nyie cdm kwa kweli mnatupa shida sana... Ili mradi tu mtimize ile ahadi yenu ya nchi kutotawalika... Na habari zilizopo ni kuwa mmekula njama ya kudhamisha meli iliyokuwa ikielekea znz... Na hii kulingana na uchunguzi tuliofanya imebainika kuwa mliona wivu kwa jinsi ya serikali ya bara na znz ilivyolighulikia kwa umakin na uchunguz wa hali ya juu ikiambatana kuwawajibisha wote waliosababisha ajali ya MV SPICE..
Our take: Plz cdm achen kula njama ya kuzamisha vyombo vya baharini.. Uchunguz unaendelea ukiongozwa na kamanda kova.. 2nahuakika 2tawatia nguvuni 2 cdm...
Tatizo la ccm na serikali yake wamesahau historia, historia ina vipindi vifuatavyo-
1. kipindi cha ujinga/matumaini- watu huvumilia shida, ukiukaji wa haki na kuwapa watawala muda ili waweze kubadili hali ya uchumi na haki za raia kidemokrasia
2. kipindi pili ni cha kuhoji - watu wanapoona hakuna maisha bora kwa kila mtanzania, huanza kutathmini rasilimali nchi ilizonazo na matumizi yake na kisha kuanza kuhoji uadilifu, ufisadi na udhaifu wa uongozi wa chama na serikali yake
3. kipindi cha mwisho uvumilivu huisha katika hili huwa kuna vipindi viwili tofauti vya mpito-
3.1 kipindi cha kudai kupitia sanduku la kura- kipindi hiki watu huamua kufanya mabadiliko kupitia njia ya amani bila kumwaga damu, hapa huwa na matumaini kuwa suluhisho pekee kwao ni kukiondoa chama kilichopo madarakani kwa njia ya kura. watanzania wamejaribu kufanya hivyo mwaka 1995-2010 lakini matokeo yameendelea kuchakachuliwa na ushindi kupewa chama cha ccm
3.2 kufanya mapinduzi- hapa watu huwa wamepoteza matumaini na sanduku la kura kuwa linaweza kuwasaidia kubadili chama na serikali yake. Hii njia siipendi kabisa kwani huleta umwagaji mkubwa wa damu kama ilivyotokea Tunisia, Misri, Syria, Marekabi miaka ya 1700, zimbabwe, kenya, mapinduzi ya Zanzibar na nchi nyingine nyingi duniani.
wasiwasi wasi wangu ni kuwa elimu za wana.ccm na vichwa vyao haitaki kuikubali historia ambayo ipo well documented kwenye vibabu vingi duniani hata vingine wanacham wa ccm wanavyo na wamesoma. kinachonishangaza ivi ccm wakitupeleaka katika vita vya wenyewe kwa wenyewe wanadhani wao watakuwa salama?
ushauri wangu kwa ccm na serikali yake walione hili, wajue ni desturi ya binadamu yeyote kupenda mabadiliko hata kama hayana msingi kwake. Ndio maana ziko nyumba ukiingia zamani walikuwa wanatumia pikipiki, sasa hivi wana uwezo wa kununua magari unakuta wamenunua magari ya aina mbalimbali makubwa kwa madogo. hata mengine unaweza kumuuliza endapo anayatumia atakwambia hakumbuki lini aliliendesha/alilitumia. ukimuliza kama hulitumii inakuwaje ulinunua jibu utakalopewa halitakuwa mbali na alipenda kuwa na gari tofauti na la mwanzo.
Namwomba Mungu ccm na Serikali yake ipewe masikio wayasikie haya na kuyatendea kazi ili waache historia ya kufanya kazi yake