Cheka aingia orodha ya mabondia bora IBF

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
Imani Makongoro
BINGWA wa ngumi za kulipwa, Francis ‘SMG’ Cheka ameingia katika orodha ya mabondia bora 15 duniani wanaotambuliwa na Chama cha Masumbwi cha IBF.

Cheka bingwa wa taji hilo Afrika ameingia kwenye orodha hiyo kufuatia viwango vya ubora vya dunia vya IBF vilivyotolewa hivi karibuni.

Kwa viwango hivyo, bingwa huyo wa Afrika wa uzani wa super middle ana nafasi ya kuwania Ubingwa wa Dunia wa IBF dhidi ya mabingwa kutoka nchi mbalimbali ulimwenguni.

Kwa mujibu wa Rais wa Chama cha Ndondi cha PST, Emmanuel Mlundwa, Cheka anaweza kuwania taji hilo dhidi ya Benjamin Simon na Henry Weberwa wa Ujerumani.

"Mabondia wengine wanaoweza kucheza na Cheka kuwania ubingwa huo ni Maxim Vlasov wa Russia, Marco Periban wa Mexico na Ezequiel Maderna wa Argentina," alitaja Mlundwa.

Wengine ni Paul Smith wa United Kingdom, Junior Talipeau na Serge Yannick (Australia), Nikola Sjekloca na Alexander Johnson (United States), Roman Shkarupa (United Kingdom), Luis Garcia (Ireland), Rudy Markussen (Denmark) na Fulgencio Zuniga wa Colombia.

GAZETI MWANANCHI


 
Back
Top Bottom