Chama cha ACT-Wazalendo taabani fedha za kampeni

Chama cha ACT-Wazalendo taabani fedha za kampeni

Kaptula la Marx

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2015
Posts
981
Reaction score
449
Hali ya kifedha ya Chama cha ACT-Wazalendo ni taabani, Kaptula La Marx anaweza kuthibitisha. Kwa mjibu wa taarifa kutoka vyanzo vya uhakika ndani ya ACT-Wazalendo akaunti za chama hicho kichanga zina salio la fedha kiasi cha shilingi millioni kumi zikiwa ni ada ya viti maalum pamoja na fedha zilizoingizwa kimakosa katika akaunti hiyo ya kampeni kutokana na ada ya madiwani. Habari zaidi kutoka ndani ya ACT-Wazalendo zinasema kuwa mgombea urais kupitia chama hicho, Mama Anna Elisha Mgh'wira anatarajia kuendelea na ziara yake katika mikoa ya kusini ambako viongozi wa hiyo mikoa wameandika barua kudai hizo pesa ili waendelee na maandilizi. Nakala ya barua hizo mwandishi anazo lakini hataziweka hapa kwa sasa kwa sababu sio vizuri kumaliza risasi zote kwenye bunduki kwa wakati mmoja. Mwandishi ataendelea kumwaga risasi moja baada ya nyingine, na hatua kwa hatua ili kuumbua vikundi vya kitapeli na kilaghai kama hiki cha ACT-WAZALENDO na mawakala wao.

Kutokana na ukata huo wa fedha, timu ya mikakati ya kampeni ndani ya ACT-WAZALENDO imeshauri ziara za mgombea Urais kupitia ACT-WAZALENDO mama Anna Elisha Mgh'wira ziendelee ili kiasi cha fedha kinachofikia milioni 7 kitolewe katika fedha hiyo ya milioni kumi iliyoko kwenye akaunti maalum kwa ajili ya kampeni. Kwa mjibu wa mnyetishaji wangu kutoka jikoni ndani ya ACT-WAZALENDO, kiasi cha milioni 3 kilichosalia kimetolewa kwa ajili ya services ya magari ya kampeni ili kesho mgombea wa Urais na timu yake waondoke kwenda kuendelea na kampeni huko mikoani. Kaptula La Marx hajaweza kuthibitisha kama kiasi cha milioni 7 kinatosha kuandaa mikutano mingapi yenye hadhi inayotakiwa na ikiwa hiyo fedha itatumika kwa siku ngapi. Inahitajika bana matumizi kali kweli kweli. Mgombea wa Urais kupitia chama hicho cha ACT-WAZALENDO anatarajia kuendelea na ziara yake mikoa ya kusini, hususani Lindi, Mtwara na Ruvuma; na akimaliza huko ataelekea Zanzibar. Chanzo changu kilithibitisha

Kuvuja kwa taarifa hizi za ACT-WAZALENDO kuwa taabani kifedha kunakuja ikiwa ni baada ya mazungumzo yao na chama dada cha CCM kutozaa mafanikio. Mnyetishaji wangu kutoka jikoni ndani ya CCM na Ikulu amenithibitishia kuwa "Makubaliano yetu na Kuongozi Mkuu wa ACT-WAZALENDO, Mh.Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah, yalikuwa kwamba CCM itaisaidia ACT-WAZALENDO gharama za kampeni kama watasimamisha mgombea wa Urais ili kupunguza makali ya nguvu kubwa za mgombea wa CHADEMA, anayewakilisha pia UKAWA ndugu Edward Lowassa". Hata hivyo, mnyetishaji wangu huyo amesema CCM wamegundua kuwa uwepo wa mgombea wa Urais kupitia ACT-WAZALENDO hakujaleta athari zozote kwa UKAWA kama CCM walivyotarajia. Kutokana na hali hiyo, CCM wameendelea kusita katika kutoa fedha hizo ambapo makubaliano ya awali ilikuwa watoe kiasi cha milioni 800 katika awamu ya kwanza ya kampeni; na kiasi cha milioni 800 kilichobaki kitolewe katika awamu ya pili ya kampeni.

Hata hivyo, mpaka wakati wa kuandika andiko hili, mwandishi hakuweza kuthibitisha ni asilimia ngapi ya kiasi hicho cha fedha imetolewa katika awamu ya kwanza ya kampeni mpaka sasa. Mawasiliano kwa ajili ya kupata kiasi kamili kilichotolewa mpaka sasa yanaendelea ndani ya CCM na ACT-WAZALENDO. Kutokana na mkwamo huo, mnyetishaji wangu ndani ya ACT-WAZALENDO amenithibitishia kuwa viongozi wakuu wa wa chama hicho wameamua kuandaa fundraising dinner itakayofanyika tarehe 2th Oktoba, 2015 ili kuokoa jahazi. Mpaka sasa maandalizi ya fundraising au harambee hiyo yanaendelea na yako katika hatua nzuri. Mmoja wa vigogo ndani ya ACT-WAZALENDO, amenithibitishia kuwa kama hali itaendelea kuwa ni ya ukata kama ilivyo sasa, itaathiri kwa kiasi kikubwa kampeni za chama hicho katika ngazi zote za urais, ubunge na udiwani.

Kigogo huyo amewalaumu pia viongozi wenzake kwa kitendo chao cha kukaidi ushauri wa kitaalamu uliowataka wasisimamishe mgombea wa Urais, na badala yake wajikite kwenye majimbo na udiwani. Aidha, ushauri huo wa kitaalamu uliotolewa na watalaamu wao uliwataka ACT-WAZALENDO wasimamishe wagombea wachache wa ubunge na udiwani hususani katika maeneo ambayo chama chao kina nguvu kubwa kama Kigoma na baadhi ya maeneo katika mikoa ya Katavi, Tabora na Kagera. Lakini kiongozi mkuu wa chama hicho, alikataa katakata kwa madai kuwa tayari alikuwa ameshaongea na viongozi wakuu wa CCM waliokuwa wamemhakikishia kumpa fedha za kampeni. Pamoja na viongozi wakuu wa chama hicho kujitapa kuwa ndicho chama cha pili kuwa na wagombea wa Ubunge wengi baada ya CCM, lakini kutokuwa na rasilimali za kutosha ili kugharamia kampeni hizo kutakifanya chama hiki kipoteze hata vile viti ambavyo kingeweza kuvipata kama kingekuwa na wagombea wachache.

Kaptula La Marx (Jikoni muda huu)
 
ACT wazalendo....ni chama makini mbadala

Ni chama makini wakati ni genge la wahuni & matapeli? Soma bandiko kwanza mkuu uunganishe dots. Nasubiri mtu wa ACT-WAZALENDO akanushe haya niendelee kushusha nondo
 
Waliotembeza bakuki pale mlimani city was hawajaishiwa wanazo nyingi tuuu ndio maaana HAWAOMBI
 
Wakifanya kampeni kwa spidi mnahoji fedha zinatoka wapi,wasipofanya mnawacheka wamefulia,sasa cjui nyie mnataka wafanye nn.
 
Mtowa news ana onyesha wazi kwamba haipendi ACT sasa watu wata aminije? Muda mungine tumieni akili kuandika sio vidole tu

Kama watu hawaamini walete ushahidi ili kukanusha haya niliyoandika. Lakini mimi nakuhakikishia kuwa haya niliyoyasema ni uhakika 100%. Niko jikoni kabisa, najua kila kitu. Niko CCM na ACT-WAZALENDO kwa kazi maalum kama hivi ninavyowajuza.
 
Mtowa news ana onyesha wazi kwamba haipendi ACT sasa watu wata aminije? Muda mungine tumieni akili kuandika sio vidole tu


Mkuu mtoa mada kasema itadhibitika mada yake ni ya ukwel ifikapo tar 2/10/2015 ambapo itakua n fund raising dinner ya hicho chama.
 
Ni chama makini wakati ni genge la wahuni & matapeli? Soma bandiko kwanza mkuu uunganishe dots. Nasubiri mtu wa ACT-WAZALENDO akanushe haya niendelee kushusha nondo

Sasa si afadhali act wanacampeni mpaka wanaishiwa, halafu wanafanya mikakati ya kupata hela zaidi, je nyie mliouzwa kwa bei ya hasara ( jumla ). Sasa bendera yenu inapeperushwa na jamaa kutoka chama jirani. 😛 laana yenu ni maradufu.
 
Wakati CCM ina billion 150 za kampeni ACT wana millioni kumi.Pamoja na dhambi ya usaliti lakini ni dhahiri ulingo wa kisiasa hautoi fursa sawa kwa vyama vyote.
 
Iwapo act_wasaliti wakiingia ikulu basi bwana zitto ayakuwa ndo firstlady
 
Hiki ni chama cha makabwela, Si chama chenye fedha nyingi, Bora chama cha aina hii maana hakina fedha za Mafisadi!
 
Wapi MOTOCHINI na mwekundu wakachangie vibaraka wenzao?
Jahazi linazama hivyo!

Chama kichanga lakini ndo nuru na tumaini la watanzania hadi hapa kilipo kina jitahidi!!sasa unashangaa nini hapa?mbona mbowe juzi ameanza kupitisha bakuri la michango?tena wale waliokua kwenye list of shame ndo wanakichagua?
 
Last edited by a moderator:
Chama kichanga lakini ndo nuru na tumaini la watanzania hadi hapa kilipo kina jitahidi!!sasa unashangaa nini hapa?mbona mbowe juzi ameanza kupitisha bakuri la michango?tena wale waliokua kwenye list of shame ndo wanakichagua?

Inashangaza kufulia wakati mna wafadhili.
Hamna jipya ndio maana wamewatosa,mkipata hata wabunge wa5 nitafute unikumbushe tamko hili.
 
Inashangaza kufulia wakati mna wafadhili.
Hamna jipya ndio maana wamewatosa,mkipata hata wabunge wa5 nitafute unikumbushe tamko hili.

We ni kituko kwani chadema wanaoomba hawana wafadili?
 
inashangaza kufulia wakati mna wafadhili.
Hamna jipya ndio maana wamewatosa,mkipata hata wabunge wa5 nitafute unikumbushe tamko hili.

mbowe na lowa sasa walikuwa wanaomba muwachangie ilihali chama kinapewa ruzuku tofauti na act?
 
Kwani wanakutana na Wanachaggadema tu huko kwenye kampeni.Kwanini wapunguze kura za Chaggadema na siyo za CCM???!Na kwanini UPDP,UDP,APPT Maendeleo,SAU,ADC wasipunguze kura za UKIWA??Kwanza CHAGGADEMA ndo inapunguza kura za ACT Wazalendo ili CCM ishinde.
 
Back
Top Bottom