mtume wawatu
JF-Expert Member
- Oct 30, 2016
- 1,000
- 1,080
Kwanza kabisa, naomba nitangulize shukrani kwa kupata nafasi hii ya kulitumia jukwaa hili kuanzisha mjadala huu. Nimeamua kuanzisha mjadala huu kama sehemu ya namna ya majadiliano ya wana jamii kuhusu masuala yanayotuhusu na pengine michango itakayotolewa iwe na manufaa kwa wanajamii kwa ujumla.
UTANGULIZI
Ulemavu ni hali ya kuwa na mapungufu katika viungo vyako vya mwili au akili hivyo, kukusababisha ushidnwe kutekeleza sulala au jukumu fulani kwa namna sawa na watu wengine. hali hii husababisha mtu mwenye ulemavu kuhitaji msaada ili kukamilisha jambo hilo.
kwanza kabisa, nianze kwa kujitambulisha kwamba mimi pia ni mtu mwenye ulemavu wa kutokuona (blind person) hivyo nina uzoefu wa kiwango fulani wa kuishi na wanajamii na hali yangu ya ulemavu.
Kwa ufahamu wangu mdogo, kuna aina kama 5 za ulemavu ila yawezekana zikawa ni zaidi ya hizi nitakazo ziorodhesha hapa chini.
1. Watu wasioona.
2. Viziwi. (yaani watu wenye changamoto ya kutosikia au kuongea). angalizo hawaitwi watu wasiosikia.
3. Walemavu wa ngozi. (zipo aina nyingi za ulemavu wa ngozi)
4. Walemavu wa viungo.
5. Watu wenye mtindio wa ubongo. (hawa kwenye mada hii ya mahusiano naomba nisiwazungumzie)
.
Kwanini sitawazungumzia? Sababu ili mtu uanzishe mahusiano ni lazima upate ridhaa toka kwa mwezako wa upande wa pili akiwa sawa kiakili. lakini, walemavu wa akili hawakidhi kigezo hiki.
Watu wenye ulemavu tajwa hapo juu ni sehemu ya jamii tunayoishi. lakini kumekuwa na changamoto ya namna gani bora ya kuwa na mahusiano na watu hawa katika jamii.
tafsiri ya mahusiano ninayoomba niitumie hapa ni mahusiano ya kimapenzi. hivyo neno mahusiano litaakuwa likimaanisha hivyo.
MASWALI YA KUONGOZA MJADALA HUU
1. UPI MTAZAMO WAKO JUU YA KUWA NA MAHHUSIANO NA MTU MWENYE ULEMAVU??
2. UNAONA CHANGAMOTO GANI KATIKA MAHUSIANO YA AINA HII?
3. UNAHISI MTAZAMO WA JAMII UKO SAWA JUU YA WATU WENYE ULEMAVU?
4. KAMA KUNA CHANGAMOTO NINI KIREKEBISHWE KULETA MABADILIKO CHANYA?
Toa uzoefu wako kama mwanajamii. Mwisho kabisa naomba kuwashukuru wana MMU kwa kusoma uzi huu.
Naomba kuwasilisha
Unaweza kuona michango ya wadau pia katika uzi huu
Ushauri: Hataki kuolewa na mimi, anaogopa kuchekwa kuolewa na "asiyesikia".
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
UTANGULIZI
Ulemavu ni hali ya kuwa na mapungufu katika viungo vyako vya mwili au akili hivyo, kukusababisha ushidnwe kutekeleza sulala au jukumu fulani kwa namna sawa na watu wengine. hali hii husababisha mtu mwenye ulemavu kuhitaji msaada ili kukamilisha jambo hilo.
kwanza kabisa, nianze kwa kujitambulisha kwamba mimi pia ni mtu mwenye ulemavu wa kutokuona (blind person) hivyo nina uzoefu wa kiwango fulani wa kuishi na wanajamii na hali yangu ya ulemavu.
Kwa ufahamu wangu mdogo, kuna aina kama 5 za ulemavu ila yawezekana zikawa ni zaidi ya hizi nitakazo ziorodhesha hapa chini.
1. Watu wasioona.
2. Viziwi. (yaani watu wenye changamoto ya kutosikia au kuongea). angalizo hawaitwi watu wasiosikia.
3. Walemavu wa ngozi. (zipo aina nyingi za ulemavu wa ngozi)
4. Walemavu wa viungo.
5. Watu wenye mtindio wa ubongo. (hawa kwenye mada hii ya mahusiano naomba nisiwazungumzie)
.
Kwanini sitawazungumzia? Sababu ili mtu uanzishe mahusiano ni lazima upate ridhaa toka kwa mwezako wa upande wa pili akiwa sawa kiakili. lakini, walemavu wa akili hawakidhi kigezo hiki.
Watu wenye ulemavu tajwa hapo juu ni sehemu ya jamii tunayoishi. lakini kumekuwa na changamoto ya namna gani bora ya kuwa na mahusiano na watu hawa katika jamii.
tafsiri ya mahusiano ninayoomba niitumie hapa ni mahusiano ya kimapenzi. hivyo neno mahusiano litaakuwa likimaanisha hivyo.
MASWALI YA KUONGOZA MJADALA HUU
1. UPI MTAZAMO WAKO JUU YA KUWA NA MAHHUSIANO NA MTU MWENYE ULEMAVU??
2. UNAONA CHANGAMOTO GANI KATIKA MAHUSIANO YA AINA HII?
3. UNAHISI MTAZAMO WA JAMII UKO SAWA JUU YA WATU WENYE ULEMAVU?
4. KAMA KUNA CHANGAMOTO NINI KIREKEBISHWE KULETA MABADILIKO CHANYA?
Toa uzoefu wako kama mwanajamii. Mwisho kabisa naomba kuwashukuru wana MMU kwa kusoma uzi huu.
Naomba kuwasilisha
Unaweza kuona michango ya wadau pia katika uzi huu
Ushauri: Hataki kuolewa na mimi, anaogopa kuchekwa kuolewa na "asiyesikia".
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app