Demokrasia ianzie kwenye chama chako kwanza. Kuna mtu ni mwenyekiti kwa miaka 20 sasa. Ukigombania hiyo nafasi aidha ufukuzwe kwenye chama uitwe msaliti , umauti ukupate, ukikoswakoswa basi upate kilema cha maisha kama yule aliyepo ubelgiji.Naona umetoka jela na nguvu nyingine. Cdm sio chama cha kigaidi, sasa hivi cdm inafanya siasa dhidi ya polisi na kundi la watu wasiojulikana. Hivyo inabidi ili ifanye ulichokuwa unakiona hapo kabla, inabidi wamiliki silaha za kijeshi ili iweze kwenda sambamba na siasa hizo. Sasa ccm imekuwa chama cha pili kwa umaarufu, baada ya yesu wa chattle kujigeuza yeye ndio mihili ya nchi.
By nature yesu wa chattle hawezi siasa za ushindani, bali anahitaji kuabudiwa tu, na yoyote anayemkosoa anaishia jela, kuachiwa kilema cha maisha, kuhujumiwa shughuli zake za kujiingizia kipato nk. Kwa ujumla yesu wa chattle anaaminisha wananchi kuwa ukiwa na demokrasia, huwezi kupata maendeleo.
Upinzani unapita kipindi kigumu huenda kuliko kipindi cha ukoloni wa mzungu
Demokrasia ianzie kwenye chama chako kwanza. Kuna mtu ni mwenyekiti kwa miaka 20 sasa. Ukigombania hiyo nafasi aidha ufukuzwe kwenye chama uitwe msaliti , umauti ukupate, ukikoswakoswa basi upate kilema cha maisha kama yule aliyepo ubelgiji.
Chadema kama TLP,Mbowe ni Mrema ajaye
Demokrasia ianzie kwenye chama chako kwanza. Kuna mtu ni mwenyekiti kwa miaka 20 sasa. Ukigombania hiyo nafasi aidha ufukuzwe kwenye chama uitwe msaliti , umauti ukupate, ukikoswakoswa basi upate kilema cha maisha kama yule aliyepo ubelgiji.
Moja ya kosa kubwa kwenye vyama ambavyo vinatangaza kuwa na Demokrasia ni kumuachia kiongozi wake kukaa kwenye uongozi zaidi ya miaka 20.Mimi sio muumini wa kiongozi kukaa madarakani zaidi ya miaka 10, na msimamo wangu uko wazi kwenye hilo, na post zangu ziko humu humu jukwaani. Huyo kiongozi aliyekaa miaka 20 nimeenza kumpinga toka alipozidi na miaka 10. Na sasa Kavuka 15 ndio nimeepinga, na nitaendelea kupinga kwa nguvu zangu zote. Kwa bahati mbaya mimi sio mwanachama wa chama chochote cha siasa, bali shabiki wa kutupwa wa cdm. Hivyo sina maamuzi yoyote kwenye chama hicho unachokisema, au chama chochote kile.
Hayo ya watu kutekwa, kuachiwa vilema, hata ufanyeje bado huwezi kubadilisha ukweli, hizi ni tabia za jiwe na ndio maana anasaka kinga ya kutoshtakiwa akitoka madarakani. Yaani hilo wala halihitaji elimu kubwa ya kujua kuwa jiwe ndio anamiliki kundi la watu wasiojulikana.
Moja ya kosa kubwa kwenye vyama ambavyo vinatangaza kuwa na Demokrasia ni kumuachia kiongozi wake kukaa kwenye uongozi zaidi ya miaka 20.
Hali ni ngumu sana pia bila tume huru tunaenda kushuhudia kilichotokea uchaguzi wa Serikali za Mitaa kinatokea kwenye uchaguzi mkuu.Hiyo haihitaji kuwa na binocular kuigundua