CHADEMA yawapa raha watanzania: Taifa Lazizima

fmpiganaji,

Bravo. Huo ni ukweli na ukweli mtupu. CHADEMA wanastahili pongezi za dhati kabisa. Frankly speaking CHADEMA ndiyo kioo cha Uongozi katika Taifa hili mabalo kwa sasa limepoteza mwelekeo kutokana na uongozi MBOVU wa Chama cha Magamba.
Kwa heshima na Taadhima napenda nami kuwapa pongezi nyingi Viongozi waandamizi wa CDM,Wabunge,Wanachama na Wapenzi wa CDM.

Sitakuwa nimetenda haki pasipo kumtaja Marehemu, dada yetu mpenzi Bi Regia Mtema(RIP) kwa mchango na mawazo yake kwenye mchakato huu kabla hajatutoka mapema mwezi uliopita.
Kumbe sasa napata picha kwamba tatizo la Kikwete ni washauri wabovu, waliovimbiwa ufisadi na kupofushwa na tamaa zao binafsi yaani wao kwanza, taifa baadae. Nasema hivi kwa sababu baada ya Kikwete kukaa chini na kuwasikiliza CHADEMA vizuri aligundua mapungufu mengi yaliyochomekwa kwenye ule muswada aliousaini (Kwa hili anastahili pongezi) na kilichofuata ni kuchukua uamuzi mgumu kabisa dhidi ya mavuvuzela yake na kuurudisha muswada ule Bungeni bila kujali vitisho vya kupigiwa kura za kutokuwa na imani. Hebu sasa tujiulize, ni mara ngapi JK kapotoshwa na washauri wake na kufanya maamuzi yaliyompunguzia mvuto na heshima?
My Take:
JK sasa amegundua kwamba ni salama zaidi kusimama upande wa umma kuliko wa mashabiki na walevi wa kifisadi. Namshauri asisite kushirikiana na wapinzani hata katika masuala tata kama hili linalolitesa taifa sasa la mgomo wa madaktari ili kuiepusha nchi na maafa yasiyo ya lazima.
 
Pamoja na kuwapongeza CDM na JK kufanikisha, hatutajisahau sisi wana JF kujipongeza kwa kutoa elimu kwa members wengine kama kina ritz, rejao, FF na wenzao waliokuwa wanabeza walk out ya wabunge wa CDM. Hili liwe fundisho kwao pamoja na wabunge wa CCM na CUF waelewe kuwa si kila kitu kinacholetwa na wapinzani ni cha kupinga.
 
Hongera cdm na makamanda wote, hongera JK.. mchambuzi nakupa hongera zako umefanya kazi nzuri ilinayostahili pongezi, mimi naona tunaelekea kuona mwanga wa ukombozi, mashaka yangu ya 2015 yamepungua sana japo huu ni mwanzo tu.. yawezekana mzee wa kaya kaona nguvu ya umma ndio silaha pekee ya kumkwamisha Mzee white maana spidi yake sasa inaonekana hakuna wa kuizuia ndani ya magamba, na nguvu hiyo inapatikana kwa cdm pekee kwa kuwepo kwa katiba nzuri.. sijui ila ni mawazo yangu tu wadau.
 
Hizi ndio thread za viwango vya JF ambazo zimekuwa adimu sana kipindi hiki, Nawaomba memba wenzangu bila kujari kwamba Thread inawapongeza Chadema ninachokiomba tuwe na uandishi na uchangiaji wa namna hii.
Hongera zako mleta mada, nimependa ulivyojipanga kuwasilisha mada yako, na ninamualika Pdidy wa humu JF aje kujifunza namna bora ya uandishi kwenye thread hii. kudos.
 
Wakati tukiwapongeza mashujaa waliofanikisha kufika hapa, tusisahau kuwalaani na wale waliojaribu kusambaratisha hii safari takatifu. Wapo wengi lakini tuwataje wachache wawakilishe wenzao;

1. Mh. Celina Kombani
2. Mh. Anne Kilango Malecela
3. Mh. Anna Makinda
4. Mt. Seif Sharif Hamad
5. Mh. Jussa
6. Yule Mbunge mnafiki wa CUF aliyesema hao siyo Wapinzani

Eeh, Mungu uwasamehe hawa kwani hawajui watendalo. Washindwe na walegee.

Hapo kwenye red: Mt. ni kifupisho cha mtoro, mtukutu, mtakatifu au mountain?
 
Ndio maana huwa mimi nadhani mashabiki wote wa chadema wamerukwa na akili na kama si hvyo basi ni kwamba mnajifanya wajuaji saaana tu mpaka mnakuwa kama wajinga.kwanini swala la katiba mnalifanya kam lenu na kujigamba eti nyie ndio source?acheni masifa bwana it wl cost u!
 
Kuelewa kunategemea uwezo kiakili mkuu. ukiona huelewi ingia kundi la akina Rejao.
Hilo ndilo kundi gani?
Hongereni CDM kwa kushindwa kufanya SWOT dhidi ya chama tawala ili muweze kuwashawishi wananchi vizuri 2015!
Suala la katiba limeshafanyiwa kazi na CCM...2015 mtakuja na sera gani????
 
Mimi nafikiri mpaka sasa kwa mtanzania wa kweli mwenye kuitakia mema nchi hii ameshawatambua Chadema ni nani na wapo kwa maslahi ya watanzania, na pia tumeshagundua usani wa wabunge walio wengi wa ccm na cuf, ila pia nimefurahi kumfahamu jinsi Anne kilango Malecera alivyo na ubinafsi na kutoitakia mema nchi hii.

Viva Chadema tupo pamoja mpaka nchi yetu ya maziwa na asali itakapokombelewa upya.
 
Hizi ndio thread za viwango vya JF ambazo zimekuwa adimu sana kipindi hiki, Nawaomba memba wenzangu bila kujari kwamba Thread inawapongeza Chadema ninachokiomba tuwe na uandishi na uchangiaji wa namna hii.
Hongera zako mleta mada, nimependa ulivyojipanga kuwasilisha mada yako, na ninamualika Pdidy wa humu JF aje kujifunza namna bora ya uandishi kwenye thread hii. kudos.

Mkuu Matola hata mimi nimeipenda hii thread.Ni ya viwango vya hali ya juu.Hata wana CCM wanapaswa kupongeza hii thread.Mchambuzi ametoa sifa kwa kila anayestahili.Natoa ombi kwa Moderators hii thread iwekwe juu kabisa iwe STICKY ili kila member hapa achangie na kutoa maoni yake kwenye hili suala muhimu la Katiba.
 
Hilo ndilo kundi gani?
Hongereni CDM kwa kushindwa kufanya SWOT dhidi ya chama tawala ili muweze kuwashawishi wananchi vizuri 2015!
Suala la katiba limeshafanyiwa kazi na CCM...2015 mtakuja na sera gani????

Subiri uone, na umwombe Mola akupe uhai ili siku ikifika uweze kuona ukweli, ila huo mrija wa asali na maziwa ya tz ukikukatikia utatia akili tu siku moja.

Chadema ni Chuo kitawafundisha sana tena sana. tusubiri na tuone.
 
Naunga Mkono kuwalaani wote waliokosa uzalendo na nchi yao. Walaaniwe wao na vizazi vyao, wasipate nafasi za kuongoza chochote zaidi ya familia zao wenyewe.
 
Pongezi za dhati zimuendee Regia Mtema kwa kuibua hoja hiyo kwenye kikao cha CHADEMA hoja ya kumuona rais Hakika sitakusahau dada Regia ijapokuwa umetanualia mbele ya haki RIP
 
pongezi zangu zawaendea wazee wetu wa heshima sana ndani ya nchi wazee joseph sinde warioba na salim ahmed salim kwa kufanikisha hili.

Aidha pongezi za pekee ziwaendee vijana kote nchini pamoja na jf kwa kusimama kidete muda wote katika hili. Hata hivo vijana tusilale bado mapambano.

Kwa mara ya kwanza nawapongeza pia rais kikwete, dr kashillila, kichaa wetu ndugai pamoja na wabunge wa ccm kwa kuonyesha uzalendo katika hili na kubwa zaidi ni kule kutambua kwamba yote juu ya yote, taifa kwanza!!!!!!!

mwisho natoa laana kubwa kuliko zote kwa spika wa bunge anne makinda, mungu amlaani milele kwa kuweka jitihada za makusudi kukwamisha mambo ya msingi bungeni alaaniwe yeye na kizazi chake chooote kama kipo maana ninamashaka kama anandugu huyu mama!
 
Pamoja na pongezi tunazoendelea kumimina humu, naona itakuwa vyema na haki sasa kuiunga mkono cdm kwa dhati, kwa hali na mali ili kuwaongezea nguvu zaidi. Mfano tuhamasishe vijana na wote wenye uchungu na nchi hii kununua kadi za CDM na kuchangia chote kitu mara kwa mara kwa lengo la kufanikisha usambazaji wa elimu ya uraia huko vijijini - 2015 siyo mbali jamani na watu wana kiu ya kuhubiriwa 'Habari njema'

Ni wazo tu.

Sio kununua kadi tu na tutagombea katika majimbo kwa nguvu zote ili kuhakikisha pale alipo ccm anabwagwa. 2015
 
Hilo ndilo kundi gani?
Hongereni CDM kwa kushindwa kufanya SWOT dhidi ya chama tawala ili muweze kuwashawishi wananchi vizuri 2015!
Suala la katiba limeshafanyiwa kazi na CCM...2015 mtakuja na sera gani????

Amka kama wewe ni kijana, huu sio muda wakushabikia mambo yasio na msingi. Katiba ni kwa maslai yako wewe watoto wako na watanzania kwa ujumla. Rais angalau amefunguka macho na kuona zaidi ya tumbo lake na maslai ya chama chake. Kama CDM itaendelea kuweka maslai ya Taifa mbele kama jinsi ilivyofanya kwenye swala hili, wananchi wataipeleka ikulu ili ifanye zaidi na kwa ubora zaidi ikisaidiwa na dola.
 
Hizi ndio thread za viwango vya JF ambazo zimekuwa adimu sana kipindi hiki, Nawaomba memba wenzangu bila kujari kwamba Thread inawapongeza Chadema ninachokiomba tuwe na uandishi na uchangiaji wa namna hii.
Hongera zako mleta mada, nimependa ulivyojipanga kuwasilisha mada yako, na ninamualika Pdidy wa humu JF aje kujifunza namna bora ya uandishi kwenye thread hii. kudos.

Mafisadi washaanza kulegea baada ya nguvu ya umma kupiga makelele mpaka sauti zimekauka. Hongereni sana Makamanda wote wa CDM ukimtoa SHIBUDA. Tusijipe moyo sana lazima tuwe macho kuhakikisha walichopambana mpaka kikafanikiwa tunakitumia ipasavyo bila kuchaniana mashati. Bungeni wamemaliza sasa huku uraiani, wakurugenzi wasipokuwa makini lazima walambwe na mawe, kwa ajili ya hao viwete wa CCM.
 
Bunge endelevu na fikra endelevu, kujenga hoja na kutetea hoja, nguvu ya mshikamano usiotetereka, kuona makosa na kuyarekebisha, waheshimiwa wote wako happy, na sisi sote tumefurahishwa sana, sasa tosonge mbele kulijenga Taifa letu!
 
Kwa kuongezea tu, baba Riz1 itapendeza sana kama walau mara moja kwa mwezi mkakutana na watu wenye mawazo ya kujenga ambao hawaogopi kukuambia ukweli pale unapokosea ili kujenga taifa lao kuliko kuwasikiliza hao wanaokulisha pumba na kasa kila uchao, ili wajaze matumbo yao kama Anna M. Ondoa washauri wasiojielewa kama MKPP, mawaziri wasio na msaada kama WN, Mp, Maig n.k. Watanzania milioni 40 ni mtaji tosha kwako achana na ushauri wa wachumia tumbo.
 
Back
Top Bottom