CHADEMA yawatia shime Serengeti Boys

Tumaini Makene

JF-Expert Member
Jan 6, 2012
2,642
6,071
CHADEMA YAWATIA SHIME SERENGETI BOYS

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatoa salaam za heri kwa Vijana wa Timu ya Taifa chini ya miaka 17, Serengeti Boys wanaoiwakilisha nchi yetu kwenye mashindano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Vijana, ambao leo wameingia dimbani kwenye mechi yao ya kwanza dhidi ya Timu ya Mali, ambayo ni bingwa mtetezi wa kombe la michuano hiyo.

Tunapenda kuwatia shime vijana hao kuwa wamebeba dhamana kubwa ya taifa letu katika mashindano hayo na matamanio ya Watanzania ambao wangependa kuona jina la nchi yao likiwika na kutamkwa katika mafanikio ya mchezo wa soka barani Afrika na dunia kwa ujumla.

Kutokana na matokeo waliyopata leo ya kutoka sare tasa dhidi ya timu bingwa mtetezi na kwa kuzingatia mwenendo wao katika safari ya kuelekea fainali hizo nchini Gabon, kuanzia kwenye hatua ya mtoano, kisha maandalizi waliyoyapata wakiwa kambini Morocco ambapo walishinda michezo mitano ya kirafiki kati ya saba waliyocheza huku wakitoka sare mmoja na kupoteza mmoja, wakizifunga timu mahiri barani Afrika, Watanzania wamewekeza matumaini yao kwa vijana hao kuwa wataipatia heshima nchi yetu na kumaliza kiu ya muda mrefu ya kutaka kuona timu zao za taifa zinazoshiriki kwenye mashindano ya michezo mbalimbali, zinaliweka jina la nchi yetu katika 'ramani ya michezo' duniani.

Watambue kuwa Watanzania wa kila hali bila kujali tofauti zao zozote, wanafuatilia fainali za mashindano hayo kwa ari kubwa kwa sababu hawatazami tu sura za vijana wa mataifa mengine, bali pia wanafuatilia ushiriki wa vijana wao mahiri, hivyo ushindi wao kwa kila mechi (zinazofuata) na hatimae kufika mbali katika michuano hiyo na kuchukua ubingwa, utakuwa furaha na heshima kubwa kwa Watanzania wote na nchi kwa ujumla.

Mungu ibariki Serengeti Boys

Mungu ibariki Tanzania

Imetolewa Jumatatu, Mei 15, 2017 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
IMG-20170516-WA0008.jpg
 
Mtatafuta sana kiki mwaka huu ..wakati WA kuwachangia chadema mlikuwa wapi?mlitoa shilingi ngapi? Chama kimekwisha..no Sera..no Dira..kinakwenda na matukio..Mara kiki za misibani kugombea mic..shame on you ..I wish Dr slaa angekuwepo
 
Mtatafuta sana kiki mwaka huu ..wakati WA kuwachangia chadema mlikuwa wapi?mlitoa shilingi ngapi? Chama kimekwisha..no Sera..no Dira..kinakwenda na matukio..Mara kiki za misibani kugombea mic..shame on you ..I wish Dr slaa angekuwepo
Wewe unadhani.chadema wanakula pesa za rambirambi kama ccm?leo hii baba bashite na ccm yake wanaomb a Mungu serengeti boys wapate ajali ili wale rambirambi tena yaani serikali imeishiwa hadi kuombea wananchi wapate matatizo ili tu wapate kuiba rambirambi zao


Swissme
 
Kwa hili niwapongeze Cdm kwa kunesha uzalendo na kutanguliza mbele maslahi ya taifa. Siasa zinakiwa zituweke pamoja na sio kujitenga. Tunashukuru kwa kuonesha utaifa pia nashauri mhimize michango kwa wanachama wenu na watanzania wote kwa ujumla ili kutoa hamasa kwa vijana wetu. Mungu ibariki Tanzania
 
Wewe unadhani.chadema wanakula pesa za rambirambi kama ccm?leo hii baba bashite na ccm yake wanaomb a Mungu serengeti boys wapate ajali ili wale rambirambi tena yaani serikali imeishiwa hadi kuombea wananchi wapate matatizo ili tu wapate kuiba rambirambi zao


Swissme
Maneno ya kipuuzi na kilofa yaliyosemwa na mlevi wa buza kupindukia.
 
Siku alipochaguliwa mtu anaitwa Mashinji kuwa katibu wa chama ndo siku cdm ilipojitumbukiza kwenye shimo
 
Wewe unadhani.chadema wanakula pesa za rambirambi kama ccm?leo hii baba bashite na ccm yake wanaomb a Mungu serengeti boys wapate ajali ili wale rambirambi tena yaani serikali imeishiwa hadi kuombea wananchi wapate matatizo ili tu wapate kuiba rambirambi zao


Swissme
Umemjibu kadri anavyostahili...
 
Maneno ya kipuuzi na kilofa yaliyosemwa na mlevi wa buza kupindukia.
Kwa hiyo kula rambirambi za wahanga wewe unaona sifa ok BUKOBA MMEKULA ARUSHA MMEKULA sasa mnawaombea SERENGETI BOYS wapate ajari ili mle tena?haki ya Mungu hamtaweza tena kula rambirambi za wahanga UKAWA tutasimamia mazoezi yote


Swissme
 
Wanataka kutuletea nuksi na sumu ya siasa kwenye soka...waacheni vijana wacheze soka msilete siasa.
Hii ni kukosa jambo la maana la kuwaambia wananchi...mmebakia kudakia na kurukia matukio tu.

subirini msiba muhudhurie na kushika mic
 
Mtatafuta sana kiki mwaka huu ..wakati WA kuwachangia chadema mlikuwa wapi?mlitoa shilingi ngapi? Chama kimekwisha..no Sera..no Dira..kinakwenda na matukio..Mara kiki za misibani kugombea mic..shame on you ..I wish Dr slaa angekuwepo
Waziri mkuu alichangisha bungeni wabunge wote walitoa mchango wakiwemo wa vyama vyote acha kuhusisha mambo ya michezo na kiki.
 
Wanataka kutuletea nuksi na sumu ya siasa kwenye soka...waacheni vijana wacheze soka msilete siasa.
Hii ni kukosa jambo la maana la kuwaambia wananchi...mmebakia kudakia na kurukia matukio tu.

subirini msiba muhudhurie na kushika mic
Wanasiasa ndiyo wameichangia hiyo Timu na hawakuchanga kwa kutumia siasa na kuipingeza timu sio Nuksi wala siasa
 
Wanataka kutuletea nuksi na sumu ya siasa kwenye soka...waacheni vijana wacheze soka msilete siasa.
Hii ni kukosa jambo la maana la kuwaambia wananchi...mmebakia kudakia na kurukia matukio tu.

subirini msiba muhudhurie na kushika mic
Tetetetete Ukawa wamewapiga bao



Swissme
 
Wanataka kutuletea nuksi na sumu ya siasa kwenye soka...waacheni vijana wacheze soka msilete siasa.
Hii ni kukosa jambo la maana la kuwaambia wananchi...mmebakia kudakia na kurukia matukio tu.

subirini msiba muhudhurie na kushika mic
Tetetetete Ukawa wamewapiga bao



Swissme
 
Mtatafuta sana kiki mwaka huu ..wakati WA kuwachangia chadema mlikuwa wapi?mlitoa shilingi ngapi? Chama kimekwisha..no Sera..no Dira..kinakwenda na matukio..Mara kiki za misibani kugombea mic..shame on you ..I wish Dr slaa angekuwepo
Kwani CCM wamechangia sh.ngapi?
 
Asante sana, hii ni hatua nzuri kuelekea Tanzania tunayoitaka. Tanzania yenye vyama vya siasa vinavyolenga kuwa boreshea watanzania hali nzuri za kimaisha na kusonga mbele kimaendeleo. Tuepuke siasaza kukwamisha mmaendeleo ya watanzania kwa kuingiza siasa za kugawanywa linapokuja suala la kitaifa. Ninaunga mkono tamko hili la Chadema. Natarajia matamko mengine kama haya ya kutuweka pamoja watanzania na wala si vinginevyo kutoka kwa Chadema ama chama chochote cha siasa. Mungu ibariki Serengeti Boys, Mungu ibariki Tanzania. Amen.
 
Back
Top Bottom