Changamoto ya kuoa/Kupata mke

Kama ni mwamini muombe Mungu wako akukutanishe na mwanamke wa ndoto zako! Usimbane Mungu wako kukuchagulia maana ukishasema unamtaka mwalimu umembana! Mwache akuchagulie anayeona anakufaa na akupe mwanamke aliyemuumba kwa ajili yako, maana najua Yeye anakujua zaidi ya wewe unavyojijua!
 
Asante kwa ushauri mzuri.[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120]
 
Kumbe unataka mwl. Huku wako wengi lakini wamezalishwa kama hujali tupia contact nkuunganishe.

Note: mke akiwa mzima, hana hiv oa tu izo changamoto zingine mbele kwa mbele, ila tabia nyingine hujionyesha mwanzo tu kabla hujamuoa kama mapepe, tamaa, shobo, uchawi, uchoyo
 
Aliyezalishwa hapana.
Sihitaji kuwa mume mdogo pia hata kazini wapo waliozalishwa.
Sitaweza kumudu kuishi na single mother.
Asante kwa ushauri
 
Pole sana Mheshimiwa.
Kipindi ulichonacho ni kigumu na usipokuwa makini utapata bora mke maana unashauku ya kuwa na mke. Mimi naona uanze kuomba Mungu ili aonyeshe njia, Afungue macho na pia akupe wepesi wa kuamka na kuanza kuwa karibu na hao walimu kwa kuwa mke huchaguliwa na sio kutafuta.
 
Asante mkuu
 
Mke mwema anatoka kwa bwana,jipe moyo utampata ambae ni chaguo sahihi kwako
 
Uwe makin cku hiz Kuna wake wa kutengenezwa.
 
Wanawake wa dar watakusumbua sana nenda mikoani ukae hata mwezi utaopoa mke unayemtaka
 
Unafanya uamuzi mzuri na muhimu kwa maisha yako. Kila la kheri mkuu.

Ushauri:
1. Kuwa makini sana kwenye zoezi la uchaguzi. Sio kila king'aacho ni dhahabu.
2. Huna sababu ya kuwa na presha za kuoa. Uko kwenye age inayofaa kuoa lakini kwa miaka hiyo yako bado una muda wa kutosha wa kumtafuta mtu sahihi. Nakuomba usiwe desperate utaumia mbaya. Ukiwa desperate uwezo wako wa kufanya maamuzi unavurugika.
3. Wanawake wana uwezo mkubwa sana wa ku-fake ili ampate mwanaume anayemtaka. Tumia akili kufanya maamuzi.
4. Usifumbie macho baadhi ya vigezo vyako vya msingi in a woman. Ukiona mtarajiwa ana upungufu (tatizo kubwa la kitabia) usikubali ahadi ya kubadilika baada ya ukishamuoa. Mambo hayo yana tendency ya kujirudia at a certain point in time kwa watu wengi na bahati mbaya ni kuwa kama ushamuoa tayari unapoteza power ya kutosha kumbadilisha (hasa km alikupa ahadi ya kubadilika ili usimbwage). At that time hashindwi kukuambia ulinikuta niko hivi....kumbuka anakuwa hana vya kupoteza vingi. Yeah...ashaolewa. Ha ha ha
 

Wenye experience wanasema kama hukupata mke/mme wakati ukiwa bado unasoma chuo, basi jiandae kupata bora mke/mme na sio mke/mme bora. Nina rafiki yangu naye baada kuanza kazi ndio akaanza mchakato wa kutafuta mke japo kampata lakini ilimchukua muda. Tena ni afadhali kwa sisi wanaume tunaweza chelewa sana kuoa, lakini Dada zetu wanapo approach 30's watamkubali yeyote atakayejitokeza.
NB: Hii ni life experience ambayo huwatokea wale ambao toka wameanza shule primary, maisha yote wameunga kusoma mpaka kufikia degree, masters....na wale ambao hawakuweza kuendelea na elimu ya juu huoa/huolewa mapema sana.
 
Hebu rudi kwenye maisha yako huko ulikopitapita mkuu, kuna mmoja wapo atakuwa ni mkeo tu ,ila kwaajili ya maisha ya schule na kuhangaikia kazi labda uliona wa kawaida. . Picha pic miaka mitano ya nyuma ulikuwa na nani. ..na nashauri ukiweka kigezo kuwa mwalimu utakuwa umekosea, Mwenyezi Mungu hapangiwa wa kukupa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…