Chadema

rosemarie

JF-Expert Member
Mar 22, 2011
6,889
3,412
Kwa Wakuu wote wa Chadema
napenda kuchukua nafasi hii kuwauliza kama kweli mna mpango wa kuchukua madaraka 2015
kila wakati nikiwaza miaka mingine mitano na ccm nakata tamaa,je wakuu mna mpango kweli wa kuchukua Nchi?hivi kwa sasa hivi baada ya uchaguzi wa Igunga kuna nini kinaendelea ndani ya chama?
napenda kuwafahamisha tumaini la Watanzania lipo mikononi mwenu,kama chama cha Cuf wangekuwa hawajaungana na ccm tungewashauri kufanya makubaliano ya kuunganisha vyama hivi viwili haraka jinsi inavyowezekana
kwa sasa hivi sioni chama chochote ambacho kinaweza kuunganisha nguvu na nyie,Nccr wako hoi!
sasa basi kama mna mpango wa kuchukua madaraka 2015 mtayachukuaje?je ni rahisi kunyang'anya ccm madaraka?kwani wao hawataki kutawala?
ccm ndio wanajua utamu wa kutawala,ukionja asali lazima uchonge mzinga!
wakuu mimi nina mashaka sana na mwenendo mzima wa mabadiliko,kwa kweli sielewi mpaka sasa hivi kama mna mipango yoyote mipya ya kuchukua madaraka
kuchukua madaraka sio kitu rahisi kama tunavyofikiri,mmejionea wenyewe uchaguzi wa igunga mambo yalivyokuwa,nawahakikishia hata uchaguzi mkuu 2015 itakuwa kama igunga!
nitahuzunika sana kama Chadema mkituangusha na kuachia ccm iendelee kutawala 2015,ina maana tutaendelea na ccm mpaka 2020,jamani ni mbali sana tumeshateseka kiasi cha kutosha
nina mengi sana kuhusu hii mada,kwa ujumla nina mashaka na maandalizi ya kuchukua madaraka,ninachojua ,huwezi kujenga nyumba bila kuchora ramani,na mjenzi atatumia ramani iliyochorwa na wataalam kukadiria matumizi yote mpaka nyumba kukamilika,
Viongozi wote wa chadema nawashauri kubalini kubadilika sasa hivi kama itawezekana,msiridike na hatua mliopiga,yaani kwa ujumla hamjafika hata nusu ya safari,
jengeni uhusiano wa karibu na chama cha Pf cha Zambia,Rais wake Sata amepitia mengi na kwa taarifa yenu haipendi ccm hata chembe, source ni mimi mwenyewe nilikuwa zambia
ndugu zangu chadema mna jukumu kubwa sana lakini mashaka yangu kila siku yanaongezeka,Dr Slaa tunajua upo hapa na utatusaidia kwenye hili.
 
CDM wanapambana na kila aina ya vizuizi kutoka kwa watawala, kwa hiyo lazima wawe smart kutuongoza! Na ndicho hicho ninacho amini hadi sasa!
Tuwape muda huku nasi wapenda maendeleo aka wachukia ufedhuli/ufisadi/wizi wa uongozi! tukijipanga kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ndani ya chama ili kusaidiana na viongozi wakuu. Naimani kwa pamoja tutasonga mbele daima, nyuma ni mwiko tulipofikia ni zamu yetu sasa tunaopiga kelele huku majukwaani kuonyesha vitu kwa vitendo.
 
usihofu..sasa hivi chama kinajiimarisha kwa kujenga ofc na kufungua matawi vijijini huko


attachment.php
 
mimi binafsi niliomba tuige baadhi ya mambo kutoka ccm,kwa mfano nafasi aliyo nayo nape sijui kama kuna mtu wa nafasi hiyo,yaani katibu mwenezi,nafikiri kwa kuwa tuna wakati mgumu tungekuwa na makatibu waenezi watatu na kazi yao ni kufungua mashina na kuelimisha
 
@Malaria Sugu, kwenye ile thread nyingine unalalamika kuwa CHADEMA wanafanya mambo ya kitoto, sasa dakika chache baadae unalaumu CHADEMA wamekuwa kimya! Hii inaonesha jinsi ulivyo obsessed na CHADEMA.
 
@Malaria Sugu, kwenye ile thread nyingine unalalamika kuwa CHADEMA wanafanya mambo ya kitoto, sasa dakika chache baadae unalaumu CHADEMA wamekuwa kimya! Hii inaonesha jinsi ulivyo obsessed na CHADEMA.

Obsessed kivipi mkuu'ili ni wazo langu sijasukumwa na ms hata kidogo
 
Ni vizuri tukajua kuwa chadema sio mboye, dr. slaa wala ndesa. Hawa hawawezi kufika kila mahali, kwa maana nyingine kushindwa kwa cdm lawama hazitaenda kwao peke yao. Na pia ukumbuke, ushindi hautokani na wao tu, bali ushindi utategemea kiasi gani tunawapa support. Mi naona kabla ya kuhoji wamejipanga vipi, ulitakiwa kwanza ujihoji kwamba, kwa nafasi yako wewe hapo ulipo umechangia vipi ktk kuleta mabadiliko?

Watu kama wewe hawatakiwi katika jamii inayotafuta mabadiliko. Usije ukajidanganya hata siku moja kwamba lema ataleta mabadiliko bila support ya watu wa arusha. Wanampa support ndiyo maana unamwona ni mpiganaji. Hakuna jeshi la mtu mmoja duniani.
 
Tusiwalaumum uongozi wa juu wakati wanamagezi tupo. Kitu cha kuangali ni sisi wenyewe je tunaushawishi kiasi gani kwa jamii wakati tunaona uongozi wamebanwa kila upande na wanatoa ushirikiano mara wanapoona tatizo juu ya wanachama wao. Mf Mh Lema amewagusa watanzania wengi kiasi wengine hawaamini kama mbuge amekubali kwenda gerezani kwa ajili ya wanachama wa chadema waliokamatwa kwa kesi isiyokuwa na kichwa wala miguu.

My take: Tuhakikishe kila upande katika Tanzania hii ina nguzo inayofaa kuelimisha jamii, kuanzia mashina mpaka mkoa. Viongozi wa wilaya na mkoa wasilale hao ndio nguzo kubwa wakisaidiwa na wabunge. Wawe tayari kama Mh Lema kupambana wanapotafuta haki bila kuvunja sheria.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom