Changia Mawazo kuboresha mchango wangu bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu!

Ulipooomba kuchangia hukujua unataka kuzungumzia nini?jipange Mh. yako mengi sana sio lazima tukuambie chakuzungumza japo hapa ndo GT,
Kuna General Tyre imekufa je ni viwanda vingapi vilivyo kufa na kwanini?
Kwanini gharama za cmu zipandishwe ilhali hata baadhi ya sehemu za nzega hakuna mawasiliano wala umeme.
 
Mkuu! Ebwanaeee! Bahati mbaya kwenye simu hakuna kile cha kubofya like. Yaani ungekula like 10000000000000000.
 
I only have 10 precious minutes, hivi haya yana tija kweli?

Mkuu Kigwa, yenye tija ni yapi..? C ungeweka reference na bottom line ili tuji-squeeze humo. Anyway, na mi naweka machache:
  1. Sera ya uraia wa mTZ ni mbovu na haimtambui mtanzania hasa ni yupi. Uliwahi mwenyewe kuhisiwa kuwa we ni Mrundi. Ulijitetea sana lkn bado watu wanaamini we si raia. Zitto amewasemea leo bungeni wale wa Kigoma baada ya kuguswa kwenye maslahi yake. Lkn kuna watutsi wenye asili ya Tanzania kihistoria wameteswa kwa miaka mingi kwa kufanywa vitega uchumi na maafisa uhamiaji. Suala la uraia liwe na sera inayoeleweka maana hata vitambulisho vya taifa siyo soln ya hili.
  2. Bodi ya Pamba ivunjwe na kuundwa upya km haiwezekani kumrejesha kazini DG bila masharti na kumpa meno. "Hatuwezi kuendelea kwa kuruhusu akili ndogo zitawale akili kubwa...Mhe. Mch. Msigwa". Huyu alitakiwa kuambiwa rekebisha 1,2,3 halafu songa mbele siyo kaa pembeni. Tuna-politicise kila kitu..?
  3. Kutenganisha Wizara ya Kilimo na Mifugo ni kosa linaloibua vita baina ya wakulima na wafugaji. Lkn pia DALDO na wagani wa kilimo mara nyingi ndo wa mifugo. Serikali ifikirie kurudisha hii Wizara km ilivokuwa.

Eng. Willy
 
Ndg zangu, nataraji kupata fursa ya kuhutubia bungeni kwenye bajeti ya ofisi ya waziri mkuu iliyowasilishwa leo, hapa tutapata fursa ya kusema lolote la kisera na hata la kijimbo, kama mlivyoshuhudia leo wachangiaji wa mwanzo walivyoanza.

Jina langu ni la 34 kwenye orodha ya wachangiaji hivyo nina matumaini makubwa ya kupata nafasi ya kuchangia endapo orodha hii itafuatwa kama ilivyo. Naomba mawazo ya nini unadhani ni nyeti sana na ungependa kisemewe na wabunge?

Nitatoa fursa kwa watu watakaonipa issue nyeti na zenye mantiki na hususan zilizokaa kitaifa zaidi. Kwa wale wa Nzega na hata Tabora kwa ujumla, mnakaribishwa kunipa issue za Kijimbo, kiwilaya ama hata kimkoa ili nizisemee bungeni.

wakatabahu,
HK.
Dk. naona una malengo mazuri kwa taifa lako lakini shida ipo kwenye hilo lichama unalolitumikia kimsingi limepoteza mvuto hata kama utakuja humu kwa nia njema watu wanakuona walewale toka humo kisha tuongee tuna mambo mengi yanatuchefua kila kukicha wakati tunatafakari la madaktari limeibuka hili la bilions mia tatu za uswiss sasa katika hali kama hii sisi tuseme nini wewe nenda na staili ya lusindelism au kombalism sisi tutavumilia tu kwani aka tatu si mingi
 
Pasco wa JF unachoongea ni kweli tupu, nilishamuweka huyu ndugu HK kwenye vitabu vyangu vya kumbukumbu, lakini alinichefuwa nyongo pale alipokataa kusaini Paper ya Zitto Kabwe, lakini tatizo kwangu si yeye kukataa kusaini bali sababu dhaifu alizokuja nazo hapa JF na kuanzisha thread ni kwa nini hakusaini ile paper ya Zitto Kabwe.

Utetezi wa HK ulijaa udhaifu mwingi na kibaya zaidi akajiingiza tena kwenye mtego uleule wa chama changu!! kwa kweli alinisikitisha sana, na ndio maana kwenye mgomo wa kwanza wa madaktari aliwaunga mkono vizuri madaktari wenzake, lakini mwishoni akajidhihirisha kwamba yeye ni nothing but a Coward. anyway bado nampa muda atleast nyakati nazo zitaamuwa zenyewe, still bado ana nafasi ya kutuonesha kama yuko upande wa wananchi au upande wa wakolono weusi.
Mkuu Matola, kiukweli HK aliukwaa ubunge baada ya kuteuliwa kwa hisani!, hivyo naamini moyoni alikuwa na Zitto lakini kimatendo aliogopa kuonekana ni mtu asiye na fadhila au shukrani kwa waliombeba kwenye ile mbeleko ya uteuzi wa CCM!. Kama angejinyamazia tuu kama wabunge wengine wengi walioko CCM, na wameshaichoka CCM kwa mioyo japo bado wako na ile kauli ya "kidumu" tungemwelewa!. Hata ule utetezi wake, ukiusoma in between the line, ulikuwa ni wa kujikosha tuu!. The guilt, always are afraid!. Maadam the end justifies the means, at the end of the day, amejitokeza na kusimama kuhesabiwa, lets just him the benefits of doubt by leaving his questionable past behind, and concentrate on his very promising future ahead in Tanzanian politics!.
 
sioni mantiki ya ccm na wadau hapa kumpigia chapuo huyo msomali wao,,,bashe si mtanzania its ova,BASHE NA RAGE SI WATANZANIA,WAENDE BAIDOA HUKO NA MOGADISHU WAKAENDESHE SIASA,,,,,,
Mkuu Bajabiri, huo ni ubaguzi mbaya kabisa!. Hivi tukiwafukuza na Wahaya warudi kwao chini ya Baganda Kingdom, Wahangaza tuwafukuzie kwao Rwanda, Masai tuwafukuze wakaunganike na ndugu zao wa upe wa pili, so do Wajaluo wakajiunge na Waluo, Wamakonde nao warudi kwao Msumbiji, Wangoni, warudi walikotoka, tangu walipoletwa nchini kwetu na Zongendamba, Wanyasa tuwarudishe kwao Nyasaland, na makabila mengine yote, tuwatimue warudi kule kwenye asili yao, ili Tanganyika wabaki pure breed tuu ya bantustans, jee unajua nani watabaki?!.

Kuna makabila kibao tumewahifadhi tuu kwa hisani ya mipaka ya mkoloni, na baada ya kupata uhuru, kila aliyekuwepo ndani ya ardhi ya Tanganyika tangu ile saa 5:59 ya kuamkia Desemba 9, 1961, alipata uraia wa Tanganyika bure!, sasa wewe ni nani kuanza kuwanyooshea watu vidole kuwa sio Watanzania!.

Wenyewe wenye asili halisi ya Tanganyika wamejinyamazia na kuwakubali wageni kibao!, nyie ambao nanyi ni wageni tuu, ndio kwanza mnaanza kupiga kelele!, tena mna bahati, Nyerere aliwapigania, vinginevyo saa hizi mngekuwa kwenu!.

Tuachane na ubaguzi huu!.
 
Back
Top Bottom