CHADEMA yakarabati nyumba ya bibi kizee Mwanza.

CHADEMA yakarabati nyumba ya bibi kizee Mwanza.

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,328

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kata ya Igoma, jijini Mwanza, imejitolea kukarabati nyumba ya bibi kizee, Magdalena Thomas (64), mkazi wa Soko la Chini Igoma, iliyokuwa imebomoka na kuhatarisha usalama wa maisha ya familia hiyo.

Msaada huo umekuja baada ya viongozi, wanachama na mashabiki wa CHADEMA kata hiyo ya Igoma, kutembelea na kujionea jinsi familia hiyo ya watu 12, inavyonyeshewa mvua na kukesha ikiwa imesimama.

Wakizungumza juzi na waandishi wa habari kwenye mji wa bibi kizee huyo, Katibu mwenezi wa CHADEMA Kata ya Igoma, George Said Lujina, na mwenyekiti wa chama hicho kitengo cha Movement fo Change (M4C), kata hiyo, Ezekiel Nkuba, walisema msaada huo umetolewa Novemba 17 mwaka huu, baada ya kuguswa na tatizo hilo.

Akifafanua zaidi kuhusu msaada huo, George alisema, walipata taarifa kutoka kwa wasamalia wema jinsi familia hiyo inavyoteseka, hivyo kuamua kuchangishana fedha.
“Kama inavyofahamika kwamba CHADEMA ni chama kinachojali wanyonge. Baada ya kupata taarifa, tulichangishana fedha kisha kwenda kufanya ukarabati wa nyumba hiyo sisi wenyewe na kwa gharama zetu.

“Tulifika tukakuta bibi ana watoto watatu na wajukuu zake wanane wanalala kwenye chumba kimoja. Chumba chenyewe kina bati moja tu zima, mengine yameoza na kuchanikachanika. Mvua inanyeshea ndani, na ikinyesha usiku hakuna kulala, wote wanaamka na kusimama,” alisema George.

Bibi Magdalena alieleza kwa furaha msaada huo akikishukuru chama hicho. Alisema msaada aliopewa na CHADEMA hauelezeki, kwani walikuwa wanalala watu 12 katika chumba kimoja, na walikuwa wakiumwa na panya na mbu usiku kucha, na mvua inapokuja wanalala huku wamesimama.

“Kwanza sikuamini nilipoona watu wamekuja nyumbani hapa na vifaa vya ujenzi. Nilitaka niwasaidie angalau hata kusogeza bati na maji, wakaniambia wewe kaa tu bibi tuachie kazi hii sisi.

“Siku hiyo sikulala kabisa, maana nilikuwa na furaha sana. Wamekarabati na kupatikana vyumba viwili ambavyo sasa mimi nalala huku, wanangu wakubwa na wajukuu wanalala chumba kile,” alisema bibi kizee huyo, Magdalena huku akiiombea CHADEMA itawale mwaka 2015.


Imeandikwa na Sitta Tumma
Source: Tanzania Daima
 
asante sana kwa taarifa nzuri chadema chama makini kinachojali wananchi siyo maccm majambazi na wanafiki wakubwaaa
 
haha :CDM wangejisahau wakasema kuwa watwkwenda fanya kesho..Usiku huu lumumba ingeahamia huko.tuiwahi mvalisha matonya bendera ya NCCR ili kujizua na jua,dkk km 10 hivi,CCM walijaza bendera na hela ktk daraja lote.
 
Bora wewe umetujuza mambo ya kimaendeleo na ustawi wa jamii mana thread nyingi zimejaa ZITTO...blah blah blah.....Mbowe....cdm.....blah blah blah....hadi ubongo unalewa porojo hizi.
 
Miaka 64 sio bibi kizee lakini japo ana qualify kuitwa bibi. Huyo bado ana nguvu zake
 
Asanteni Chadema na makamanda wa Mwanza kwa kufanya shughuli za kijamii,tuwaache wanafiq masisiem na jangili wao eti wanapanda mitumbwi mto ruhuhu...
 
Chadema itastawi zaidi Igoma hata bila ya msaliti Chagulani. makamanda kazi tu. hakuna kulala mpaka kieleweke.
 
kwa hili natoa pongezi za dhati, hizi ni salamu tosha kwa wapenda maendeleo. muendelee kuonyesha moyo wa upendo na amani kwa watanzania hasa wanyonge na waliokosa mtetezi, hii ndiyo maana halisi ya siasa safi, hii ndiyo maana halisi ya chama cha maendeleo (CCM) fanyeni kwa vitendo na si maneno matamu yenye matumaini kila kukicha!
Hakika kwa hatua hii moja iliyofanyika, zikifanyika nyingi kama hizi kura zangu tatu muhimu ( rais, mbunge na diwani) ukiacha ya serikali za mitaa mtazipata.....
 
Sasa 2015 nisipoipigia chadema kura nitakipigia chama gani? chadema iko juu.
 
Hapa huwezi kuwaona magamba
cc Ritz,
 
Last edited by a moderator:
Bibi yangu Magdalena,rais wako 2015 ni Lowassa, wape shukrani wasepe mbele kwani ilishasemwa "tenda wema sepa zako, huo msaada hadi umeletwa jamii forums! Gawiza mayo!
 
Back
Top Bottom