Chanzo cha sikukuu ya Valentini

Chanzo cha sikukuu ya Valentini

Ruach

Member
Joined
Jun 8, 2013
Posts
31
Reaction score
15
Siku ya valentine ni kila mwezi wa pili ambapo watu hudhihirisha mvuto na haiba za mapenzi kwa kila mmoja kwa kupeana kadi na zawadi.

Sherehe hii chanzo chake ni mambo ya dini za kirumi.

Lupercalia ni sherehe iliyoadhimishwa na Warumi wa zamani kila mwezi wa pili tarehe kumi na tano. Lengo lake ilikuwa kuwaheshimu miungu Lupercus na Faunus na ndugu mapacha wawili ambao ni Romulus na Remus ambao huaminiwa kuwa waanzilishi wa mji wa Rumi.

Sherehe za Lupercalia zilifanyika juu ya kilima kiitwacho Palatine ambapo warumi wa zamani walijenga nyumba zao.

Makuhani wa miungu lupercus walivaa mavazi ya ngozi ya mbumzi. Baada ya kutoa kafara ya mbuzi na mbwa, walijipaka damu ya mbuzi na mbwa kwenye miili yao, walikimbia kuzunguka kilima wakiwa wamebeba usinga wa ngozi ya mbuzi ulioitwa Februa(kifaa cha utakaso).

Wanawake wa Kirumi walisimama kando ya Kilima cha Palatine ili wale makuhani waweze kuwapiga na ule usinga/ februa wakiamini kwamba tendo hilo litawasaidia kuwa na uzao mwingi na wepesi wakati wa kujifungua.

Pia sherehe hii ilihusiana na vijana wa kiume na wa kike kuchagua mpenzi. Makuhani waliweka majina ya wasichana kwenye boksi na kila mvulana alichukua karatasi ya jina la msichana kwenye boksi na msichana huyo atakuwa mchumba wake mpaka sikukuu nyingine ya Lupercalia.

Mwaka 270 A.D, Sikukuu ya Lupercalia iligeuzwa na kuwa sikuu inayoitwa ya kikristo Kumuheshimu mtakatifu Valentini aliyeuwawa karne ya tatu

Kuna hadidhi nyingi kuhusu Valentini.
Kuna hadidhi inayosema valentini alikuwa mkristu aliyekuwa rafiki ya watoto wengi, warumi wakamfunga kwa sababu ya kukataa kutambikia miungu yao. Watoto wakapeleka kadi zenye maneno ya upendo na kupachika kwenye Vizingiti vya dirisha la chumba cha gereza alimokuwamo Valentini.

Hadithi nyingine inasema Valentini alimponya binti wa mfungwa mwenzake na baadae huyo binti kuangukia kwenye penzi la Valentini.

Inaaminiwa kuwa valentini aliuwawa Februari 14 mwaka 269 A.D.
Mwaka 496A.D Papa aliamuru Februari 14 kuwa sikukuu ya valentini. Ikawa ianasheherekewa na kanisa kama mbadala wa sikukuu za kipagani.

Chanzo: Kitabu cha GLOBAL HISTORY AND GEOGRAPHY, the grouth of ccivilizations kilichoandikwa na HENRY BRUN, LILLIAN FORMAN na HERBERT BRODSKY


Yehoshua Hamochiah
 
Tutaiga mpaka imani za freemason kwa kutojitambua.
 
Ni kweli Ruach nakuunga mkono katika hilo na ndio maana kwangu mimi binafsi siku hiyo huwa hainichukulii muda kabisa nachoamini mimi ni upendo unapaswa kuwepo masaa 24 siku saba za wiki miezi kumi na mbili ya mwaka yaani sikuzote na sio one special day its meanignless to show love periodocally because love is suppose to be TIMELESS.
 
Last edited by a moderator:
sometime tunageuza sheria za Mungu kwa kutenda mambo yetu wenyewe na kuziacha njia za haki. ni kweli hii sikukuu ipo kwa faida za kishetani na sio za Ki Mungu na ndio maana siku hii inaongoza kwa uzinzi kwa kisingizio cha kuonyeshana mapenzi. Na hata jina la sikukuu limekaa vibaya, ni jina la mtu. kwanini isiitwe LOVER'S DAY? ikaitwa valentine day
 
Mcha Mungu wa kweli hawezi kusheherekea sikukuu hii maana chanzo chake ni miungu na mizimu ya kizungu.

Mungu atusaidie ili wengi wawe na ufahamu.

Warumi12:2-Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Yehoshua Hamochiah
 
Romans 13:8 Owe no man any thing, but to love one another: for he that loveth another hath fulfilled the law.

Happy valentines day mmu!
 
Back
Top Bottom