Chama langu Simba hatari inakuja tuchukue tahadhari

M
Mkuu naweza kukupangia vikosi vya Simba tangia kile kilichocheza na Mehla Al Kubra ya Misri 1974, Kilichoitoa The Mighty Mufulira Wanderers 1979, kilicheza na Union Spotive Duala na kupoteza goli nne taifa mwaka 1980, kilichotaka kushuka daraja tukaifunga Yanga taifa 1986, kilichocheza tangia mechi ya mwanzo na Ferreviario de Nampula ya Msumbiji 1993 na kuendelea hadi kuingia fainali ya kombe la Abiola kabda ya kupoteza kwenye fainali mna Stella Abijan, kikosi kilichocheza Ccl makundi 2003 na vyoote hadi cha juzi kilichotambulishwa kwa Mkapa

Lakini nasisitiza kazi ya kupanga kikosi sio yangu ni ya kocha ila akitupangia hivyo tutamlaumu

Jambo la mwisho nikwambie mapenzi yako kwa Simba hayajafikia ya kwangu kwa chama hilo, pengine kabda hujazaliwa
Mzee, umeongea maneno meeengi,wewe huwezi kumpangia kocha, simple toa kikosi unachoamini ni cha ushindani,unazunguka sana Mkuu,unashindwa nini kuweka list unayoamini ndio ya kimashindano na sio ya kimajaribio kama unavyotahadharisha?Mwaga kikosi hapa, hivyo vya Mehala fungia kabatini kwako viendelee kupigwa vumbi.hata hivyo umetoa vidokezo vinavyoashiria wewe ni Shabiki LA Simba kweli na sio Kwasukwasu hongera kwa hilo.Sasa tiririka kikosi unachodhani hiko kitamrarua MTU mithili ya Mnyama Simba porini
 
Hapo hakuna alternative kwa Simba zaidi ya ushindi. Afadhali ile sare waliotoka watani zetu wa Jangwani na Township Rollers, sare ya bao moja kwa moja. Kama Yanga wakikaza ugenini wakatoka angalau sare ya bao mbili kwa mbili au zaidi wanafuzu kwa raundi inayofuata
Acheni matusi someni muelewe hajasema Yanga wakitoka sare bila kufungana. Nyie ndo mumekurupka.
 
Kikosi ambacho naamini kitamrarua Mmakonde bila huruma pale Taifa August 25

..........................Kakolanya

Kapombe..... Wawa .....Nyoni .....Tshabalala

...............................Fraga

...............Chama...,...................Shiboub


.....Kahata............Kagere................. Kanda
 
Kikosi ambacho naamini kitamrarua Mmakonde bila huruma pale Taifa August 25

Kakolanya

Kapombe Wawa Nyoni Tshabalala

Fraga

Chama Shiboub


Kahata Kagere Kanda
Kiko vizuri mkuu ila apo bila kiungo mkabaji sijui kizungu mnaita holding midfield nj hatari
 
Huyo Fraga ndio holding midfielder mwenyewe au umezoea kumuona Mkude
Kwa maoni yangu Fraga azoeshwe hapo, atatusaidia sana huko mbeleni tukikutana na wajuvi zaidi kina Esperance.Halafu Tairone baadae aanze kupatna na Nyoni.Huyu Beki Mbrazili Tairone tunamuhitaji sana aondoe matatizo Mwaka Jana.Na Uzuri wote Nyoni na Tairone wanaweza Holding midfielder hivyo watakuwa wanampa Back up Fraga timu ikiwa INA mpira.
 
Sevilla mwenyewe aliponea kwenye tundu la sindano.pale si mahara pazuri mnyama huwa anacheza kama kajeruhiwa na kifaru.

ngoja tusibiri mtani!
Ila Sijui zahera atatuambia nini sisi wananchi
Mtani hebu wacha utani naona unataka kuwa kama Mc Tilly Chizenga aliyesema eti munaweza ifunga mpaka Barcelona. 😀😀😀

Level hiyo bado sana Mtani.
 
Mtani hebu wacha utani naona unataka kuwa kama Mc Tilly Chizenga aliyesema eti munaweza ifunga mpaka Barcelona.

Level hiyo bado sana Mtani.
Ina maana hujanielewa???kusema Tunaweza kuifunga Barcelona ni alama Ya Mentality ya Ushindi iliyoko Simba!!Ukiwa na Wanasimba ukawaambia Tunaweza kuifunga Barcelona wanakupa tano, ukisema hivi Jangwani wanaweza kukukimbiza kama MTU aliyegundulika anaenda kuchomoa betri!!!Bado tu hujaelewa??
 
Ina maana hujanielewa???kusema Tunaweza kuifunga Barcelona ni alama Ya Mentality ya Ushindi iliyoko Simba!!Ukiwa na Wanasimba ukawaambia Tunaweza kuifunga Barcelona wanakupa tano, ukisema hivi Jangwani wanaweza kukukimbiza kama MTU aliyegundulika anaenda kuchomoa betri!!!Bado tu hujaelewa??
Hahaaa!! Haya bana Mtani we ni MC najua ,usije uhamishia hapa bure sababu najua hamjawahi ishiwa maneno Mtani. 😂😂😂
 
Kikosi ambacho naamini kitamrarua Mmakonde bila huruma pale Taifa August 25
..........................Kakolanya
Kapombe..... Wawa .....Nyoni .....Tshabalala
...............................Fraga
...............Chama...,...................Shiboub
.....Kahata............Kagere................. Kanda
Kikosi safi sana hiki mkuu
SUB: Ally, Gadiel, Tairone da silva, Mzamiru, Dilunga, Bocco, Mkude
 
Back
Top Bottom