Mimi sio muumini wa kiongozi kukaa madarakani zaidi ya miaka 10, na msimamo wangu uko wazi kwenye hilo, na post zangu ziko humu humu jukwaani. Huyo kiongozi aliyekaa miaka 20 nimeenza kumpinga toka alipozidi na miaka 10. Na sasa Kavuka 15 ndio nimeepinga, na nitaendelea kupinga kwa nguvu zangu zote. Kwa bahati mbaya mimi sio mwanachama wa chama chochote cha siasa, bali shabiki wa kutupwa wa cdm. Hivyo sina maamuzi yoyote kwenye chama hicho unachokisema, au chama chochote kile.
Hayo ya watu kutekwa, kuachiwa vilema, hata ufanyeje bado huwezi kubadilisha ukweli, hizi ni tabia za jiwe na ndio maana anasaka kinga ya kutoshtakiwa akitoka madarakani. Yaani hilo wala halihitaji elimu kubwa ya kujua kuwa jiwe ndio anamiliki kundi la watu wasiojulikana.