Changamoto biashara za misimu

Changamoto biashara za misimu

lugom

Member
Joined
Oct 26, 2024
Posts
29
Reaction score
64
Habarin wanaJF .Mimi ni mtumishi wa umma katika mkoa wa mwanza vijijini nje na ajira nimekuwa nikifanya biashara ya mpunga Kwa kukusanya nakuweka stoo ukipanda bei nakoboa nauza, ambayo ukikusanya mwezi 6 almost unakuja kuuza kwenye mwezi wa 2 next year Kwa sasa mtaji wangu nikama 10M.

Ila changamoto ya hii biashara unatumia nguvu kubwa sana kupata mazao haswa mvua zinapo goma kama mwaka huu kwaiyo unajikuta muda mwingine pesa unazo mfukoni ila changamoto kupata mzigo.kutokana na hizo changamoto mimi nimetageti huku kwenye mazao nitafute mtaji nikafanye biashara ya vifaa vya ujenzi(hardware).

Ila naskia mtaji wake nimkubwa sana.ushauri wenu wadau.Je nianze na huu mtaji wa10M,au nipambane kidogo zifike 20-30M.au ndo mbaka zifike 50M kuendelea na location ya hii biashara inataka mjini zaid au vijijini ?,kwasababu ndoto yangu nikuja kumiliki hardware kubwa sana hapo badae.
 
Habarin wanaJF .Mimi ni mtumishi wa umma katika mkoa wa mwanza vijijini nje na ajira nimekuwa nikifanya biashara ya mpunga Kwa kukusanya nakuweka stoo ukipanda bei nakoboa nauza, ambayo ukikusanya mwezi 6 almost unakuja kuuza kwenye mwezi wa 2 next year Kwa sasa mtaji wangu nikama 10M.

Ila changamoto ya hii biashara unatumia nguvu kubwa sana kupata mazao haswa mvua zinapo goma kama mwaka huu kwaiyo unajikuta muda mwingine pesa unazo mfukoni ila changamoto kupata mzigo.kutokana na hizo changamoto mimi nimetageti huku kwenye mazao nitafute mtaji nikafanye biashara ya vifaa vya ujenzi(hardware).

Ila naskia mtaji wake nimkubwa sana.ushauri wenu wadau.Je nianze na huu mtaji wa10M,au nipambane kidogo zifike 20-30M.au ndo mbaka zifike 50M kuendelea na location ya hii biashara inataka mjini zaid au vijijini ?,kwasababu ndoto yangu nikuja kumiliki hardware kubwa sana hapo badae.
kwanza hongera
kingne subiri waje wajuzi wa mambo
 
Mkuu asikudanganye mtuu mtaji ni mtaji. Kikubwa ni kuanza. Kuna baadhi ya watu wanaanza na mtaji wa milion 2 na wewe unasema unamilion 10.

Unaweza kuanza tuu vizurii mkuu
Kubwa fatilia uanze biashara
Asante sana mkuu.
 
M 10 ni nyingi pia ni chache inategemea kama utaanza kuuza bizaa zenye samani kubwa ila kama utaanza za saman ndogo na utizame hasa kwenye uhitaji wa nyumba za huko mf bomba,koki,ppc na vingine basi huo mtaji ni mrefu sana
 
M 10 ni nyingi pia ni chache inategemea kama utaanza kuuza bizaa zenye samani kubwa ila kama utaanza za saman ndogo na utizame hasa kwenye uhitaji wa nyumba za huko mf bomba,koki,ppc na vingine basi huo mtaji ni mrefu sana
Changamoto ninayo iona hapa nilipo Kuna vihardware vidogo vidogo ambavyo wanauza ivyo vitu vidogo vidogo kama bomba,PVC,vifaa vya umeme,nondo ,misumari, cement na zaidi.sasa nlikuwa na wish niwe tofauti kidogo.
 
Changamoto ninayo iona hapa nilipo Kuna vihardware vidogo vidogo ambavyo wanauza ivyo vitu vidogo vidogo kama bomba,PVC,vifaa vya umeme,nondo ,misumari, cement na zaidi.sasa nlikuwa na wish niwe tofauti kidogo.
Utofauti hauwezi kupatikana kwa kukaa na mtaji mfukoni nenda field kwa mtaji huo huo ila uanze na bidhaa kama hizo wanazouza wao na kuongeza zingine ambazo zitatofautiana na hao

Inawezekana hizo bidhaa wanazouza hao wengine ndizo zinauzika kwa wingi kwenye hayo maeneo kulingana na mahitaji ya hilo eneo
 
Back
Top Bottom