CHADEMA yasisitiza kufanya maandamano kesho ya amani

CHADEMA yasisitiza kufanya maandamano kesho ya amani

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,917
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA kimesisitiza kwamba maandamano ya amani ambayo yalipangwa kufanyika kesho nchi nzima yatafanyika.

Akizungumza na MwanaHalisi Online, Edward Simbeye, katibu mwenezi wa Baraza la Vijana la chama hicho (BAVICHA), amesisitiza kuwa maandalizi kwa ajili ya maandamano hayo yanaendelea vizuri na tayari chama hicho kilishaandika barua kulitaarifu jeshi la polisi kuhusiana na uwepo wa maandamano hayo katika kila mkoa nchini.

Aidha, kiongozi huyo amesema kuwa mpaka muda huu bado jeshi hilo halijajibu barua ambayo chama hicho kimeliandikia na kuongeza kuwa maandamano hayo yatafanyika hata kama jeshi hilo litakuwa halijajibu barua yao mpaka kufikia siku ya kesho.

“Maandalizi yanaendelea vizuri na hapo kesho tutatoa muongozo kwa wanachama wetu na wananchi kwa ujumla kuhusiana na mahali ambapo maandamano hayo yataanzia na kuishia katika kila mkoa nchini.” amesema Simbeye

Akifafanua kuhusiana na tabia ya jeshi la polisi kuzuia kufanyika kwa maandamano kwa sababu mbalimbali, Simbeye amesema kuwa maandamano ni haki ya kikatiba na jeshi la polisi lina wajibu wa kulinda wananchi ambao wanatumia haki yao ya kikatiba kufanya maandamano na si kuzuia maandamano na kuongeza kuwa maandamano hayo yatafanyika hata kama jeshi hilo litazuia maandamano hayo.

Wiki iliyopita, baraza hilo la vijana lilitangaza kuwepo kwa maandamano ya amani siku ya kesho ambayo waliyapa jina la “Black Thursday” yenye lengo la kushinikiza kuwepo kwa haki za kisiasa, kiuchumi, utawala wa sheria pamoja na haki za binadamu nchini.
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesisitiza kwamba maandamano ya amani ambayo yalipangwa kufanyika kesho nchi nzima yatafanyika.

Akizungumza na MwanaHalisi Online, Edward Simbeye, katibu mwenezi wa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha), amesisitiza kuwa maandalizi kwa ajili ya maandamano hayo yanaendelea vizuri na tayari chama hicho kilishaandika barua kulitaarifu jeshi la polisi kuhusiana na uwepo wa maandamano hayo katika kila mkoa nchini.

Aidha, kiongozi huyo amesema kuwa mpaka muda huu bado jeshi hilo halijajibu barua ambayo chama hicho kimeliandikia na kuongeza kuwa maandamano hayo yatafanyika hata kama jeshi hilo litakuwa halijajibu barua yao mpaka kufikia siku ya kesho.

“Maandalizi yanaendelea vizuri na hapo kesho tutatoa muongozo kwa wanachama wetu na wananchi kwa ujumla kuhusiana na mahali ambapo maandamano hayo yataanzia na kuishia katika kila mkoa nchini.” amesema Simbeye

Akifafanua kuhusiana na tabia ya jeshi la polisi kuzuia kufanyika kwa maandamano kwa sababu mbalimbali, Simbeye amesema kuwa maandamano ni haki ya kikatiba na jeshi la polisi lina wajibu wa kulinda wananchi ambao wanatumia haki yao ya kikatiba kufanya maandamano na si kuzuia maandamano na kuongeza kuwa maandamano hayo yatafanyika hata kama jeshi hilo litazuia maandamano hayo.

Wiki iliyopita, baraza hilo la vijana lilitangaza kuwepo kwa maandamano ya amani siku ya kesho ambayo waliyapa jina la “Black Thursday” yenye lengo la kushinikiza kuwepo kwa haki za kisiasa, kiuchumi, utawala wa sheria pamoja na haki za binadamu nchini.


Hivi hawa jamaa hawana matatizo mengine? I mean hata tu kusaidia waototo wao home work?
 
Police hawajajibu kwa kuwa bado wanasubiri maagizo ya IGP. IGP nae anasubiri Waziri mwenye dhamana aseme kabla hajawaagiza watu wake.

Waziri mwenye dhamana na yeye anasubiri msg aliyomtumia mwenye Nchi ijibiwe maana kwa hofu na woga alionao, anagwaya hata kupiga simu jumba jeupe kuomba mwongozo kwa kuhofia kuitwa mpumbavu. One man show ni tatizo kubwa.
 
Hakuna tamko LA CHADEMA hata moja liliwahi kutekelezwa hebu watuambie M4C iko wapi? Operation Sangara iko wapi? Ushindi SAA NNE asubuhi ya Lowasa iko wapi? Maandamano ya Kupinga Udikteta yako wapi?

Maandamano ya TLS yaliyosisitizwa na Tundu Lissu Juzi yako wapi? Maandamano ya Kuziba Midomo bungeni yako wapi? UKAWA yenyewe iliishia wapi kama kila Chama kilisimamisha mgombea uchaguzi wa mwaka 2015, " Ukistaajabu ya Mbowe utashangaa ya Lissu
 
U. C. H. O. C. H. E. Z. I itatafsiriwa hivyo na watu wakiandamana tutegemee selo kujaa kesho maana tatizo bwana yule hadi sasa hajatoa jibu na ndio maana polisi wanashindwa wajibu nini
 
hivi nchi hii ina selo za kutosha? i mean watakua watu wengi, halafu wote wanahitaji kushikwa!
sipati picha!
 
Labda itakuwa ni maandamano ya kushinikiza serikali imruhusu Wema aendeelee kubwia Unga
 
Back
Top Bottom