Awsom
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 1,085
- 307
Habarini wadau,
Tokea Alhamisi asubuhi mpaka jana jioni kulikuwa na meeting katika ofisi mpya ya CWT iliyojengwa kwa mfuko wa waalimu kuanzia june 2013, Kwakweli ingawa halikuwa katika agenda,ila Ghafla waalimu kwa pamoja walilizungumzia na walikubaliana kutomchagua Mgombea yeyote wa CCM.
Asilimia 80% ya waalimu walisema kuwa CCM imekuwa ikiwadanganya waalimu kama watoto wadogo,yaani wakitoa ahadi ambazo hawazitekelezi kwa miaka yote.
Aliyekuwa katibu wa CWT Mkoa naye alisema tatizo la kutopandishiwa mishahara au kupandishiwa kwa asilimia ndogo sana,Waalimu kutopandishwa madaraja na Malimbikizo ya mshahara ndilo limewafanya waalimu wasiwe na imani na serikali ya CCM tena.
Naye Mwalimu mkuu kwa muda wa miaka 15 kazini alisema kuwa: Hatuwezi kuwapigia kura viongozi wa serikali wanaotudharau na kudharau fani yetu ya ualimu,aliendelea kusema kuwa Waalimu wa taifa hili wamekuwa wakipuuzwa na hata kutukanwa tofauti na wafanyakazi wa taasisi zingine,na wamekuwa wakionekana bora tu wakati kipindi cha kampeni na sensa ya watu na makazi.
Mwishoni kwa kumalizia,Katibu wa CWT kwa waalimu wa shule za msingi yeye alisema tu wanachotaka ni Mabadiliko,ije serikali nyingine labda itawajali waalimu kwa kazi zao ngumu na zisizo na overtime wala marupurupu.
Tokea Alhamisi asubuhi mpaka jana jioni kulikuwa na meeting katika ofisi mpya ya CWT iliyojengwa kwa mfuko wa waalimu kuanzia june 2013, Kwakweli ingawa halikuwa katika agenda,ila Ghafla waalimu kwa pamoja walilizungumzia na walikubaliana kutomchagua Mgombea yeyote wa CCM.
Asilimia 80% ya waalimu walisema kuwa CCM imekuwa ikiwadanganya waalimu kama watoto wadogo,yaani wakitoa ahadi ambazo hawazitekelezi kwa miaka yote.
Aliyekuwa katibu wa CWT Mkoa naye alisema tatizo la kutopandishiwa mishahara au kupandishiwa kwa asilimia ndogo sana,Waalimu kutopandishwa madaraja na Malimbikizo ya mshahara ndilo limewafanya waalimu wasiwe na imani na serikali ya CCM tena.
Naye Mwalimu mkuu kwa muda wa miaka 15 kazini alisema kuwa: Hatuwezi kuwapigia kura viongozi wa serikali wanaotudharau na kudharau fani yetu ya ualimu,aliendelea kusema kuwa Waalimu wa taifa hili wamekuwa wakipuuzwa na hata kutukanwa tofauti na wafanyakazi wa taasisi zingine,na wamekuwa wakionekana bora tu wakati kipindi cha kampeni na sensa ya watu na makazi.
Mwishoni kwa kumalizia,Katibu wa CWT kwa waalimu wa shule za msingi yeye alisema tu wanachotaka ni Mabadiliko,ije serikali nyingine labda itawajali waalimu kwa kazi zao ngumu na zisizo na overtime wala marupurupu.