusha ufunguo wa gari.

“Una hakika hakuna watakachoambulia?” Jamaa aliuliza kwa wasiwasi.

“Kitu pekee watakachotegemea kuona ni kibati cha namba za gari, lakini gari lako halikuwa na kibandiko hicho. Pia wanaweza kutafuta sehemu ya kubandika stika za magari, lakini gari lako lilikuwa na usajili maalumu kutoka mamlaka ya mapato na halikuhitaji stika ili kuwa barabarani. Gari lako wataambulia injini mbovu tu, lakini sasa hivi limeshakuwa vipande vipande.” Miguu ya kuku alimwambia.

“Mh!” Jamaa aliishia kuguna na kujilaza kwenye kiti, huku akisikia tairi za gari zinavyolalama kwenye lami.

“Kitu kikubwa kwa sasa ni kuomba tusisimamishwe na askari yeyote maana, niko uchi na wewe umejeruhiwa.” Miguu ya kuku alisema huku akiwa makini barabarani.

“Wanaweza kuhisi unaroga” Jamaa aliongea kwa masihara.

“Na nilivyo mwembamba, watajua natoka kuvunja nazi njia panda!” Miguu ya kuku alisema huku akiangua kicheko kidogo.

****

Gari iliingizwa kwenye maegesho yaliyokuwa yamesheheni gari zaidi ya ishirini, kisha ikazimwa na kufuatia utulivu wa sekunde kadhaa na mlango wa upande wa dereva ukafunguliwa.

Miguu ya kuku alitoka na kufungua mlango upande wa nyuma na kumtoa jamaa aliyekuwa na jeraha la risasi.

Walikokotana na kuelekea ndani.

“Nimeanza kuhisi baridi sasa!”Miguu ya kuku alisema huku akimketisha mwenzake sofani na yeye kuelekea chumbani kwake.
Huko aliingia bafuni na kuoga, kisha alichukua nguo na kuzivaa na kuchukua simu nyingine na kuiweka mfukoni.

Alitoka nje ya chumba chake na kuelekea sebuleni alipokuwa amemwacha mwenzake.

“Nahitaji kukufanyia tiba kidogo!” Alimwambia na kumuinua.

“Unaweza kunihudumia!?” Jamaa aliuliza huku akisimama.

“Kuna jamaa huwa namtumia kunitibu, atafika hapa muda si mrefu” Miguu ya kuku alijibu huku akifungua mlango wa chumba kingine, ambacho kilikuwa na vifaa tiba vya kila aina.

Walipoingia ndani, alifunga mlango na kumsaidia kumlaza kwenye kitanda kilichokuwa pale ndani.

“Atafika hapa muda mfupi tu kuanzia sasa” Alisema huku akitoka ndani ya kile chumba.

Dakika kumi baadae, alirejea akiwa ameongozana na jamaa mmoja mrefu, akiwa amevalia miwani usoni mwake.

“Kutana na George Dau, ila hupenda kujiita Alfa na, mimi huwa napenda kumuita Boy'one.” Miguu ya kuku alimtambulisha jamaa aliyeingia nae, huku akimwoneshea jamaa aliyekuwa amelala chali akiwatizama.

“Alfa, huyu ni Dokta Masu, ni msiri wangu na tabibu wangu binafsi. Usiwe na wasiwasi anakifua na hatoweza kusema popote, atakuhudumia na utapona kabisa” Alifanya utambulisho kwa mtu aliyekuwa ameongozana nae.

“Nashukuru kukufahamu Dokta!” Alfa aliongea kivivu.

“Namimi nafurahi kukufahamu” Dokta nae alisema huku akivua begi lililokuwa mgongoni mwake.

“ Nadhani uendelee na huduma ngoja ni….” Miguu ya kuku alikatishwa na mlio fulani kwenye simu yake.

Haraka aliitoa simu yake mfukoni na kuitizama.

“Shiiit!” Alisema kwa wahka huku akiirejesha simu mfukoni na kuwatizama wenzake, ambao na wao walikuwa wanamtizama kwa wasiwasi.

“Nyumba yangu ya Tegeta imeingiliwa!” Alisema.

“Whaat!” Alfa alimaka huku akijizoazoa kitandani.

“Yes! Imeingiliwa na inanibidi niondoke hapa…. Dokta hakikisha Alfa anakuwa salama kiulinzi na kimatibabu.” Alisema huku akifungua mlango na kutoka nje, bila kungoja majibu ya Dokta Masu.

Alipofika nje ya nyumba, alielekea yalipokuwa maegesho ya pikipiki zake. Alidandia pikipiki moja, huku akiwa anaificha bastola yake kiunoni, kisha alipiga kiki na kuondoka kwa mwendo wa wastani.

Aliongeza mwendo alipofika nje ya uzio wa nyumba yake.

Barabarani mwendo wake haukuwa wa kawaida, alikimbiza pikipiki mithili ya washindanaji kwenye mbio za pikipiki. Hakujali kona kali, wala hakujali alama za barabarani.

Dakika thelathini na tano zilitosha kumfikisha hadi Tegeta kwa ndevu. Alisimamisha pikipiki yake na kuigesha kweny e kituo cha abiria, kisha alifuata njia iliyokuwa inapita sokoni.

Alitembea kihahehahe, nusu atembee na nusu akimbia, huku akiwa amekaza fizi zake kwa uchungu na hasira.

Maisha yake yote, hakuwa akipenda kuingiliwa ndani ya himaya yake, labda uingie kwa heri lakini kwa shari, ilikuwa ni kujitakia matatizo yasiyo na kikomo. Angelikuwinda usiku na mchana hadi ahakikishe hakuna kilichosalia kwako na kisha anakumaliza kimya kimya.

Mwendo wake ulimfanya awahi kufika nyumbani kwake, lakini macho yaliwahi zaidi kuliko mwili.

Macho yake yalishuhudia kile ambacho hakuwa amekifikiria, mwili ukamtetema, moyo ukamuuma.
Alijikuta akienda chini bila kupenda huku mikono ikiwa kichwani.
Nguvu zilimwishia!

Wakati yeye akiwa amepiga magoti chini na kuweka mikono kichwania mithili ya mateka, pembeni yake mita kadhaa kulikuwa na mtu aliyevaa nguo nyeusi na kujifunika barakoa na kubakiza macho yake tu. Mtu yule alikuwa na bunduki ya kudungulia.

Alimlenga huku akitabasamu kifedhuli.

Miguu ya kuku alikuwa kwenye rada za muuaji hatari, aliyesafiri kilomita nyingi kuja kulipiza kisasi kwa yale yaliyowahi kumkuta kwa sababu ya Miguu ya kuku.

Miguu ya kuku nae hakuwa akijua yupo matatizoni, akili yake yote iliishia kwenye nyumba yake..

Hakika ulibaki kuwa mtihani usio na majibu rahisi.
 
Bro Kudo ukishusha kitu kipya uwe una tutag mashabiki zako, me ndio naona leo hivi vitu aisee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom