CHADEMA yatumia mbinu za Mugabe na Jubilee

CHADEMA yatumia mbinu za Mugabe na Jubilee

B.G TANTAWI

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
496
Reaction score
379
Kuna taarifa za Uhakika na sahihi kuwa Chadema imeamua kutumia mbinu kama zile za Mugabe kule Zimbabwe na Jubilee kule kenya ili kuweza kushinda Uchaguzi mkuu wa 2014 na 2015, Mbinu hizo ambazo mpinzani wake alibweteke baada ya kupata Uwaziri Mkuu zilimsaidia sana Mugabe Kushinda Uchaguzi ulioisha juzi, Hata Odinga anaelezwa kubweteka sana baada ya kupata Uwaziri mkuu, wakati wenzake walikuwa vijijini wakichapa kazi.

Baada ya kuwepo taarifa kuwa chadema haipo vijijini na CCM ikawa inatumia hiyo kama kete yake, sasa Chadema imesambaza vijana wake nchi nzima hasa maeneo ya vijijini ili kuweza kujipenyeza na kupenyeza Chama chao huko vijijini, Taarifa kutoka kwa mmoja wa vijana hao ambaye yeye yupo kanda ya ziwa zinasema kuwa Chadema lazima itashinda uchaguzi wa 2014 na ule wa 2015, amesema "Unajua kwa muda mrefu watu wamekuwa wakisema kuwa chadema haipo vijijini ila ipo tu mjini, sasa tumeamua kuanza kazi mapema na hadi kufikia sasa tumeweza kuvuna wanachama wengi sana.

Taarifa za ndani ya chadema zinathibitisha kuwa kwa sasa wanawatumia pamoja na watu wengine vijana waliomaliza vyuo vikuu ili kuweza kufikisha ujumbe vijijini,

Vile vile, katika kuonyesha kuwa Chadema inafanyia kazi maoni ya watu hasa hapa Jamii forums, mtoa habari huyo amesema, "Unajua Katibu mkuu wetu "akimaanisha Dr. Slaa" ni member wa Jamii Forums kwa hiyo kuna uzi uliwahi kuwekwa JF kuwa kwa sasa Chadema itafute wanachama wengine wapya wa vyama vingine hasa hasa CCM badala ya kuhangaika na mtaji walionao kwa sasa, kwa hiyo habari ile ilimgusa sana Dr. Slaa na kuamua kuwapa majukumu zaidi vijana hawa.

Mbinu nyingine ambayo tayari inafanyiwa kazi na Makao makuu ya Chadema ni ile ya kuteua team maalum ya watu 100 ambao kazi yao kubwa wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 itakuwa kufuatilia kwa ukaribu Mchakato wa upigaji kura, kukusanya matokeo kwa ustadi mkubwa na kuangalia na kukusanya taarifa na ushahidi wowote kama au ikiwa kuna dalili zozote za uchakachuaji, hii imefanyika kwa sababu imeonekana kuwa wakati wa uchaguzi kila mtu huwa yupo "busy" jimboni kwake.
 
Hili ni jukwaa la great thinker ur not among of them toa ushudu huuu
 
unatunga habari zako za umbea halafu unajidai umepata toka chadema unapoteza mda wako tu.
 
Chadema hawafanani na Mugabe wala Jubilee ila wanafanana na Odinga na Tshvangilai maana wote ni vibaraka wa wazungu magharibi kama chadema.
 
Book 7 group mbona mnamshambulia mleta mada kama nyuki? Yeye ameeleza kinachofanywa na CHADEMA. CHADEMA imekuwa na busara kupeleka vijana vijijini ili kukinadi chama na sera zake wakati CCM imechagua kutumia hela nyingi kuwatuma vijana JamiiForums ili kutetea ujinga wa chama chao. Hii ni poor strategy kwa upande wa CCM kwani hapa JF hakuna anayeweza kudanganywa kwa propaganda za kijinga na kina Ritz, Lizbon, Wema_1, Marcopolo, na book 7 group lote. Mkitaka CCM ipate support zaidi na nyie nenda vijijini muwaeleze wananchi CCM imewafanyia nini na inategemea kuwafanyia nini in future. Lakini kukaa mbele ya keyboard na kumkashfi Dr. Slaa na uongozi wa CDM haiwasaidii hata kidogo.

Kama mna masikio mmesikia.

Tiba
 
Book 7 group mbona mnamshambulia mleta mada kama nyuki? Yeye ameeleza kinachofanywa na CHADEMA. CHADEMA imekuwa na busara kupeleka vijana vijijini ili kukinadi chama na sera zake wakati CCM imechagua kutumia hela nyingi kuwatuma vijana JamiiForums ili kutetea ujinga wa chama chao. Hii ni poor strategy kwa upande wa CCM kwani hapa JF hakuna anayeweza kudanganywa kwa propaganda za kijinga na kina Ritz, Lizbon, Wema_1, Marcopolo, na book 7 group lote. Mkitaka CCM ipate support zaidi na nyie nenda vijijini muwaeleze wananchi CCM imewafanyia nini na inategemea kuwafanyia nini in future. Lakini kukaa mbele ya keyboard na kumkashfi Dr. Slaa na uongozi wa CDM haiwasaidii hata kidogo.

Kama mna masikio mmesikia.

Tiba
hoja yako haishangazi maana hata sura yako kwenye picha ionekana ni "manka" aikambe!
 
Ambaye hataki kuamini hajalazimishwa! Uzuri mimi sina Chama chochote cha siasa, habari hiyo ni sahihi, hata saddam hussein wakati majeshi ya marekani yameingia Bagdad, waziri wake aliuambia ulimwengu kuwa" Hapana, hawajaingia, wakiingia tu tunatumia Silaha za maangamizi" bomu liliporushwa karibu yake akakimbia, kwa hiyo siwezi kuwalazimisha kuamini au kutoamini.

Cha msingi CCM nayo ibuni mikakati yake, shauri zenu.
 
Chadema hawafanani na Mugabe wala Jubilee ila wanafanana na Odinga na Tshvangilai maana wote ni vibaraka wa wazungu magharibi kama chadema.

Bora wazungu maana ndio waliotutawala kuliko wachina na wasomali wanaomaliza Tembo wetu
 
Hili ni jukwaa la great thinker ur not among of them toa ushudu huuu

Unajua maana ya Great Thinker wewe? wakitumwa GT. na wewe utakuwemo mkuu? kwanza sifa ya Great thinker ni kuwa, Lazima athibitishe kwa vitendo kuwa yeye ni Great thinker! sasa wewe kwa hiyo post yako u-Great Thinker wako upo wapi?
 
Book 7 group mbona mnamshambulia mleta mada kama nyuki? Yeye ameeleza kinachofanywa na CHADEMA. CHADEMA imekuwa na busara kupeleka vijana vijijini ili kukinadi chama na sera zake wakati CCM imechagua kutumia hela nyingi kuwatuma vijana JamiiForums ili kutetea ujinga wa chama chao. Hii ni poor strategy kwa upande wa CCM kwani hapa JF hakuna anayeweza kudanganywa kwa propaganda za kijinga na kina Ritz, Lizbon, Wema_1, Marcopolo, na book 7 group lote. Mkitaka CCM ipate support zaidi na nyie nenda vijijini muwaeleze wananchi CCM imewafanyia nini na inategemea kuwafanyia nini in future. Lakini kukaa mbele ya keyboard na kumkashfi Dr. Slaa na uongozi wa CDM haiwasaidii hata kidogo.

Kama mna masikio mmesikia.

Tiba

Tena wakae wakijua kwamba CDM ina makamanda wamo humu jf wakichangia toka vijijini,mfano mimi hapa natoka madibira mkoani mbeya naelekea Mlalo Tanga.
 
Unajua maana ya Great Thinker wewe? wakitumwa GT. na wewe utakuwemo mkuu? kwanza sifa ya Great thinker ni kuwa, Lazima athibitishe kwa vitendo kuwa yeye ni Great thinker! sasa wewe kwa hiyo post yako u-Great Thinker wako upo wapi?

Waambie hao,hawajui GT must think big? Kama hayataki kwanza ni vema ili mchwa wa CDM umalizie msingi na ccm wajenge msekondari.
 
Hizo ni opinion zako mleta mada ila kaa ukijua CCM bado inanguvu na bado inauwezo mkubwa wakutetea viti vyake na kwakila chaguzi zitazotokea hapa nchini hata Chadema ifike chini ya bahari bado CCM kila eneo ishaota mizizi na haiwezi ng'olewa kwa upepo wa mvua za vuli wala kimbunga cha Katrina...KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Mdharau mwiba huota tende. Juzi nikiwa njia nimeshangaa kuona bendera za CDM njia nzima. Na zilongezeka sana kuanzia Sherui kuja Singida eneo la misigiri ndo baraa. Hiyo ni picha halisi kuwa hawa CDM kwa sasa si wa kubeza hata kidogo. Kinana akimaliza ziara arudi kwa barabara ajionee kazi ya CDM huko vijijini.
 
Back
Top Bottom