Chama cha ADC chapata usajili wa muda

Kama umesikiliza habari ya ITV utajua kwamba hawa jamaa kila kitu wamecopy. Mwenyekiti wake mwenyewe anaongea kama Lipumba. Sijui chama gani hiki kisicho na uniqueness.
 
Wachokozi kweli hawa! Mbona rangi zipo nyingi tu....hakuna sababu ya 'kugezana'.

sijui ni mbinu za magamba au ndo kama kawaida yetu wabongo tusivyopenda kuumiza vichwa ,,tunapenda kweli copy and paste
 
Mar 26

[h=1]Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) Chapewa Usajili Wa Muda[/h]



IMG_1321.JPG
Mwenyekiti wa ADC, Said Miraji (kulia) akionesha cheti cha usajili wa muda
IMG_1317.JPG

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa (kushoto) akimkabidhi cheti cha usajili wa muda Mwenyekiti wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Said Miraji katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam
IMG_1271.JPG

Wafuasi wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) , wakipeperusha bendera ya chama hicho kipya huku wakiwa kwenye pikipiki wakati wakitoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini baada ya chama chao kupata usajili wa muda Dar es Salaam.Picha na Mdau Richard Mwaikenda
 
Ni mbinu za CCM kutaka baadae kufoji ili kwenye mikutano ya ADC watakapokuwa wanapata watu kiduchu wao wapate nafasi ya kuwadanganya watu kwamba CDM kimekosa mvuto na kutoa picha za mikutano ya ADC wakionyesha na bendera zinazofanana na CDM kwenye magazeti yao Uchwara yaJamba leo, Habari leo, Uharo, Mzalenda, Dailypuuzi n.k.

Mkuu hapo kwenye red....
 
Vp wana JForum

Kufuatia kupewa usajili kwa chama kingine cha siasa Tanzania,Je utitiri huu wa vyama vya siasa Tanzania ndio demokrasia kukua na kupanuka?
 
Vp wana JForum
Kufuatia kupewa usajili kwa chama kingine cha siasa Tanzania,Je utitiri
huu wa vyama vya siasa Tanzania ndio demokrasia kukua na
kupanuka?

unaujua utitiri wewe? uliza DRC kuna vyama vingapi. 100+ kwetu hata 20 havijafika. of course ni kukua kwa demokrasia.
 
Hii ni ishara ya watu kuwa na njaa kali kwa wao kuanzisha chama ni kujitengenezea ajira hivyo kufuata ruzuku na sio kuwatetea wananchi!
 
mimi ndio siwaelewi kabisaa hawa jamaa, rangi ziko kibao au hata wangechukua kitambaa cheusi waweke vitobo vingiiiiii kwani msajili angelikataa ?
 
Hii ni ishara ya watu kuwa na njaa kali kwa wao kuanzisha chama ni kujitengenezea ajira hivyo kufuata ruzuku na sio kuwatetea wananchi!

kwani dr wenu hajikopeshi ruzuku? Acha watu wajigawanie ruzuku tu. Maana hamna mwanasiasa msafi na hamna siasa safi bongo, dr alikuwa anapiga vuvuzela tu wakati huo lakini kumbe anataka ruzuku pia.
 
Back
Top Bottom