Chalamila: Rais Samia ni kama nabii

Chalamila: Rais Samia ni kama nabii

comrade_kipepe

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2019
Posts
6,446
Reaction score
11,504
Screenshot_20260303_162824_Instagram.jpg

"Nabii" ni neno la Kiswahili lenye maana ya mjumbe au msemaji kwa niaba ya Mungu

Chalamila anamuweka samia kundi moja na watu kama Yohana Mbatizaji na wakina Musa.

Hapa ndio wanaosema hakuna Mungu wanapokua na point, Kama kweli Mungu yupo, kwa damu aliomwaga anaruhusu vipi hizi dharau ziendelee?!

Ngoja tuone.

======

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amesema uwekezaji wa Serikali katika ujenzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ni hatua muhimu ya kulilinda taifa dhidi ya misukosuko ya kiuchumi inayoweza kutokea duniani.

Ametoa kauli hiyo leo, Machi 3, 2026, wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa matanki ya kupokea mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.

Soma Rais Samia: Wizara ya Nishati iimarishe akiba ya kimkakati ya mafuta ili kujilinda dhidi ya misukosuko ya siasa za kidunia

Chalamila amesema kuwa miradi mikubwa kama hii mara nyingi wananchi wa kawaida hudhani haiwahusu, lakini kwa muktadha wa matukio ya dunia, umuhimu wake ni mkubwa kuliko inavyodhaniwa.

“Mheshimiwa Rais unapotekeleza miradi kama hii ni rahisi kwa mwananchi wa kawaida kuhisi kwamba mradi huu sio wa watu. Mtu wa kawaida akiangalia anaweza kudhani haumhusu yeye, lakini Mheshimiwa Rais wewe umekuwa kama nabii. Kwa yale yanayoendelea duniani leo, unaweza kuona hatari ya taifa kukosa maghala yanayomilikiwa na Serikali.” amesema
 
Kutoka 20:7 NEN
Usilitaje bure jina la BWANA Mungu wako, kwa kuwa BWANA hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.


Yer 17:5 SUV
BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.

Marko 13:31 (pia Mathayo 24:35 na Luka 21:33), ambapo Yesu anasema: "Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe"

WAFALME WA DUNIA WATAPITA....VYEO VYA DUNIA VITAPITA...

Kutoka 20:3-17
“Usiwe na miungu mingine ila mimi.

Mt 12:36-37
Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.
 
Kwa yale yanayoendelea duniani leo, unaweza kuona hatari ya taifa kukosa maghala yanayomilikiwa na serikali​
Kama serikali inajali sana kuwa na matenki ya hifadhi ya mafuta, kwa nini iliachia 50% ya umiliki wa TIPER kampuni ya matenki ya kuhifadhi mafuta, na kuwapa wageni?

Kwa mwendo huu kuna siku mtauza Serengeti yote kisha mseme tutengeneze mbuga ya wanyama mpya ya serikali!
 
Mbona lema huwa anashangiliwa na kuitwa hivyo pia
 
Back
Top Bottom