OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,336
MGOMBEA wa kiti cha uwakilishi wa Jimbo la Uzini, mjini Zanzibar kupitia tiketi Chadema, Ali Mbaruku,amewasilisha pingamizi akipinga kuteuliwa kwa Mohammed Raza wa CCM, kuwania nafasi hiyo.
CCM imemteua mfanyabiashara huyo, upeperusha bendera yake katika uchaguzi mdogo wa kiti hicho unaotarajiwa kufanyika Februari 12 mwaka huu.
Hata hivyo jana, mgombea wa Chadema, aliwasilisha pingamizi dhidi ya Raza.Pingamizi hilo lililowasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo la Uzini ambaye ameombwa kutengua uteuzi wa Raza kuwa mgombea wa nafasi hiyo kupitia chama kinachotawala.Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari,pingamizi hilo linatokana na hati ya kiapo cha Raza cha kumruhusu kuwania nafasi hiyo.
Mgombea wa Chadema, amesema kuteuliwa kwa mwanachama huyo wa CCM kinapingana na Sheria ya uchaguzi namba 11/1984 Kifungu cha 46 (3) kwa madai kuwa Raza hakidhi vigezo.Taarifa hiyo ilifafanua kwamba sababu za kumwekea pingamizi mgombea huyo ni kiapo cha muombaji au mgombea huyo wa CCM kushindwa kukidhi matakwa ya kisheria za viapo.
Ilisema pamoja na mambo mengine, hakuna kumbukumbu za namba zinaonyesha stakabadhi halali za malipo.
Taarifa hiyo pia ilisema mlaji kiapo hakulipa malipo halali kwa mujibu wa sheria na wala hakuomba nafuu.
Kiapo cha muombaji kwa nafasi hii ni kinyume cha sheria za viapo Zanzibar pamoja na kukosa stempu halali, lakini pia ni kinyume na matakwa ya sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, ilisema.
MWANANCHI.
CCM imemteua mfanyabiashara huyo, upeperusha bendera yake katika uchaguzi mdogo wa kiti hicho unaotarajiwa kufanyika Februari 12 mwaka huu.
Hata hivyo jana, mgombea wa Chadema, aliwasilisha pingamizi dhidi ya Raza.Pingamizi hilo lililowasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo la Uzini ambaye ameombwa kutengua uteuzi wa Raza kuwa mgombea wa nafasi hiyo kupitia chama kinachotawala.Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari,pingamizi hilo linatokana na hati ya kiapo cha Raza cha kumruhusu kuwania nafasi hiyo.
Mgombea wa Chadema, amesema kuteuliwa kwa mwanachama huyo wa CCM kinapingana na Sheria ya uchaguzi namba 11/1984 Kifungu cha 46 (3) kwa madai kuwa Raza hakidhi vigezo.Taarifa hiyo ilifafanua kwamba sababu za kumwekea pingamizi mgombea huyo ni kiapo cha muombaji au mgombea huyo wa CCM kushindwa kukidhi matakwa ya kisheria za viapo.
Ilisema pamoja na mambo mengine, hakuna kumbukumbu za namba zinaonyesha stakabadhi halali za malipo.
Taarifa hiyo pia ilisema mlaji kiapo hakulipa malipo halali kwa mujibu wa sheria na wala hakuomba nafuu.
Kiapo cha muombaji kwa nafasi hii ni kinyume cha sheria za viapo Zanzibar pamoja na kukosa stempu halali, lakini pia ni kinyume na matakwa ya sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, ilisema.
MWANANCHI.