PreGE2025 CHAUMMA wanashambulia CHADEMA badala ya CCM imekuwaje tena?

PreGE2025 CHAUMMA wanashambulia CHADEMA badala ya CCM imekuwaje tena?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Master Legendary

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
579
Reaction score
887
Nimewasikiliza hawa jamaa naona kama kuna kuchanganyikiwa flani hivi au wana hasira za kutoka CHADEMA kiasi cha kupoteza Dira na kutumia Mikutano yao waliyoiandaa kwa Gharama kubwa kuisakama CHADEMA badala ya CCM, siyo kwamba wanarudia kosa walilofanya ACT?

Lengo la Chama chochote cha Siasa ni kushika Dola inakuwaje sasa wao wanaishambulia CHADEMA ambayo haina Dola na kuacha Chama kilichoshika Dola?Hii si itathibitisha sasa kwamba wanafanya kazi ya Bosi?

Nimemsikiliza Salum Mwalimu analalamika anadai hela zake CHADEMA, yeye si alikuwa Kiongozi Mkubwa tu alipotoka na walisema Sekretariet yote wanaingia CHAUMMA sasa kama hawakuwajibika kiasi cha watu kutolipwa katika kipindi chao wanamlaumu nani?

Analia sana CHADEMA waingie kwenye Uchaguzi, kama yeye anaona Mazingira ni rafiki na atashinda kwanini asinadi sera zake akaingia ulingoni kuliko kulazimisha wanaoona mazingira hayaruhusu waingie.

Anyway hoja kubwa ni ndani ya muda huu mfupi ni wapi zimepatikana Fedha nyingi hivi za kufadhili Mikutano ya CHAUMMA kwa kujenga Majukwaa ya Gharama, Misafara ya Magari, helikopta,Pikipiki nk.

Kuna mtu anaona ninachoona hapa?Au niendelee tu na mtori?
 
CHAUMMA ni poor investment ya CCM.

Wameenda kuokota makapi wakidhani ni vichwa kumbe uoza mtupu🤣🤣🤣🤣🤣.

Anaaecheka kizungu kwa sasa ni Mzee wa Ubwabwa. Kapata ruzuku yake uzeeni kabisa🤣.
 
Mwana siasa aliyekomaa huuza sera siyo kushambulia alikotoka Bagonza alisema ubaya wa mlikotoka tunaufahamu kwa sasa tuambieni uzuri wa mlikohamia. Hawa jamaa hawana political strategy. Mna sera ya ubwabwa ifafanueni vizuri iwe brand!
 
Chauma kimetengenezwa hiyo ikowazi na inafahamika wazi...
Viongozi waandamizi wakezao walikuwamo katika wabunge wa COVID.
 
Pakiendelea kunyesha hivi ndipo tunaona vyema panapovuja.

Au nasema uongo ndugu zangu?

Namnukuu Benson Kigaila siku ile ya kuwapokea sijui wanachama 3,000. Alisema, ^Leo ni mwisho kabisa wa sisi kuwazungumzia Sidiemu!^
 
Back
Top Bottom